SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA MKUU WA MAJESHI YA ULINZI KUFUATIA AJALI YA HELIKOPTA ILIYOTOKEA TAREHE 9 JUNI, 2008

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametumia salamu za rambirambi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange kufuatia kifo cha watu sita, wakiwemo marubani wawili, mafundi wawili na abiria wawili waliofariki tarehe 9 Juni, 2008 baada ya helikopta waliyokuwa wakisafiria kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam kuanguka katika eneo la Oljoro mkoani Arusha

“Nimesikitishwa sana na vifo hivyo vya askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ambao walitoa mchango mkubwa sana wa kuhakikisha kuwa ulinzi na usalama unadumishwa wakati wa mkutano wa Leon H. Sullivan na hivyo kufanikisha na kuiletea nchi heshima”, amesema na kuongeza “Kwa kweli tumepoteza wazalendo na wachapa kazi hodari, natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo,” Ameongeza.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 10, 2008

    Poleni kwa wote waliopatwa na msiba huu (familia na wa-Tanzania wote)!

    Kuna pia habari hii kutoka Khartoum:

    By MOHAMED OSMAN, Associated Press Writer

    KHARTOUM, Sudan - A plane carrying about 200 passengers apparently veered off a runway late Tuesday and burst into flames. It was not immediately clear whether there were casualties.

    An Associated Press reporter at the scene said the plane arriving from Amman, Jordan apparently veered off the runway as it landed in Khartoum and then burst into flames. It was not immediately clear what airline was involved.
    Ambulances and fire trucks were seen rushing to the scene.

    Na nyingine ndogo nchini Kenya pia imeanguka na kuua Waziri na Waziri Mdogo!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 10, 2008

    hao marehemu hawana majina?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...