christine mosha a.k.a seven (shoto) na vanessa mdee ni wabongo wanaofanya kazi mtv kanda ya afrika ya kusini ambapo seven yuko kituo cha dar na vanessa anafanyia sauzi. hawa ni baadhi ya nyota wetu wenye vipaji vya utangazaji wanaopasua anga za kimataifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 19, 2008

    seven i would recommend apricot scrub.it would make you look shiner and take out all the clots of acne that you are enduring.you are very BEAUTIFUL!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 20, 2008

    Dada wa kushoto mzuri kwa asili....ila ukitumia Proactive Step 1,2 & 3 utapata chocolate complexion ya nguvu.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 20, 2008

    Ndumba Bungeni: Mapolisi wafikia patamu

    2008-06-19 18:50:26
    Na Mwandishi Wetu, Jijini


    Baada ya kuzua gumzo kubwa Bungeni na hata nje ya chombo hicho cha kutunga sheria, hatimaye lile soo la kudaiwa kufanyika kwa mambo yanayoashiria ushirikina ndani ya Ukumbi wa Bunge limefikia patamu baada ya Polisi kueleza kuwa wako katika hatua nzuri ya kulipatia majibu muafaka.

    Utamu wa mahala palipofikiwa katika sakata lenyewe, unatokana na taarifa `latest` za Polisi kueleza kuwa kumbe, hadi sasa wameshatuma vijana wao wa kazi ambao wamekusanya sampuli za vumbi linalodaiwa kuwa na madubwana ya namna ya unga yaliyokutwa ndani ya ukumbi huo na kupelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili baada ya hapo, kila kitu kiwekwe bayana kuhusiana na sakata hilo.

    Hata hivyo, hatua ya Polisi inatokana na hofu waliyokuwa nayo baadhi ya wabunge kuwa pengine, kuna watu wamenyunyiza unga unga wenye sumu, hasa baada ya kuwepo kwa taarifa za kuonekana watu kwenye kamera za ndani ya ukumbi wa Bunge wakizunguka kwenye viti vyao.

    Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Bw. Peter Kivuyo, amesema kuwa vumbi lilofagiliwa katika ukumbi wa Bunge, tayari limeshafikishwa katika ofisi za Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi na hatimaye kujua kama limechanganyika na aina yoyote ya dawa.

    Kaimu Mkurugenzi huyo wa Upelelezi akasema kwa kawaida, vumbi na taka zinazokuswanywa bungeni hutupwa, lakini kutokana na madai ya kuwepo kwa hofu hiyo, walilichukua vumbi hilo na kisha kulisafirisha hadi Jijini Dar.

    Hata hivyo, akasema watu wanaodaiwa kushiriki katika zoezi hilo la kumwaga unga bungeni hawakuhojiwa na Makao Makuu yao na kuongeza kuwa kazi hiyo inafanywa na Polisi mkoani Dodoma.

    Aidha, Kivuyo akawaahidi Watanzania kuwa hadi sasa, uchunguzi kuhusiana na sakata hilo unaendelea na mambo yote yataanikwa, kadri ukweli utakavyokuwa unapatikana.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samwel Sitta, ni kwamba Jumanne ya wiki iliyopita, alipata taarifa kuwa kamera za usalama bungeni ziliwaonyesha watu wawili wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge usiku, huku wakipita katika viti mbalimbali vya wabunge.

    Hata hivyo, Spika akawahakikishia wabunge kuwa hakuna wasiwasi wowowte kuhusiana na usalama ndani ya ukumbi huo na kuwaambia kuwa suala hilo liko mikononi mwa wana usalama kwa uchunguzi zaidi.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 20, 2008

    MMEPENDEZA JAMANI AKAA..DADA WA KUSHOTO NANIHII ZAKO KALI KWELI MPAKA NANIHII ZINATOKA USONI..NIMEKUBALI

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 20, 2008

    samahani kwa kuwaulizeni swali, ila naomba sana msaada wenu, eti katika picha kama hapa, mwandishi anaposema kushoto anamaana kushoto kwa hao waliopigwa picha au kushoto kwa sisi watazamaji wa picha?
    mfano picha hii, alie kushoto ndie mwenye nyeusi au njano?

    otherwise nimewapenda wasichana wako cute na wanaonekana ni brave young girls.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 20, 2008

    Haya wadau kwa kuua wameshaanza, nami nataka kuuliza huyu Saba ana bwana? Hebu tupeni 411, mimi niko tayari kuoa? Au dada bado ana dunda?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 20, 2008

    Seven please get in touch with me. My mail, alex_lyimo@yahoo.com

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 20, 2008

    Hao mabini ni wazuri na bado wadogo msiwachulie eti mnataka kuwaoa. nyie endeleza libeneke la utangazaji achana na hao wazushi.

    Nantombe
    Moshi

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 20, 2008

    hi christina mosha looks so fat nowdays,remember you since jitegemee high school,you were real modal by then,natumai na kautu uzima kameanz kukunyemelea sasa!
    hongera kwa mafanikio katika kazi from clouds 88.4 up to MTV-AFRICA.we all know u are talented
    congratz Dear Gal!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 20, 2008

    Wakuu wangu heshima mbele kama kawa, ninaomba kuweka mpya kutoka Dodoma:-

    1. Leo asubuhi Mbunge Chenge, alichukuliwa na polisi na kuepelekwa kituo cha
    polisi Dodoma mjini, kwa mahojiano ya muda wa karibu masaaa matatu kuhusiana na
    kitendo alichokifanya majuzi cha kujaribu kuweka "Uchawi" kwa baadhi
    ya wabunge wenziwe ndani ya bunge, kitendo ambacho kilikamatwa na vinasa picha
    vya jengo vilivyomo ndani ya jengo la bunge, Dodoma.

    2. Mheshimiwa Mkapa, kwa mara ya kwanza leo amehudhuria kikao cha siri cha NEC,
    kinachoendelea toka jana usiku, mjini Dodoma, ameonekana akiwa hoi na amechoka
    sana, wachunguzi wa siasa hawaelewi ni kwa nini baada ya Mkapa kukataa kwa
    makusudi kuhudhuria vikao mbali mbali vya cc na NEC vilivyopita, safari hii
    ametokea bila ya taaarifa kuhudhuria kikao hiki, ambacho kimeitwa ghafla sana.

    3. Gavana wa Benki kuuu Bwana Ndulu, kwa mara nyingine aliiitwa mbele ya kikao
    hiki kutoa maelezo mazito sana, kuhusiana na ishu za EPA, na zingine za
    ufisadi, according to the dataz ni kwamba alishambuliwa sana kwa maswali ya
    wajumbe huko ndani.

    4. Hali ya Mbunge Shujaaa Mwakyembe, sio mbaya sana lakini sio nzuri pia, sasa
    hvii ninapooandika yumo njiani kuepelekwa Dar, kwenda kuangaliwa zaidi kiafya
    na wataaalamu wa juu wa afya nchini, inasemekana kuwa chanzo ni sangoma ya
    Chenge.

    5. Kwa niaba ya wananchi wengi hapa, tumewasiliana na Mbunge Kimaro, ili aweze
    kuja na kutupa yanayojiri kulingana na haitma yake kiuongozi na all the ishus
    za siasa za taifa kwa ujumla, tunategmea kupata jibu rasmi baadaye kuhusu
    kupatikana kwake na siku, then tutawasilaina na wakulu wengine hapa na hasa
    mkulu MMMJ.

    Ahsante Wakuu, na Mods naomba ikisha expire iepelekwe popote, ni kuhabarishana
    tu kinachoendelea kwenye siasa za taifa letu!!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 20, 2008

    ... seven aint fat, she has a healhy body. na kuhusu acne, msitumie hili neno kufananisha na chunusi za kawaida. its a skin condition ambayo anaweza kupata mtu yoyote vile, hata wewe unaweza kupata hormone zaka zikichagua kwenda huko and will take years to correct it self.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 20, 2008

    hey seven,
    good to see you going places...
    i remember Ashira girls...
    big up sana tu, and you are beautiful... lets get in touch,
    nilikuwa nimemcoat mdogo wake kidada enzi hizo za ashira.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 21, 2008

    All the best to Tanzanian young girls who are doing great!!!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 21, 2008

    Dada Seven hongera,sura yako ni ya uasilia bila kutumia manjonjo yoyote. Nyie mnaemshauri kutumia madawa ya kung'arisha uso hamumtakii mema,wanga wakubwa nyie!

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 23, 2008

    Kama sijakosea huyu Vanessa Mdee atakuwa mtoto wa marehemu Sammy Mdee... kama ndiye naona amekuwa binti mrembo. Amechukua uzuri wa mama yake sofia. Hongera sana Vanessa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...