kocha abdallah 'scolari' ezza (kwanza shoto, mstari wa nyuma) akiwa na kikosi chake cha fc bongo leo kabla ya kukipiga na algeria


Leo hii vijana wa FC BONGO ya helsinki imewabamiza Algeria goli 6-2 katika mchezo wa mwisho wa kundi B katika mashindano ya HELSINKI PREVENTION CUP.


Timu hii tishio tayari imeshajikusanyia ponti 15 swaaaafi kwa kushinda mechi zote tano na kukolifai kuingia semifainali siku ya jumatano watakapokutana na GUINEA.

Magoli ya FC BONGO yalifungwa na SAMI 2, FRANCIS 1, BOB 2 na EDO 1.
Mungu ibariki TANZANIA,
Mungu ibariki FC BONGO
Mungu Tubariki watanzania woote kwa jumla.

Habari zaidi za maendeleo ya FC BONGO katika mashindano hayo ya HELSINKI PREVENTION CUP utazipata hapa katika blogu yetu hii ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 29, 2008

    Hongera fc bongo, moto ule ule msirudi nyuma, mkishinda nyie ndio tumeshinda Watanzania wote. peperusheni bendera yetu juu huku nyumbani akina Maximo wameshindwa kufanya kweli.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 29, 2008

    siku wakifungwa kimyaa..! lakini hogereni..! ila mkirambwa muwe wa kwanza kutufahamisha!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 29, 2008

    Njooni mcheze na Yanga ndio saizi yenu.Nataraji siku hiyo hawataingia mitini.

    ReplyDelete
  4. Naona Bongo FC mambo mzuka sasa... endelezeni dozi katika Semi.. Tupo pamoja

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 29, 2008

    Wale madogo wawili mmoja mrefu na mmoja mfupi walizungusha kinoma pale kati, na yule mtoto jimmy kwanini siku zote anawekwa benchu tu, jana alikipiga vizuri sana.

    ReplyDelete
  6. huyo scolary aje kuchukua nafasi ya maximo, moto wake si mchezo tunawatakia ubingwa

    ReplyDelete
  7. hongera fc bongo pamoja na kocha mr skorare. kwa kupeperesha bendera ya tz. ulaya.ceepit on ezze.
    mss benn. mariehamn

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...