Marehemu Chacha Wangwe

HABARI TOKA DODOMA ZINASEMA MBUNGE WA TARIME KUPITIA CHADEMA MH. CHACHA WANGWE (PICHANI) AMEFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI ILIYOTOKEA USIKU HUU SHEHEMU ZA KONGWA, MKOANI DODOMA.

KWA MUJIBU WA HABARI HIZO MAREHEMU WANGWE, AMBAYE ALIKUWA AMETOKEA BUNGENI DODOMA AMBAKO ALIHUDHURIA KIKAO CHA ASUBUHI, ALIKUWA NJIANI KUELEKEA DAR KWENYE MAZISHI YA HAYATI MZEE BHOKE MUNANKA AMBAYE AMEFARIKI DUNIA JUMAMOSI HII, AMBAPO LEO ANATARAJIWA KUZIKWA KWENYE MAKABURI YA KINONDONI, DAR.

CHANZO CHA AJALI HAKIJAJULIKANA NA POLISI HUKO KONGWA WAKITHIBITISHA HABARI HIYO IMESEMA MAITI YA MAREHEMU IKO KATIKA DISPENSARI YA KIJIJI CHA KIBAIGWA IKISUBIRI KUPELEKWA HOSPITALI KUU DODOMA KWA HIFADHI NA HUDUMA ZINGINE.
HABARI ZINASEMA MWENYEKITI WA CHADEMA MH. FREEMAN MBOWE LEO ANATARAJIWA KUTOA TAARIFA RASMI YA KIFO HICHO PAMOJA NA MIPANGO YA MAZISHI.

GLOBU HII YA JAMII INATOA MKONO WA POLE KWA WAFIWA KWA NIABA YA WADAU WOTE. ITAENDELEA KUTOA TAARIFA ZA MSIBA HUU MZITO KWA KADRI ZINAVYOINGIA. HIYO NI PAMOJA NA CHANZO CHA AJALI NA ENDAPO KAMA MAREHEMU ALIKUWA NA WATU WENGINE KWENYE HILO GARI, NA HALI ZAO ZIKOJE.


MOLA AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MH. CHACHA WANGWE MAHALI PEMA PEPONI


AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 24 mpaka sasa

  1. Mungu amlaze mahali pema peponi Amen.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 29, 2008

    May Lord rest his soul in peace.

    Mbona ajali ni nyingi sana Tanzania?

    Serious ajali zinaweza kuua watu wengi sana kwa mwaka kuliko hata malaria

    Poleni sana wafiwa

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 29, 2008

    REST IN PEACE.
    wewe ni mwanaume hadi MBOWE ANAKUOGOPA.
    UNGEKUWA MWENYEKITI WA CHADEMA, KWANI USINGEKUWA NA MPINZANI KWENYE UCHAGUZI MKUU CHADEMA DECEMBER.

    ReplyDelete
  4. Mungu aliyemuumba Chacha Wangwe hatimaye amemchukua. Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana libarikiwe. Amen (Ayubu 1:21)
    Poleni sana wafiwa Mungu awape faraja wakati huu wa Majonzi.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 29, 2008

    Sisi tulikupenda lakini bwana amekupenda zaidi. Roho ya Marehemu Chacha Wangwe ipate rehema kwa Mungu na ipumzike kwa amani.. AMEN.
    Nalo Pumziko la milele uwape ee bwana... na mwanga wa milele uwaangazie ..Marehemu wote waliotutangulia wapumzike kwa amani...Amen.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 29, 2008

    Namwomba Mwenyezi Mungu Ailaze Pahali Pema Peponi Roho Ya Marehemu Wangwe. Amina.

    Nawapatia Pole Za Dhati Wanafamilia na Marafiki Wa Marehemu.

    SteveD.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 29, 2008

    bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 29, 2008

    Hakuna mtu mwenye upendo mwingi, kama afae kwa ajili ya mwenzake.Chacha, tutakukosa sana bungeni ulikua changamoto kubwa watanzania wenzako, na utakumbukwa na wapenda haki na maendeleo wote.

    Inna-lilah wainna Illah rajyun.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 29, 2008

    Du! unaweza kukufuru coz ukilinganisha ugomvi wa juzijuzi na jama zake wa chadema na ajali hii...anyway...rip Chacha Wangwe

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 29, 2008

    poleni waheshimiwa wabunge hasa mh Sitta ambaye ameshindwa kujizuia kutoa machozi leo asubuhi wakati akiahirisha kikao cha bunge...wapiga kura wa tarime,wanachama wa chadema.n.k.

    Mungu alimpenda zaidi Chacha...

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 29, 2008

    Jamani Chacha
    Wameku... wameona mwaka 2010 unaimaliza CHADEMA kwa kusema ukweli.
    RIP poleni wanafamilia

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 29, 2008

    My God!
    Mkombozi wa Wana-CHADEMA wasiotoka mkoa wa kule naniiiliii ...Poleni sana sasa changamkeni muendeleze changamoto ya kugombania haki zenu.
    Ulale mahali pema peponi Chacha

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 29, 2008

    Ngoja nifungue Jamii Forum nione mawazo yao maana wazuri sana kusema maovu akifa mhe wa upande wa chama tawala

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 29, 2008

    Inna-lilah wainna Illah rajyun.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 29, 2008

    So sad jamani, RIP CHACHA WANGWE!!MAY ALMIGHT GOD REST HIS SOUL IN ETERNAL PLACE AMEN!

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 29, 2008

    It is really shocking but no way other than accepting what has happened.My sincere condolences to the family and all Tanzanians.
    May God rests the soul of Chacha Wangwe in Eternal Peace. Amen

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 29, 2008

    Mungu aiweke roho ya Chacha Wangwe mahali pema peponi. Amina.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 29, 2008

    WEeee Michuzi acha kutumix mzee wa roiko mchuzi mix wewe tangu lini hii ikawa Globu hebu sema sawasawa Bwana tutakushtaki kwa Ndesanjo Ngasanjika kapisa.


    Mdau

    Makini Makini Sana.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 29, 2008

    RIP Mh. Chacha Wangwe.

    Poleni sana wafiwa kwa msiba huu mzito sana.

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 29, 2008

    RIP Chaha wangwe.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 29, 2008

    Inna Lillah Wainna Ilaih Raajiun

    Kuntakinte.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 29, 2008

    POLE KWA WAFIWA NA WOTE WA KARIBU NA WALIOGUSWA NA MSIBA HUU.

    Hili wazo la Mungu alimpenda zaidi linatoka wapi, wanaoishi Mungu hawapendi? !!!

    Tuwe hai au tumekufa MUNGU anatupenda.

    RIP Mheshimiwa !!!

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 30, 2008

    Tutakukumbuka sana, Mola akulaze pema Amina.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...