Mechi ya leo ilikua ni ile ya Mbwa kala Mbwa, kwani Hao Wanigeria ndio tishio la timu zote katika mashindano hayo, Lakini wabongo wamepania mwaka huu kuwa kombe hilo lazima walifikishe Ubalozini Stockholm wakati watakapozuru huko tarehe 16 august mwaka huu na kuchuana na kilimanjaro fc ya Stockholm.
Fc Bongo mpaka sasa inaongoza katika Kundi A wakiwa na pointi 9, wakifuatiwa na Nigeria na Ageria wakiwa na pointi sita wote na mwisho wakishika mkia Congo na Greece wakiwa na pointi 3 kila mmoja.
Magoli ya Fc Bongo yalifungwa na Ubaldino, Kevin na Zakaria.
Alhamisi Wabongo wanajimwaga tena uwanjani kuchuana na Wagiriki.
Wanaigeria wamefunga mdomo, kiboko ile.
ReplyDeletena mazungu yanini hapo? ina maana hakuna wabongo wakutosha hapo? au ndio ma supervisor wa viwandani!!
ReplyDeleteJamani, mchezo wa jana mlicheza kwa ustadi na nidhamu ya hali ya juu. Nidhamu ya wachezaji inaonekana hata katika hiyo picha mliyopiga. Mnastahili pongezi nyingi sana. Endeleeni hivyo hivyo kombe mtalitwaa na kutupa sifa Watanzania wote.
ReplyDeleteWatanzania wenzangu nawaombeni tujitokeze kwa wingi zaidi siku ya Alhamisi ili kuongeza ushangiliaji hivyo kuinua ari ya wachezaji uwanjani.
Pia michango ya kifedha ni muhimu hata kama ni Euro 5. Mnaona kila siku jezi zinakuja zimefuliwa, madawa, maji ya wachezaji na gharama za kuleta vifaa uwanjani vyote vinalipiwa toka mfuko wa timu ambao haupati ruzuku toka mahali popote bali kwa kujitolea au kwa michango au mauzo ya vinywaji. Tunajivuna tunaposifiwa kila siku kwamba Tanzania ndiyo timu pekee yenye jezi safi na tofauti tofauti. Sifa hizi zinahitaji michango yetu sote.
Viva Tanzania! Aluta Continua! Ushindi ni wetu!
Asanteni.
It's all gud...get it done guyz.
ReplyDelete