chubwi....bibie fatma akidanki shampeni kwa mai hazbendi wake shafii kassim
ndoa ilianzia kwenye mkeka na shaba maeneo ya sea view, dar
shafii akimlisha kwa mahaba mai waifu wake fatuma kipande cha ndafu
shafii akishukuru wageni waalikwa
shafii na mai waifu wake fatuma wakifungua dansi
maharusi katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa daily news na habari leo ambako shafii anafanyia kazi. fatuma ndo kwanza kamaliza udsm na ataanza kazi baada ya fungate
mambo ya vioda kwa sana harusi ya shafii na fatuma ambao wazazi wao wote ni sala tano
shafii na fatuma na wapambe wao mara tu baada ya kuwasili ukumbi wa sherehe wa mgulani jkt
kunywa nikunyweshe





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. hey shafi hongera sana , na mmependeza sana tuu.. nakumbuka ndio mlikuwa ma kaka zetu wa seaview..tumuombe mwenyezi mungu aibariki ndoa yenu.

    mkami- linda
    ottawa-canada

    ReplyDelete
  2. maharusi wamependeza, mungu awape amani na upendo kwenye ndoa yao. ila mbona ukumbi umepambwa kma kenye mikutano ya CCM?

    ReplyDelete
  3. mkamiti Gembe ? na Eva Gembe? na Linda nashukuru sana kwa pongezi zenu ,nami nawatakia maisha mema huko Canada.

    ReplyDelete
  4. mkamiti Gembe ? na Eva Gembe? na Linda nashukuru sana kwa pongezi zenu ,nami nawatakia maisha mema huko Canada.

    ReplyDelete
  5. Hapa kwa kuweka picha nyingi hivi na nikizingatia unavyopenda mnuso na kula, Michuzi utakuwa ulipewa kadi bila kuchanga na huu ndio mchango wako. hongera maharusi
    Natombe
    Moshi

    ReplyDelete
  6. Hongera kaka shafii na dada Fatuma.Mimi ningependa kuwapa wosia mfupi.Tofauti na mlivyokuwa boyfriend/girlfriend,fiancee.sasa mpo kwenye ndoa.Ndoa inahitaji,kuheshimiana,uvumilivu sana na upendo,mara moja moja(HIYO NI MUST) mtakuwa mnakwaruzana kwa sana tu ndani ya nyumba lakini hakuna kupeleka hiyo mikwaruzo nje ya ndoa jitahidini kuimaliza nyie wenyewe ndani ya ndoa yenu.Nawatakia afya njema na maisha yenye furaha.Mungu awabariki

    ReplyDelete
  7. Hongera Shafii kwakuchinja mzee. waache wanaopenda kudownload mafile ambayo hayajulikani source. jihadhalini virus, trojans,spyware,worms wote wamejikita kwenye honey ports ambazo munadhani dili kuzibeba.

    Hongereni na muishi maisha ya upendo wa dhati, manung'ayembe yaulizane.

    G7
    UK

    ReplyDelete
  8. Hongereni sana kwa kufunga pingu za maiha. pia mmependeza sana. ila hiyo picha mmejifunika khanga ni mambo gani tena hayo? au inamaana gani maana kama ninyi ni waislam ilikuwaje tena mvae vazi la kikristo? kwani kama nijuwavyo uislamu hauruhusu mwanamke kuacha mabega wazi mbele ya kadamnasi ispokuwa kwa mmewe tu ndani ya chumba.

    au kama mliona hayo mambo yamepitwa na wakati msingevaa mashungi hayo kabisa na sio kuidhalilisha dini yenu.

    hayo ndiyo maoni yangu asanteni.

    ReplyDelete
  9. kaka michuzi mimi nilikua nataka kujua huyo bi harusi ni fatuma au fatma mana hakuna jina la fatuma katika uislam kuna fatma naomba umuulize mwenyewe asije kuona umemuharibia jina lake fatuma ni jiwe la kuvunjia nyumba linalotumiwa na majambazi. jina liwe fatma.

    ReplyDelete
  10. Hongera sana shafi na fatuma.ilikuwa babu kubwa.

    kwame,london.

    ReplyDelete
  11. ay jamani majina mengine, lol ati Natombe!!

    ReplyDelete
  12. Hongera maharusi mola awadumishie ndoa yao waishi kwa upendo na amani . Walipendeza mashallah

    ReplyDelete
  13. Shafi na mkeo, imekuwaje waisilamu hlafu mnaanza maisha yenu pamoja kwa kuibariki ndowa yenu kwa ulevi au sio ulevi huo kwenye gilasi mnanywishana? i hope not! kumbuka waislamu ni kukumbushana!

    ReplyDelete
  14. wewe anon aug 5,08, 12:49pm hivi jina la fatma au fatuma ni la kiislam ama kiarabu?Nijuavyo kuna waarab ambao sio waislam na wanatumia majina hayo hayo.Majina ya watu,wanyama, ama vitu yanatokana na utamaduni wa sehemu hiyo.Kuna wakristo kibao wanatumia majina ya kina Salma,salmin,fatma,hadija halikadharika kuna waislam wanaotumia majina yajulikanayo kama ya kiislam.Jamani kumbukeni hizi dini zililetwa kwetu na wageni.Waliwa brainwashed mababu zetu ni muda wa kuvumbuka na kuanza kutumia majina yetu ya kinyumbani kama Jakaya kikwete,sekilojo chambua,malota soma, Zamoyoni mogella nk.Kuna nchi kibao za kiafrika watu hawataki kutumia majina ya kizungu,kiarabu wanatumia majina ya kwao.Mimi huwezi juwa natoka wapi majina yangu yote ni ya kibantu mbigiri itakuchoma

    ReplyDelete
  15. Mwinyi hongera sana, I hope life will unfold all goodies to you and your new family. May Allah bless you today and always. Yasini M - UKerewe

    ReplyDelete
  16. FATMA au FATUMA NI MAJINI YA MSHARIKI YA KATI NA WALA SI YA KIISLAM AU KIARABU KWANI KUNA WA-IRAN AMBAO SI WAARABU WANATUMIA MAJINA HAYO, WAHINDI, WAPASITUNI NAKADHALIKA, KUNA PIA WA-KRISTO KIBAO AKINA JUMA, ALI, ABDALAH, SEFU UKIENDA IRAQ UTAWAKUTA, MISRI, PALESTINE, JORDAN, SYRIA, LEBANON, KWA HIVYO JINA SI DINI NI UTAMADUNI WA SEHEMU FULANI. KWA MFANO GAMBIA ASILIMIA KUBWA NI WAISLAM LAKINI HUWEZI KUKUTA MAJINA YA KIARABU KAMA YAPO NI MACHACHE WANATUMIA MAJINA YAO TU. PIA MAJINA KAMA ALEX, EDWIN PIA SI KI-KRISTO NI YA UTAMADUNI WA MAGHARIBI KWANI HATA HUKO MAGHARIBI KUNA WAISLAMU WANAITWA ALEX.

    ReplyDelete
  17. hongera kwa harusi yenu

    Wewe hapo juu jina sio dini lakini mimi binamua yangu anaitwa Fatuma na ni mwislamu sasa sijui wewe ni mwisilamu gani? Kama ulivyoambiwa majina yetu ni sio haya. Haya tuliletewa na waarabu tu.Tungetakiwa tuitwe Manka, Koku, Lusajo, Mwita etc etc hayo ndio majina yetu

    ReplyDelete
  18. Hey Shafi hongera kaka long time mkuu tuliishi pamoja Upanga na School mate wangu Kimbwelu!!! Kwame yuko wapi? Kila la heri kaka katika maisha ya ndoa.
    Pius-Malaysia

    ReplyDelete
  19. NAOMBA KUULIZA HAYO MASODA YOTE HAPO HIGH TABLE NI YA WAHUSIKA WA MBELE HAPO TUU AU NI MBWEMBWE .

    TUBADILIKE WATANZANIA HIGH TABLE HAIMAANISHI KUJAZA MIPOMBE AU MISODA AU MIPOMBE KALI,BORA MUWEKE MUHUDUMU HAPO MBELE AUWAHUDUMIE.

    ReplyDelete
  20. hongera sana Shafi.from walthamstow family.London.

    ReplyDelete
  21. Hongera Shafii kwa hatua hiyo, mmependeza sana na mkeo. nawatakia maisha mema. Nimeona na Kwame ametuma pongezi hapo toka UK nampa hi sana.

    Former neighbor
    Seaview

    ReplyDelete
  22. ??????!!!!!

    ReplyDelete
  23. All the best maharusi in ur marriage life, fatuma used to be my primary school mate playing 'rede' .Now she is married,brilliant. congrats friend.
    lily,
    cardiff, united Kingdom

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...