Mfano wa Jengo Uhuru Heights linalotarajiwa kuwa kubwa na refu kuliko yote jijini Dar litakalojengwa barabara ya bibi Titi Mohamed karibu na makutano ya brabara hiyo na ile ya Ali Hassan Mwinyi na ambalo jiwe lake la msingi liliwekwa na Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda wikiendi ilopita

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Sehemu gani hiyo specifically, Hassan Mwinyi na Bibi Titi sikumbuki vizuri laki zinakutana pale PEUGEOT/SHERATON. Sasa ni wapi hapo linajenga na mmiliki ni nani?

    ReplyDelete
  2. Kama halitatumia mapesa kama ya BOT

    ReplyDelete
  3. Wahakikishe tu linasimama imara siyo kula pesa na kujaza nchanga...

    ReplyDelete
  4. Uhuru Street na Ali Hassan Mwinyi Road hazikutani mahali popote.

    Uhuru inakutana na Bibi Titi pale Mnazi Mmoja.

    Bibi Titi anaendelea na kukutana na Ali Hassan Mwinyi pale Tanganyika Motors.

    Ali Hassan Mwinyi mwishoni anakutana na Kawawa Morocco

    Lakini hapo katikati Ali Hssan Mwinyi hukutana na Kenyatta na Haile Selasie.

    ReplyDelete
  5. Natumaini na parking site zimeshaandaliwa mahali pake au litakua na underground parkings.

    ReplyDelete
  6. Anony wa August 04, 2008 8:47 PM, kwani imetajwa wapi kuwa jengo litakuwepo makutano ya Uhuru na A. H. Mwinyi? Some vizuri, Uhuru ni jina la jengo tu, halihusiani na barabara. Barabara ni A. H. Mwinyi na Bibi Titi.

    ReplyDelete
  7. Naungana na anony wa 1, najiuliza hili jengo litakuwa wapi. Maana Bibi Titi, A. H. Mwinyi na Ohio zinakutana ktk Y-intersection, upande mmoja kuna Parthenon Hall ikifuatiwa na Nyumba ya Sanaa then Movenpick; Upande Mwingine kuna Peugeot House, Bustani (Ilipokuwa Bushtreker Zamani), then TDFL Building na upande wa tatu kuna BP Filing Station na Amref (kama sikosei). Sasa najiuliza hapa whwich one of these buldings itabomolewa. Tusaidie Uncle Michu

    ReplyDelete
  8. Jengo hili litajengwa kati ya UNICEF na jengo lililopo karibu na BP ambalo kuna ofisi za Air India litatazamana na Peugeot House sehemu ya Display ya Pikipiki... Zamani kabla ya kupigwa nyudozz ilikuwa ofisi ya KIBO BREWERIES...
    Mpendakeroro...

    ReplyDelete
  9. Kwa nini uhuru hausi isingejengwa along barabara ya uhuru kulingana na jina.Ningependelea wangelijenga Msimbazi/uhuru,ama mnaonaje wadau?

    ReplyDelete
  10. kwa nini hawa wapanga miji wasiache fikra za kizamani za kuporomosha majengo katikati ya Jiji? Wangeanza kujenga haya majengo nje ya city center. Maeneo kama "fire" kuelekea magomeni,shule ya uhuru kuelekea uwanja wa karume nk.Jamani serikali haikuwasomesha bure.Tumieni mlichojifunza kupanua jiji ili lionekana Kubwa na la kupendeza.

    ReplyDelete
  11. mimi acha nianze kushika mbavu mapema,mara mtasikia kabla hilo jengo halija kamilika limeporomoka chini.sijui tatizo ni ma engineer waliokuwa wanadesa past papers tangu A-LEVEL hadi vyuo vikuu,au huwa ni tamaa inayopelekea kushindwa kutumia pesa kwa kujenga kitu chenye quality inayo stahiki ktk ardhi inayo himili uzito.
    maana hata wanasahau kuweka tahadhari za risk zinazoweza jitokeza baadaye ziwe natunaly occuring kama mvua,upepo n.k ama human induced kama moto n,k na jinsi zitakavyo kabiliwa kuokoa maisha na mali mapema.badala yake husubiri hadi vikitokea ndipo waanze kufikiri chakufanya!!!pumbaff kabisa!!!!

    ReplyDelete
  12. Kuhusu kujengwa kwa jengo hili ni sehemu ya maendeleo ila mimi binafsi napingana na hii staili tuliyonayo ya kujaza majengo makubwa katikati ya jiji huku kukiwa ni miundombinu dhaifu. Mitaro ya maji machafu,maegesho ya magari na barabara havikidhi mahitaji halisi, hivyo kuongeza majengo kama haya ni kuongeza msongamano usio wa lazima. Kwa nini wasiige mfano wa Millenium towers kujengwa kijitonyama hii inakuwa ni changamoto ya maendeleo na katikati ya mji kuachwe kama mji mkongwe. Hivi kweli huu mji wa Dar una manispaa zinazofanya kazi?? Nini kazi ya city planners?? Siombei mabaya ila dalili ni kwamba miaka mitano ijayo itakuwa ni dhahma yote kutokana na kutokuwa na mipango endelevu kutokuwa na mtazamo wa kuona mbele.
    Mayor Kimbisa hana jipya pamoja na uongozi wake wote na manispaa zote ukipita mjini unakuta majengo mapya yasiyo na mbele wala nyuma, linabomolewa jengo lenye uwezo wa makazi ya familia nane linajengwa la kuishi familia zaidi ya ishirini bila kuzingatia miundombinu. Jengo jipya la kuishi familia zaidi ya ishirini chini lina parking za magari yasiyozidi 8 na kuna maduka pia je wanapaki wapi?? Matokeo yake ni misongamano na ukosefu wa parking za kutosha.

    Wakati umefika tufikirie kutanuwa miji yetu na kutafakari kabla ya kutoa maamuzi matatizo kama haya ya mipango duni ya miji ndio yaliyopelekea Nigeria kuhamisha mji mkuu kutoka Lagos kwenda Abuja na kwa kweli ukitizama Abuja imepangika kisawasawa tofauti na Lagos.

    Mungu ibariki Tanzania

    ReplyDelete
  13. Mimi naomba hiyo contract wasipewe wahindi maana wahindi bwana kazi zao low quality coz boss wa kampuni atataka yeye mwenyewe awe engineer, yeye mwenyewe awe mhasibu yeye mwenyewe awe secretary yote hayo kubana pesa tu lol.

    ReplyDelete
  14. We Anon wa 4:46, kwa taarifa yako hilo jengo linafadhiliwa na wahindi!!! Mswahili gani ana interest ya kujenga in town such a big building? Wote wako baa au kwa nyumba ndogo. Waswahili (wazawa), we don't think far. Lakini, all that said, jamani hili jengo baya jamani. Hivi kweli tumeshindwa kabisa kupata a decent architect? Haya ndio mambo ya wahindi. They don't care what the building looks like, just as long as wanapata pesa. Hmmm

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...