Chama cha waTanzania waishio Washington DC na vitongoji vyake ( A.T.C Metro) kinawakaribisha nyote kwenye nyama choma itakayofanyika Jumapili hii tarehe 3 saa 10 jioni katika viwanja vya michezo na mapumziko vya Middlebrook Park, Silver Spring MD.
Mbali na nyama choma na fursa ya kukutana pamoja kama wana-familia, pia kutakuwa na mechi ya soka ya marudiano kati ya Washabiki wa Simba vs wale wa Yanga.
Ikumbukwe ktk mechi ya awali iliyofanyika Juni 15, wana-Yanga waliondoka na karamu ya magoli dhidi ya watani wao hao.
Nyote mnakaribishwa
Uongozi
A.T.C Washington DC Metro


wasiwasi wangu wataingia mitini hao Yanga si tumeona kaka zao walivyoyeya AIBU.
ReplyDeleteWatatoka nduki hao baadae waanze kuleta lawama
"Double D" unakumbuka ulivokosa goli la wazi mechi ya PCM vs PCB? Badala ya kupiga mpira kufunga goli ukaishia kubamiza ugoko kwenye chuma cha goli.. I can't forget that moment bro...
ReplyDeleteKisede.
Wachovu nyie! Changanyikeni nyote Simba na Yanga mje ATL tuwamiminie mabao! Tanzanite Fc ndio baba lao!! Kwa mawasiliano please pitia www.tanzanitefc.com
ReplyDelete