nilikutaka na tangazo hili hapa khartoum mara nilipojaribu kuingia kwenye mtandao fulani. je, wadau, mnaonaje endapo kama taasisi husika zikaiga mfano huu kuzuia mitandao inayocafua hali ya hewa katika jamii?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Si utani bro Michuzi hali ya hewa imechafuka mtandaoni. Hapa kwako angalao tunapata faraja kuingia

    ReplyDelete
  2. Hapana Michuzi me napingana hiyo kabisa maana itakuwa inaingilia uhuru wa mtu kupata habari anayoihitaji. kwa mtaji huo inamaana National Telecommunication Corporation ndiyo itakuwa unaamua wananchi wapate habari gani, this is completely not fair. Siweki shilingi hapo Mkuu wa wilaya

    ReplyDelete
  3. kuratibu shughuli za mtandao kwa namna hii ni Upanga wa ncha mbili. Kwa upenda mmoja inaweza kuzuia mambo yasiyofaa, lakini kwa upande mwingine inaweza kutumiwa vibaya na serikali na mamlaka husika katika kukandamiza uhuru wa mawazo na kujieleza. Kama ikiamuliwa njii hii itumike basi TCRA au chombo kingine kitakachopewa mamlaka hayo, kiwe na uhuru na nguvu ya kikatiba kufanya shuhuli zake bila shiniko lolote la kisiasa, kidini, n.k.

    Ila kwa kuongezea mwisho, huwezi kudhibiti yatokeayo katika mtandao kwa asilimia 100, ilihali kuna sehemu nyingine ambako mambo bado yako huria. Kwani mtu anaweza akawa ana tovuti yake imetunzwa katika tarakishi nje ya nchi, na wanaoitembelea wako nje ya nchi, lakini inaandika juu ya watu/vitu vihusishavyo Tanzania. Je tutafanyaje juu ya hili?

    ReplyDelete
  4. Sudan ni rafiki mkubwa wa China, wanaonunua mafuta yote ya Sudan kwa bei poa na mapesa yanainginia kwenya mfuko wa rais binafsi ndio wao waliolete hiyo technology ya kuzuwia mitandao kufunguka kwani hawataki watu wafunguke macho na wajuwe kinachoendelea nchini nmwao na duniani kwani wakijanjaluka wata mpa tabu rais na ulaji wake, wanataka wananci wawe mbumbumbu ili waendlea kula kuku kwa mrija, na hizo ndo za China, ukienda China hutoweza kuona mitandao mingi hasa ya nchi za Ulaya. Hiyo si demokrasi na ni ukandamizaji haifai na wala Tanzania tusilete kabisa huu ujinga.

    ReplyDelete
  5. Haipingiki kuwa kila ki2 kina ubaya na uzuri wake. Hivi ndo kusema kuacha wa2 wajiachie kuna ubaya wake na uzuri wake, na ndivyo hivyo hivyo ktk kuwabana. Chamsingi ni mamlaka husika kuangalia lipi linaleta faida zaidi kwa jamii. Nikirudi kwenye swali lako mi naona utaratibu huu unafaa sana, kwani hata hao wazungu cku hizi wanatumia sana hizi software kuchuja tovuni ambazo zinachafua hali ya hewa, hasa kwa watoto. Pia hata hapa Bongo kuna sehemu za kazi ukienda email portals zinaruhusiwa mchana tu na jioni baada ya muda wa kazi. Hivyo huo utaratibu uje na Bongo, vijana na watoto wanaharibika sana kwa kuangalia 'UBWABWA'.

    ReplyDelete
  6. ...mzee ulikuwa unataka kucheki 'ubwabwa' nini?

    ReplyDelete
  7. Swala hilo ni zuri,Bongo inaenda pabaya, moral standard zina shuka, vijana wengi hawajui mila zao za kiutmaduni. Mambo mengi yakijinga yasiofaa yanapatikana kirahisi mtandoini na pia control kwenye media inahitajika hasa magazeti ya tabloid.

    ReplyDelete
  8. He!
    Kwani "UBWABWA" ndo nini wenzetu?

    Sie wengine wenzenu tumetoka Liloya leo.

    Khaa!

    ReplyDelete
  9. Michuzi unataka kuturudisha enzi za TVZ nini? Nakumbuka enzi hizo kama ulikuwa huna antena ya mwiba wa samaki wewe ni sinema za kihindi tuuu. Hii kitu imekaa kushoto sana. Kutokana na kwamba hizi serikali zetu finyu zitaweza kubania hata websaiti nyingine ambazo zinahatarisha kuwepo kwao madarakani kwa kisingizio kuwa zinachafua hali ya hewa. Katika zama hizi sitaki serikali iwe inanichagulia ni website gani ninaweza kuangalia, redio gani nisikilize au TV prog. gani niangalie. Mwishowe watasema watu wasiendeshe magari yao.

    ReplyDelete
  10. Huo ni kuwaondolea watu uhuru wa habari. Unajua ni vitu vingapi vinablokiwa kwenye hizo nchi? Kuna vitu vingine vya muhimu lakini kwa ajili Govt inaamua kublock kila kitu kutoka sehemu fulani basi ndio hivyo.

    Aheri ya hii mtu unajichagulia nini cha kusoma na nini hutaki unapitupia pembeni.

    ReplyDelete
  11. ulikuwa umeingia site gani kaka Michuzi hadi ukawa blocked??? Uliingia site chafu nini???

    ReplyDelete
  12. 'UBWABWA' ni Picha chafu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...