Mh Balozi na mkuu wa wilaya ya nanhii.......

Mzee katika soma soma yangu ya huku ughaibuni, nimekutana na hii taarifa ya maswala ya Ushindani Duniani katika sekta ya utalii.

Report ya World Economic Forum 2008 inaonesha Tanzania ni nchi ya 88 katika ushindani wa kuvutia watalii duniani, watani wa jadi Kenya na Uganda ni wa 101 na 110 kwa mfuatano(table 1).


Hii inaonesha tumewafunika watani vibaya. Na zaidi ya yote katika kijisekta kidogo cha mvuto wa maliasili kiutalii Kaka tumefunika Dunia nzima sisi ni wa kwanza (table 4).

Nilihudhuria presentation ya Dr Diana ambaye ni Mchumi Mwanandamizi wa UNCTAD aliyoitoa wiki mbili zilizopita hapa chuoni, ameisifia na kuifagilia sana Tanzania na anasema kutokana na mwelekeo unavyoendelea Bongo siku za usoni itatisha katika nyanda za kiuchumi Africa na Duniani kwa ujumla.

Wadau waweza pata habari zaidi katika mtandao huu http://www.weforum.org/pdf/CGR08/Rankings.pdf .
Warushie wadau wa Blog ya jamii wajivunie!!!!.
Ila ufisadi ipo issue!!! hahaaahhaaaaa....
Bongo oyeeeee!
Mdauzzz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. kungekuwa hamna rushwa za vijisenti ingetisha siku za usoni

    ReplyDelete
  2. Ni kweli kama anon hapo juu..hali ya uchumi ingeinuka sana kama tungeanza hapo mapema hata kabla ya mambo ya ugaidi kuchafua hali ya hewa..asilimia kubwa ya watalii na hata wawekezaji kwasasa huwa wanajiuliza mara mbili..anyway ni step nzuri tuzidi kujitangaza..

    ReplyDelete
  3. Tudo Jones(Grumeti Tented)hawa ni watu wenye hela nyingi sana U.S.A hapo Connecticut(CT)Sorry speling if any,wana mpango wa kununua Serengeti so far wameshanunua ardhi kubwa sana Northern Serengeti inaitwa Serengeti Reserve mimi nimefanya kazi huko kwa kweli tunakoelekea wataidevelop sana hiyo serengeti mpaka itapoteza authenticity as Serengeti itakua zoo as a lot of tourist complains about parks like Krouger N. Park in South Africa which is over developed.
    Kuhusu park zetu kuwa overdeveloped in a near future naomba michuzi uweke hewani tujadili na wadau wenye data watueleze,mimi niko tayari kuleta data zangu.

    ReplyDelete
  4. sio mbaya imekuwa nchi ya 88 kama ufisadi"ufisimaji" hauto endelea itakuwa nafasi nzuri lakini inaweza kurudi nyuma

    ReplyDelete
  5. anony wa 1:06 kanena. Utalii, Tanzanite, Dhahabu, Gesi, n.k tele. Tatizo ufisadi mwanangu, ufisadi unatuua!!
    Hadi ukokotoaji wa GDP ya Tanzania nashauri urekebishwe kuruhusu nafasi ya ufisadi kupunguza % kadhaa za ukuaji uchumi!!

    ReplyDelete
  6. Tumewekwa mbele ni kama nchi ya kwenda na kujichotea bila shida. Watani wa jadi wanajikomboa kiuchumi na hawataki kutawaliwa ndio maana mabepari wa nchi za nje wanakuja tanzania. Tatizo sio mafisadi, ufisadi ndio matokeo ya mfumo wa kisiasa ya kibepari tunaofata hivi sasa. Wachahe watanufaika na wengi wao ndio watakuwa masikini. Bila shaka nchi hii inaenda pabaya itafika muda watu watahamka hapo ndipo zitakapo pigwa wenyewe kwa wenyewe kati ya mabepari (mafisadi) na walala hoi (wananchi wengi na wanao watetea)

    ReplyDelete
  7. Nakubaliana na October 02, 2008 12:32 PM.Kenya ndio inayosifika dunia nzima kwa utalii hata Mlima kilimanjaro unajulikana upo Kenya.

    Pamoja na machafuko ya hivi karibuni wakenya bado wamfunika mashimo.Sisi tupo wapi?

    Ripoti ya Benki ya dunia iliyotoka hivi karibuni inasema kuwa Tanzania ni sehemu ngumu kuanzisha biashara.

    ReplyDelete
  8. Amin amin naapia, ufisadi hautaisha na kasi ya maendeleo itaendelea kudoda if and only if we young people are not MEANINGFULLY involved to take control of our resources.

    Ole wenu mlio madarakani kwa kunyonya jasho la mzee Hamza, bibi Tina, na wengineo walio masikini kama mimi na mnakimbizia vijisenti nje. Vijana tuamke, na wazee walio mlio madarakani badilikeni kwa kutubu na kuungama.

    Ubarikiwe ulieleta habari hii na sote tulio na uchungu wa nchi hii ya Tanzania. Amen

    ReplyDelete
  9. Amin amin naapia, ufisadi hautaisha na kasi ya maendeleo itaendelea kudoda if and only if we young people are not MEANINGFULLY involved to take control of our resources.

    Ole wenu mlio madarakani kwa kunyonya jasho la mzee Hamza, bibi Tina, na wengineo walio masikini kama mimi na mnakimbizia vijisenti nje. Vijana tuamke, na wazee walio mlio madarakani badilikeni kwa kutubu na kuungama.

    Ubarikiwe ulieleta habari hii na sote tulio na uchungu wa nchi hii ya Tanzania. Amen

    ReplyDelete
  10. Nimefurahi kusikia hili, ila naomba kama utatupa data zaidi kuwa kwa UFISADI sijui bongo tupo namba ngapi.


    Q

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...