JK akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Kamopuni ya simu ya Vodacom, Dielf Mare wakati wa hafla ya miaka mitatu ya kituo cha vipaji nchini (THT) jijini Dar usiku kuamkia leo viwanja vya ukumbi wa karimjee hall. Hafla hiyo ya kuadhimisha miaka mitatu ya THT ilidhaminiwa na Vodacom.

JK akiangalia shoo ya akiwa beneti na mkurugenzi mwanzilishi wa THT ruge mutahaba usiku kuamkia leo
Mwimbaji wa nyimbo za kizazi kipya ambaye ameanzia kazi katika kituo cha vipaji (THT) akitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miak mitatu ya kituo hicho juzi
Wasanii wa kundi la burudani la THT wakitoa burudani wakati wa hafla ya miaka mitatu tangu kuanzishwa kwa kituo hicho Dar es Salaam juzi
Wasanii wa THT wakitoa burudani ya 'thriller' ya maiko jeskson wakati wa hafla ya miaka mitatu tangu kuanzishwa kwa kituo hicho Dar
-------------------------------------------------------
Wadau wa muziki wa bongo flava wamepumua kwa shukrani baada ya JK kuahidi kuwatengezea studio kubwa na ya kimataifa ya muziki ili kuwasaidia kujikwamua kiuchumi na kisanii.
JK ametoa ahadi hiyo kwenye hafla ya kutimiza miaka 3 kwa THT ambapo alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo iliyoandaliwa na vodacom.
Habari kwa urefu baadaye






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Picha ya mwanzo kabisa nilidhani kwamba huyu jamaa ni Bush na JK...........

    ReplyDelete
  2. Ni kifo cha wanamuziki kama hiyo Studio itamilikiwa na huyo Ruge. haita saidia walio wengi ita saidia hao wachache atakao kubali kunyonya na huyo Ruge.ichuzi bana hiyo isitoke man anajua utalinda.

    ReplyDelete
  3. Jamaniii! Kila kitu na nafasi yake! Si kazi ya rais kuanzisha studio ya mziki! Weka taratibu za kueleweka za sanaa, especially kuwe na sheria ya hati miliki, watu wengine watafanya hayo mambo ya studio etc.

    Mbona hiyo sherehe hawakuofanya kwenye kituo cha THT, waone hali halisi.

    Tumpongeze Ruge lakini tena kuwe na utaratibu wa kudhibiti watu wanaopata fedha za wadhamini ili zitumike ilivyokusudiwa!

    ReplyDelete
  4. Jamani huyo mwimbaji wa kizazi kipya(picha ya tatu) anaonekana kama ni albino vile, ajihadhari na maharamia walio na imani potofu dhidi ya wanadamu wenzao wasije wakagawana viungo vyake.
    Eee Mola wetu waangamize wanaowaua albino - amen

    ReplyDelete
  5. Hivi huyo Ruge huwaga ni kijana au mzee? Maana siwezi kabisa kum-tathmini!

    ReplyDelete
  6. sasa mh Kikwete badilisha ilo koti baba nimekuona nalo kwenye vijisherehe kibao sasa sijui kwa nini,sasa ona mwenzio Michuzi tunamtaniaga na kijishati chake,naomba ndio uwe mwisho leo kukivaa hiko kikoti chako,nunua suti raisi,
    au nunua koti jeusi la kiana uwe unazukia hatutashitukia sasa ilo la rangi ndio maana tunashitukia kichizi raisi wangu,
    sawa natumai ujumbe umekufikia maana hii blog ya michu ni tisha mbali hata wewe Raisi wetu tunaamia kuwa unaicheki kiaina ukiwa unarelax,

    ReplyDelete
  7. JMK in the occasion that you attended navy or charcoal gray suit would have been appropriate. Dress the occasion, sport coat aren't appropriate to dress in the evening (color) a blazer would have been much better than what you have.
    Thanks

    ReplyDelete
  8. annon 7.41 Pm December 10 tafadhali tushikie shule kuhusu suti. nahisi unazijua sana. Maana wengine huwa tunazitundikaga tu kwenye mwili. Ombi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...