HABARI ZIMEINGIA SASA HIVI ZINASEMA KWAMBA MZEE GEORGE KRITSOS, YULE MWENYEKITI MSTAAFU WA KLABU YA GYMKHANA NA MMILIKI WA SHELI YA GAPCO ILIYOVAMIWA NA MAJAMBAZI LEO ASUBUHI PALE MAGOMENI MAPIPA HAJAMBO NA AMERUHUSIWA KWENDA NYUMBANI BAADA YA MADAKTARI KUMHUDUMIA MAJERAHA YA RISASI.
INASADIKIWA MZEE GEORGE ALIPIGWA JUMLA YA RISASI MBILI, MOJA ILIINGIA BEGANI NA KUTOKA UPANDE WA PILI, NA MOJA BADO IMEBAKI NDANI. INASEMEKANA WALILENGA USONI, AKANUSURIKA KIFO KWA KUDRA YA MWENYEZI MUNGU...
NIMEONGEA NA MTU ALIYE NAYE KARIBU MUDA HUU NA KANIHAKIKISHIA KWAMBA HAJAMBO NA ANAENDELEA VIZURI, ILA MOYO UNAMUUMA SANA KWA KIFO CHA MHASIBU WAKE AMBAYE ALIPIGWA RISASI NAYE WAKATI WA HUO UPORAJI.
MZEE GEORGE KRITSOS PIA AMETOA SALAMU ZA SHUKRANI KWA WADAU TOKA SEHEMU MBALIMBALI DUNIANI AMBAO WAMEKUWA WAKIMPIGIA SIMU KUMJUA HALI TOKA GLOBU YA JAMII ILIPOTOA BREKING NYUZZZ YA KUVAMIWA KWAKE.
ANASEMA INAGAWA ANAOMBOLEZA KIFO CHA MHASIBU WAKE, LAKINI ANAFARIJIKA KWA MOYO WA UPENDO AMBAO WADAU MMEMUONESHA KWAKE, NA ANAWAOMBEA AFYA NJEMA.
GLOBU HII YA JAMII INAMTAKIA MZEE GEORGE KRITSOS UNAFUU WA HARAKA NA KUMWIMBA MOLA AIWEKE PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU MHASIBU WAKE ALIYETANGULIA MBELE YA HAKI - AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Kaka mpe Pole mzee George,mwambie nampa pole kwa Kigiriki,PERASTIKA..
    Mdau Ugiriki

    ReplyDelete
  2. KAKA MICHUZI USIOGOPE KUAMBIWA NA WEWE MICHUZI NI MBEYA HIYO LISASI YA BEGANI KUTOKEA UPANDE WA PILI UMEIONA? KAMA KUNA RISASI IMEBAKI NDANI KWA NINI KARUHUSIWA KWENDA NYUMBANI? HUYO MTU KWELI AMEJERUHIWA AMA NI UMBEYA WAKO TU? JUNOLISTI MZIMA UNATAKIWA KUTUPA VITU VYA UKWELI SIYO LONGOLONGO. HALAFU UTAIBANIA HII COMENTI ETI NIMEKUTUKANA? LA ASHA NIMEKUPA VIDONGE VYAKE!

    ReplyDelete
  3. Poleni sana. Je tunaweza kupata jina la huyu mhasibu wake? maana ukisema mhasibu pake yake haitoshi kufahamu. Labda naye tunamfahamu au anatuhusu.

    Tunashukuru kwa updates za nyumbani.

    Mdau
    Mashariki ya mbali.

    ReplyDelete
  4. Pole sana
    mzee kristos,jamani ninaswali hivi huyo kristos
    ndo baba yake na Evelyn kristos

    ReplyDelete
  5. kaka Michu tunaomba jina la Marehemu, mzee Kristos tunashukuru kapona lakini haitakuwa haki kama hatutamtaja marahemu kwa jina na kuishia kumuita tu mhasibu wake nadhani kama ambavyo tunalitaja jina la mwajiri wake na la marehemu ni rahisi kulipata pia. Asante mdau ughaibuni.

    ReplyDelete
  6. Huyo mzee yeye ni robot nini anaeweza kutembea na risasi ikiwa bado ipo mwilini mwake?acheni mzaha mie nahisi hata kuibiwa basi atakuwa labda hajaibiwa pia kwa style hii

    ReplyDelete
  7. Ndugu Balozi Michuzi,
    Nakushukuru kwa kutupa habari za ndugu Kristos na tunampa pole sana.

    Nasikitika kusema kuwa baadhi yetu bado hatuwezi kuandika maoni bila ya kutoa mtusi ya nguo na naomba urudie tena kubana maoni ya wadau kama hao.

    Mimi nilikuwa mmoja wa wadau hapa waliokupinga ulipokuwa unabana maoni lakini sasa nitakuunga mkono kama ukibana maoni hasa yanayokukutukama wewe binafsi kama ya 4:02 hapo juu. Usilazimike kuchapisha maoni yanayokuita mmbeya. Tunakuunga mkono kama utawabana wadau kama hao wasiokuwa na shukurani na kazi unayoifanya hapa.

    Aluta Kuntinua.

    ReplyDelete
  8. Hi Michuzi,
    Pole kwa kazi.
    Mimi napenda tu kukusahihisha. Nafikiri watu wengi sana hapa kwetu hawajui maana ya "shell" na badala yake wamekuwa wakilitumia hili neno (ikiwa ni pamoja na wewe) kumaanisha "kituo cha mafuta". Ninavyojua mimi vyote vinaitwa "vituo vya mafuta" lakini makampuni ni tofauti. Kwa mfano: Kituo cha mafuta cha Total, Kituo cha mafuta cha Oryx, Kituo cha mafuta cha BP nk. Hii kituo cha mafuta cha shell kilikuwepo zamani huku kwetu lakini kwa sasa hakuna tena, ila nchi nyingine kama vile Kenya na Uganda ambapo mimi niliwahi kuzitembelea bado zipo.
    Ni hayo tu mzee.

    Ila hakuna kitu kama "Shell ya Gapco".. Ahahahahhaa...

    Kazi njema mzee na pole kwa wahanga wa tukio la jana la ujambazi.

    ReplyDelete
  9. wewe kabwe unadhani kila ukiongea utapata umaarufu? hii inaonesha hata huko bungeni hauko serious mimi nilikuwa nakuamini sana lakini hii coment uliyo weka inaniogopesha kabisa. sasa matusi ya nini humu unakuwa sawa na masha sasa. mimi nilikuona mwelevu lakini haya matusi nakuogopa sasa

    ReplyDelete
  10. watu kama KABWE ndiyo wale walio na roho za "KWA NINI!"
    tutafika kweli tukiwa na watu kama hawa?

    ReplyDelete
  11. He tayari mmeshajua ni Kabwe wa Bungeni? mmm...mapema mno jamani, embu muwe mnajaribu kuuliza basi ni kabwe gani sio tu kuponda, ooo kama masha, sijui nini huko. Mnaudhi kweli sometimes wadau wenzangu

    ReplyDelete
  12. Hawa wezi yawezekana kuna mkono wa askari dezaini ya zombe .Sadi kazi kwako. Wameshajua hata zombe yawezekana akatoka, hivyo kuna uwezekano mkubwa akawa ni askari tu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...