hawa ni wapiganaji waliotunukiwa nishani kwa kushiriki katika vita ya kuung'oa utawala haramu wa visiwa vya comoros. toka shoto ni mroky mroky wa habari leo na daily news, mwintanga wa zanzibar leo na khalfan saidi wa the guardian na nipashe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Jamani hiyo Vita ilipiganwa lini? mbona tunaona Nishani tu? Tunaomba tuwekane sawa....

    ReplyDelete
  2. CHRISTMAS EVE AT PILIPILI
    KWA WAKAZI WOTE WA BEIJING-CHINA NA MIJI YA JIRANI
    AFRICA NIGHT X-MAS EVE BASH @ PILIPILI. DEC 24. 10:30 TILL LATE.
    INFO LINE 13717640747. pls FORWARD MESSAGE.
    MERRY CHRISTMAS~~~~~

    ReplyDelete
  3. HEBU ACHENI SIASA NA PROPAGANDA...KAMA KWELI TANZANIA INGEKUWA NA NIA YA KUSAFISHA UOZO AFRICA, KWANINI ISINGEANZA NA CONGO? NAONA YALIYOJILI KOMORO YAMEKUWA SEWE! (I KNOW YOU WONT POST IT, THANKS)
    MTANZANIA MKWELI

    ReplyDelete
  4. DA MWANANTANGA PITIA CCM JIONI NTAKUACHIA BIA 5 CAUNTA....teheheee

    ReplyDelete
  5. jamani kuuliza sio ujinga, hili neno "wapiganaji" lina maana ngapi? kwa ninavyokumbuka mimi ni mtu anaepigana kama ni masumbwi au hata katika vita, lakini nimekuwa naona hapa hata waandishi wa habari na wapiga picha huitwa wapiganaji, na leo hii naona taarifa hii ambayo imenisumbua, jee hawa ni wanajeshi walioshiriki hivyo vita au ni waandishi wa habari? kama ni wanajeshi wako wapi wenziwao? bila shaka hawakwenda peke yao. Naomba kuelimishwa. shukrani.

    ReplyDelete
  6. Asante Kaka Michuzi kwa kutuhabarisha hilo ila naomba utupe angalau habari kidogo kuhusu hilo suala la uongozi mbaya wa Huko Comoro na hawa watu walifanya nini hasa katika kushiriki kwao
    Asante,
    Mdau

    ReplyDelete
  7. HUYO MROKY NI MPIGA PICHA WA DAILY NEWS SASA HAPO SELEWI

    ReplyDelete
  8. naunga mkono ndugu aliegusa issue ya waandishi wa habari kuitwa wapiganaji. sijui ni kwa nini, lakini kwa upande mmoja inatatanisha na kuleta taarifa isiyo sahihi, tuchukulie mfano huo wa kuikomboa commoro (kama tuambiavyo) bila shaka walioikomboa ni wanajeshi ambao ndio waliopigana hiyo vita hata kama ilikuwa ndogo na ni ya upande mmoja. sasa kumwita muandishi alie cover story ya vita hivyo kwa jina la mpiganaji unamfanaya anaesoma maelezo yako aamini kuwa hao ni majeshi waliokwenda kupigana huko commoro. Naomba kutowa hoja.

    ReplyDelete
  9. Haya mambo ni tata kiasi. Hawa walienda kama waandishi, lakini kumbukeni walienda na jeshi letu (ambalo lilikuwa linaongoza wanajeshi wengine wa Afrika). Ni sawa na kusema walikuwa sehemu ya jeshi letu.

    Wanastahili pongezi kwa hilo. Mambo ya vita yana mitaala yake, na mwisho wa mpambano SOTE TULISHINDA. Nami naungana na taifa kuwapongeza wapiganaji hawa. Neno 'wapiganaji' halijatumika kupotosha, na sio wale waliokuwa wakimimina "mioto" tu, bali hata wale waliokaa mezani kupanga vita iende vipi.

    Dr. J. K. sijui ni kwa nini unapata kwikwi kumng'a Mugabe. Ina maana Mugabe ni bora kuliko yule mkomoro aliyekimbia na baibui la shemejiye? Au unataka kusema yule mkomoro alikuwa mbaya kuliko Mugabe? AU inahitaji meno, na kwa hili la Zimbabwe unapaswa kuwajibika i.e play ur role.

    Nonviolence strategies have failed, and no longer useful. Wanaoumia ni wananchi, kwa sababu ya mtu mmoja tu, MUGABE. Why? Ruhusu ANG'OLEWE.

    Sevedo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...