JK alikuwepo kuangalia mtanange huu wa kirafiki kati ya taifa stars na zimbabwe uwanja wa neshno wa kale. matokeo ni 0-0 na imeonesh dhahiri kwamba ili tufanye vyema huko ivory coast baadaye mwezi huu safu ya ushambuliaji inahitaji lekcha ya ziada ili kuweza kufunga
mshambuliaji machachari wa taifa stars mrisho ngasa aliwekewa ulinzi wa sungusungu dakika 90 kiasi hakuweza kufurukuta kama ilivyotarajiwa
taifa stars
kikosi cha timu ya taifa cha zimbabwe






























Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. ivi stars wanaweza ku perform huko Ivory Coast from today's game???
    Mdau Japan

    ReplyDelete
  2. Hahaha mie hapa ndio napofurahia game ikiisha 0-0 Safu ya ushambuliaji wajifue Ikifungwa Kipa mbovu ambayo Kipa kweli mapunda alikuwa mbovu, mie naona Timu ya Taifa ina washambuliaji wazuri ila ma winger hawana kabisa. Pzi

    ReplyDelete
  3. Tusijidanganye, Stars haiwezi kufua dafu Ivory Coast, tusimsikilize Maximo, hatuna timu nzuri kiasi hicho, kwanza hata kipa hatuna na sasa naona tatizo la ufungaji limerudi tena. Wachezaji wazuri ni wale wa Simba walioko nje, Kuwait na huyu aliyekwenda Norway, tuwe wakweli tu.

    Ila jamani huyu Makamu wa TFF hana haiba, kakaa kama mtu wa mitaani, hivi haiba si kigezo cha uongozi Tanzania?

    ReplyDelete
  4. starz wamejitahi hii zimbabwe timu inzuri sana iliipiga bao sauz nyumbani na ugenini na kufanikiwa kuingia ktk mashindano ya chan

    ReplyDelete
  5. Zimbabwe wamelisakata kabumbu ipasawoo ila umaliziaji.

    ReplyDelete
  6. Hatujasahau ya EPA, KIWIRA, madini, nk ndugu mheshimiwa

    ReplyDelete
  7. Wee mdau wa Japani, ujue ya kwamba
    (it is 11 against 11. Anything can happen). Usema kweli mimi nadhani wamejitahidi sana ukiangalia kandanda ya zimbabwe ni nzuri ndo maana huwa wanatoa wachezaji wakimataifa kama Benjani Mwaruwari.

    P.E.D

    ReplyDelete
  8. DAKIKA 90 ZA KUKAA NEXT TO PREZIDAA HUYO VAIS PREZIDAA WA SOKA INAWEZEKANA ALIONA KAMA MASAA 9 VILE.

    ....HABARI NDIYO.....

    ReplyDelete
  9. kweli nimeamini bongo tambarare hata vip lounge hamna yani hiyo ndio sehemu ya kumuweka rais.

    ReplyDelete
  10. Michuzi naomba unijulishe jinsi nitakavyoweza kupata taarifa kamili za wachezaji wetu wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu, hapa nina maana ya majina yao kamili, sura zao wakiwa na jezi za timu ya taifa, maelezo yao au wasifu wa maisha yao ya soka.

    Hii itasaidia sana kuwafanya watanzania wapenda soka kufuatilia na hatimaye kuwafahamu wachezaji wetu kwa kina japo wengi wetu tuko nje ya nyumbani.

    Kimsingi hili ni suala la TFF, au kama unafahamu anuani ya tovuti yao, basi tupe link.

    ReplyDelete
  11. MDAU UMENIACHA HOI KWELI LEO DAH!!!ETI HAIBA SIO KIGEZO CHA UONGOZI BONGO??JAMAA KWELI PERSONALITY MBOVU SANA HUYO ANAONEKANA KAMA MTU WA KIJIWENI TU MTIZAME MIDOMO ILIVYOUNGUA KWA MAMBO YA UVUTAJI SASA SIJUI ANAVUTA NINI?TUOMBE IWE SIGARA YA KAWAIDA TU VINGINEVYO JK ALIPATA KAJISALAMU KAHARUFU KA ILE FEGI KUBWA

    ReplyDelete
  12. yan annon apo nilitaka kuuliza the same,,,
    jamani UYO NANI ALOKAA NA JK?????KITUKO GANI ICHO???dah jamaa smiling face ya camera imegoma kabisaaaaaaaaaaaaa
    hahahahaaaaaa u made my day

    ReplyDelete
  13. Nyinyi watu mna matatizo ya Problem!!! Huyo jamaa mnayesema hana haiba ya uongozi, amekwenda hapo KUONGOZA soka sio kushiriki u-MR TAnazania!!Tuonyesheni nyinyi sura zenu tuzione kama hatujakimbia hapa!! Kuhusu gemu, Vijana wamecheza vizuri tu. Tukumbuke kwamba kila mchezaji sasa hivi akili yake iko kwenye CHAN kwa hiyo kila mtu alikuwa anacheza kwa tahadhari asije akaumia dakika hizi za majeruhi akakosa kwenda kuonekana na Scouts wa matimu makubwa. Habari ndio hiyo.

    ReplyDelete
  14. Mdau PED...
    unajua...people talk from evidence....ssa this nil nil draw with zimbabwe is one of the many evidences that bring about doubts if stars are going to perform in ivory coast...i m not criticizing but im jus stating facts here
    Mdau Japan

    ReplyDelete
  15. Uzoefu umeonyesha kwamba kwenye mechi za kirafiki Stars huwa wanawakatisha watu tamaa ila wakiingia kwenye mechi wanabadilika. Ni mapema mno kukatishwa tamaa. Ila tatizo la kukosa mtu wa kucheka na nyavu bila aibu tunalo na limekuwa sugu kwa muda mrefu. Hatuna mtu kama marehemu Edo, kepteni morgan au mzee wa kiminyio mbaye akiweka mguu uwanjani unategemea goli.

    ReplyDelete
  16. Hivi ni nani anadesign jezi za Taifa Stars?????Mbona jezi hovyooo kabisa mirangi rangi tuu.Ni vizuri kutumia rangi moja au mbili sio kuchanganyachanganya its shame.Kama ni blue na nyeusi or kijani na njano,au blue na njano or njano na nyeusi sio.Atafutwe designer mwingine jezi zetu sijazipenda kihivyo.
    Cha Chandu UK.

    ReplyDelete
  17. Kila siku tunajitahidi??? we need to perform..i think maximo hajielewi kabisa...Manake sioni kwenye list mtu kama haruna moshi au Mgosi...tanzania hamna forward kwa sasa zaidi yao...Sasa mtu kama tegete kilo 55 zake anaweza kumlalia njemba ya beki ya zimbabwe na kufunga??? tunatania soccer bado halipo bongo...Kocha wa Beach soccer huyu...Huko Scotland alipokuwa anafundisha maximo walimtimua na ilikuwa timu ya 2nd division sisi tumempa National team....Kwa mwendo huu Tutajitahidi Sana then word KUJITAHIDI ndio litakuwa lipo always hatutokuwa na TUME PERFORM...!!!

    ReplyDelete
  18. wadau
    we need to understand and be able to scrutinize things here...it is evident that maximo has performed wonders on out national team...but we need to understand that to get to a certain level...the players themselves need to be enthusiastic as possible in order to be on the same level with other players...asa unakuta mchezaji wa timu ya taifa wewe mwenyewe hana balanced diet...does not visit the gym one regular basis...asa vitu kama hivi sio maximo....ni kujituma kwa wachezaji wenyewe...shabani nonda alikua anajituma to his maximum level...sasa yupo wapi??!!!if we have committed and "thirst for excellence" players like him...i m 100% sure that in the next 2 to 3 years we are going to be in a good position in the FIFA rankings...
    Mdau Japan

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...