kocha wa timu ya taifa ya vijana kutoka brazil marcus tinocco (pichani akikagua timu ya vijana akati wa copa coca cola mwaka jana, dar) ameliandikia shirikisho la soka nchini (TFF) barua ya kujiuzuru nafasi hiyo kwani amepata kibarua kipya huko trinidad and tobago kufundisha timu ya daraja la pili ya huko.
globu ya jamii imethibitisha kwamba tinocco aliitoa barua hiyo hata kabla ya taifa stars kwenda ivory coast kwenye michuano ya CHAN, ambapo ndiyo kusema hatuna tena kocha mtaalamu wa timu ya taifa ya vijana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Kulipa hamuwezi manajidai makocha hawajui kazi mnataka wazalendo
    mwaya maximo usisaini mkataba rudi kwenu. achana na wbabaishaji. wanajadili kitu wasichoweza kufanya.

    ReplyDelete
  2. Usilalamike sana mdau kuhusu kuwalipa makocha wa kigeni, Kiukweli bado WaTZ hatujafikia hatua ya kuappreciate Proffesional za Wengine KIVITENDO. Tukifika hapo utaona japo safari ni ndefu sana mdau.
    Wakatabahu,Tabata

    ReplyDelete
  3. Ni masikitiko makubwa kwetu wana michezo, lakini namuomba rais wa tff kufanya juu chini ili tuweza kupata kocha mwingine atakaye wafundisha vijana wetu, maana uko ndiko kwenye vipaji.lakini lazima awe kocha kutoka nje ya nchi, maana hapa kwetu wapo, lakini longolongo nyingi na ubabaishaji.

    ReplyDelete
  4. Du nilifikiri hilo ni tatizo la simba na yanga tu kukimbiwa na makocha, kumbe ni tatizo la taifa.

    Haya bwana.
    Mwakalebela

    ReplyDelete
  5. Huyu hajaondoka, yuko likizo ya mwaka mmoja bila malipo.

    ReplyDelete
  6. Tinoco alikuja kufundisha soka. Matazamio yake yalikuwa kuandaa timu ishindane mashindano mbalimbali ili aonyeshe uhodari wake. TFF walipoitoa timu walimtafuta ubaya tu.
    Tushazoea makocha kukimbia...Micho, Bezinski, Stanslescu.....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...