Tuncay Sanli blasted a huge hole in Liverpool's Barclays Premier League title challenge as Middlesbrough gave their survival hopes a massive boost.
RAFA BENITEZ admitted the title was out of Liverpool's hands after Middlesbrough ended their 14-game winless run.

Hivi kwa nini hawa bwawa hawawezi kushind mechi baada ya high profile game? mnakumbuka na stoke? inabidi tuwaite nyuki dume. ambao kwa kawaida hufa baada ya kumwona malkia.
GLORY GLORY.....
Mdau UK
----------------------------

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Inasemekana mkuu wa wilaya ya nanihii kakimbizwa hospitali ya Aghakhan baada ya matokeo hayo.
    mzee u will never walk alone,hahahaaaaaaaaaa

    ReplyDelete
  2. Inakuwaje maiti inapong'ang'ania mwoshaji?

    Pole sana Mh Balozi

    ReplyDelete
  3. Mtoto yake nepi.....mkubwa mkubwa tu. Benitez kwenye mechi muhimu anapanga kikosi cha ajabu. Pale juu kukaa simchezo. Rock on ManUTD.

    ReplyDelete
  4. Mtoto yake nepi.....mkubwa mkubwa tu. Benitez kwenye mechi muhimu anapanga kikosi cha ajabu. Pale juu kukaa simchezo. Rock on ManUTD.

    ReplyDelete
  5. Michuzi tuwekee kabisa na msimamo wa ligi ili tuone hali ikoje. Wenzenu Chelsea wanasema hawajakata tamaa na wana matumaini makubwa bado chini ya Mdachi wao aliyechukua kwa muda nafasi ya Scolari.

    Lakini tuweke unazi pembeni jana Liverpool ilikuwa nyanya masalo. Kuna magoli mengine 2 ya wazi yalikuwa yanawanyemelea lakini jamaa zao wakapata kitete vinginevyo ingekuwa aibu ya mwaka. Niliwahi kusema kwamba Torres asipocheza jamaa inakuwa ngumu sana kufunga magoli, kuna nafasi kama 3 hivi zilipatikana kipindi cha kwanza, angekuwa ni Torres wala asingefanya makosa ingekuwa ni habari tofauti kabisa, Rafa bado angekuwa na matumaini makubwa sana kwamba bado ni contender wa Kombe la Ligi Kuu.

    Kucheza na timu zinazochungulia shimo refu la kushushwa daraja ni balaa kubwa. Ni sawa na mtu ambaye ni mtaalam wa kuogelea na bahati mbaya ikatokea dhoruba, kama kuna mtu hajui kuogelea lazima ahakikishe anakushika shati ili umwokoe ama mzame nae na kibaya zaidi huwa hawajui namna ya kushika na hivyo anaweza kukushika vibaya kiasi kwamba ukashindwa hata kupiga mbizi na hivyo mkajikuta wote mnazama. Hayo ndiyo yaliyowatokea vijana wa Bwawa na Mapavu, maana jana wali-walk na vijana wa Middlesbrough. Vijana wa Middlesbrough wamejikuta wanakatisha mstari mwekundu wa kule chini, japo haijulikani kama wataendelea kuwa hapo above the line ama watashuka tena chini ya huo mstari.

    Poleni sana mashabiki wa Liver, lakini huo ndo mpira. Mwambieni Rafa aongeze juhudi kwenye makombe mengine ambako bado ana matumaini.

    ReplyDelete
  6. Tatizo kuchukua ligi ya UK lazima upambane na vikwazo vingi
    Cha kwanza ni waamuzi wabovu wanaochezesha ligi ile. Kama utakumbuka mechi ya Man na Blackburn wageni walistahili kabisa penalt lakini refa alikosea maamuzi na hivyo kuipa faida United. Mechi ya Liverpool na Man city Dunn alinawa mpira waziwazi refa kama kawa akakosea kitu kilichowapa Man U 2pts advantage.Achilia malalamiko ya Scolari kuhusu timu yake kuhujumiwa kwa kunyimwa penalt za dhahiri n kufungwa magoli ya offside(kama ingekua si kweli basi angeadhibiwa lakini FA hawakumwadhibu sababu aliyosema yalikua ni kweli )
    KItu kingine ni ratiba za upendeleo kwa kisingizio cha Televisheni. Liverpool walicheza Champions league jumatano tena ugenini Hispania,wakarudi Alhamisi na kupumzika ijumaa mazoezi mepesi(champions league ni mechi ngumu sana) jumamosi wanacheza tena away katika hali ile ni lazima kutakua na tatizo la match fitness tu hilo ni wazi(lakini kwa Man U kapewa 2 day off+ League cup final. Nakumbuka Mourinho alishawahi kulalamikia sana suala la ratiba hasa msimu ule wa 2006/07 baada ya FA bila sababu za msingi walisogeza mbele mechi ya Chelsea vs Man U ikachezwa zikiwa zimesalia mechi 3 tu ligi imalizike yote ni kuiokoa Man u isipanic endapo ingepoteza ile mechi ya ugenini na Chelsea.
    Kwa hiyo sishangai Manchester kusaidiwa kiaina flani na FA ili itwae ubingwa. Japo wadau wengine watalipinga hili lakini ukweli unabaki pale pale timu iliyocheza mechi ya Champions League jumatano (ugenini)kisha ikachezajumamosi mechi ya ligi ugenini mara nyingi sana huishia kupata matokeo mabaya tu.
    Maamini kungekua na usawa katika ligi ya UK Man isingekua pale ilipo kadhalika Chelsea na Liverpool zisingekua chini ya Man U.

    ReplyDelete
  7. pumba na mchele unaanza kujitenga taratiiibuuu,wenye nafasi zao washajipanga hiyo ndio mpaka mwisho.poleni sana bwawa la maini. kocha kashaishiwa ujuzi, kafika mwisho.timuen tu sasa.

    ReplyDelete
  8. Bwawa nguvu ya soda

    ReplyDelete
  9. Mishuzi matokeo ya chelsea mbona huyatoi?, au unaona njindi?

    ReplyDelete
  10. Bro Michuzi habari za kwenye mnuso. Kuna kitu kimoja nimegundua, naomba nisaidie. Mimi sio mshabiki wa boli la UK ingawa kwa sasa niko huku. Ila tangu nianze kupitapita kwenye hili jamvi la jamii, yapata miaka miwili sasa,nimegundua kuwa mara nyingi bwawa la maini likikauka maji au kujaa matope, habari huwa zinachelewa sana kuwa posted kwenye hili jamvi. sasa sijui kabla ya habari kufika kwenye hili jamvi huwa zinapitia kwenye bwawa ndipo zitufikie au kuna uhusiano gani hapo?

    Mdau
    Cardiff

    ReplyDelete
  11. Mdau wa Cardiff hii siyo siri tena. Bro Stewy ni mnazi mkubwa wa bwawa la maini!! Wakati wako juu ya ligi alikuwa anatema cheche mpaka tukawa hatunywi maji humu ndani. Pamoja na kwamba ni miezi miwili imepita tangu mwaka mpya uanze lakini nimeona bora nimtumie salamu zangu na heri ya mwaka mpya!! Ngoma ya kitoto haikeshi!!

    ReplyDelete
  12. VICHWA VYA WENDAWAZIMU WACHENI VIONGEE KWANI SASA TUNAAMINI ULIMWENGU UNA VICHAA WENGI KWANI HATA RONALDO HAMKUTAKA KUMKUBALI KUWA WORLD PLAYER BT MAKAPTENI NA MAKOCHA WA FIFA WAKAWASUTA NA AIBU IKAWAPATA,PILI MKASEMA ENGLAND MAN-YU INAPENDELEWA JE UEFA CHAMPION ILIPENDELEWA PIA? AU LILE LA WORLD CLUB CHAMPION PIA MAREFA WANAIPENDELEA MAN-YU? JAMANI BASI ULIMWENGU WOTE MNYANYUE MIKONO PIA NANYI MPENDELEE KUISHAMBIKIA MAN-YU KAMA NDIVYO MAANA KOTE INAPENDELEWA,VIVA FOREVER MAN-YU DAIMA TUTASHIKA.
    MDAU K,UK BANANA

    ReplyDelete
  13. Mdau,
    Sio kila timu ikibebwa itakuwa sawa na Man U.
    "Mbuzi ni mbuzi tu hata akipewa mabawa hawezi kuwa ndege"
    Karibuni kwa mzee Ferguson kutakuwa na MINUSo kuanzia end of March
    Mdau.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...