kanda bongoman
wazee wa pamba wakiwa kazini

Salaam Wadau,
Wakati ijumaa hii ikipamba moto kwa burudani kibao hapa jijini Dar, Wazee wa Ngwasuma "The Dream Team" FM Academia wao watakuwepo ndani ya ukumbi wa VATICAN CITY HOTEL - SINZA, show hii inafuatia baada ya maombi ya wapenzi wa Ngwasuma kuomba bendi hiyo kupiga tena baada ya kuwakonga mioyo washabiki hao wiki kadhaa zilizopita.



Katika show hiyo pia kutakuwa na suprise visit ya mkongwe wa muziki wa siku nyingi Kanda Bongoman ambaye atapita tu kusalimia akielekea katika show yake huko msasani club.



FM Academia imejiandaa kupiga nyimbo mpya sita ambazo bado hazija sikika popote na wapenzi wa Ngwasuma leo ijumaa 20/03/2009 watapata nafasi hiyo ya kipekee.


Hii ni katika pasha moto ya safari yao ya Uingereza mwezi ujao ambapo watasherehekea Pasaka pake Reading tarehe 12 aprili, 2009 na kabla ya siku hiyo tarehe 11 aprili, 2009 watakuwa birmingham.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. HIZO NYIMBO MPYA ZA NGWASUMA MIE NIMEZISIKIA KWENYE KAMBI YAO YA MAZOEZI. KAMA NYIE HAMJAZISIKIA, POLENI KWANI NI ZA KUKATA KWA SOKA BUTU. HAHAHAHAH TEHEHETEHEEHEHEE

    ReplyDelete
  2. Kanda Bongo man kasafiri na visa gani?? This is another no show!! Trust me

    ReplyDelete
  3. Natumaini hatatuachia familia zilizopeana talaka kama ilivyokuwa miaka ile kule nchi ya jirani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...