HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE
1938-1984

KESHO APRILI 12, 2009 ITAKUWA IMETIMU MIAKA 25 KAMILI TOKEA WAZIRI MKUU WA ZAMANI HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI HUKO DAKAWA KATIKA NJIA KUU YA MOROGORO-DODOMA.

KWA MUJIBU WA TAARIFA YA FAMILIA YA HAYATI SOKOINE, KESHO HAKUTAKUWA NA HAFLA RASMI YA KUKUMBUKA MIAKA 25 YA KUFA KWAKE BALI SALA MAALUMU ZITAFANYIKA KATIKA MAKANISA YA ST. PETER NA ST. JOSEPH  JIJINI DAR NA PIA KATIKA KANISA LA ROMAN CATHOLIC MONDULI JUU WAKATI WA IBADA YA PASAKA HIYO KESHO.

TAARIFA HIYO IMESEMA KWAMBA HAFLA MAALUMU YA KUMBUKUMBU YA MIAKA 25 YA KIFO CHA SOKOINE IMEPANGWA KUFANYIKA AGOSTI 1, 2009 HUKO MONDULI JUU, NA KWAMBA TAREHE YA HAFLA HIYO IMESOGEZWA MBELE KWA KUWA KESHO NI PASAKA NA WENGI WANAOTEGEMEWA KUHUDHURIA WATAKUWA KATIKA MAJUKUMU YA SIKUKUU YA PASAKA.

AGOSTI 1, 2009  NDIYO SIKU YA KUZALIWA KWAKE  HAYATI SOKOINE NA FAMILIA IMEONA ITAKUWA VYEMA HAFLA MAALUMU  YA KUMKUMBUKA IFANYIKE SIKU HIYO.

PAMOJA NA MAMBO MENGINE HAYATI SOKOINE ATAKUMBUKWA KWA UCHAPAKAZI ULIOTUKUKA PAMOJA NA KUCHUKIA NA KUKEMEA UFISADI WA AINA YOYOTE KIASI HATA RAIS WA WAKATI HUO MWALIMU NYERERE ALIMTEUA MARA MBILI KUWA WAZIRI MKUU. NA KWELI MAFISADI WALIKIONA CHA MOTO. HAKUKUWA NA MASIHARA KABISA ENZI ZAKE.

JIKUMBUSHE MAMBO YA HAYATI SOKOINE 
NA



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. those minbuses were called daladala because were charging 5sh coin which was equivalent to 1us dolla by that time. hence daladala emerged as a nickname.

    ReplyDelete
  2. Tunammisi sana, alikua waziri wa watu na sio waziri wa ufisadi.
    Edward na Amina Chifupa mkae mahali pema peponi.

    ReplyDelete
  3. EDWARD MORINGE SOKOINE,HOLLASI KORIMBA VIFO VYAO VIMEILAANI TANZANIA WAO WALIKEMEA RUSHWA
    WATU WAKAWATENDA MAMBO BASI TOKEA HAPO HII NCHI NI RUSHWA MTINDO MMOJA KWANI MTU AKISEMA WANA MFANYA MAMBO KUMBE KILA MTU NI KUKAA KIMYA NA KULA VYA WAVUJA JASHO

    HALAFU UKIICHUKIA NCHI WANAANZA KUSEMA ETI MKAATAA KWAO NI MTUMWA BORA NIKAWE MTUMWA KWA WATU KULIKO KUWA MTUMWA NYUMBANI KWENU.

    ReplyDelete
  4. TANZANIA INABIDI IHUNGAME KWA MAMBO ILIYOWAFANYIA VIONGOZI WALIOKUWA NA MOYO NA NCHI NASEMA HAYA KWA UCHUNGU TOKA MOYONI MWANGU
    LEO TUNAKUMBUKA YESU ALITUFIA MSARABANI JANA SASA BASI
    KAMA KWELI MNATAKA KUITOA RUSHWA TANZANIA INABIDI IHUNGAME KWA VIONGOZI WAPINGA RUSHWA WALIOKUFA KWA VIFO VYA AJABU AJABU SISI WOTE SI WATOTO TUNAJUWA YALIYOPITA ILA KUFANYA HIVYO HUENDA WALE WATU KULE WALIKO WATAISAMEHE NCHI NA MAMBO YAKATUENDEA VIZURI.

    MR.MICHUZI NAOMBA USIYABANIE MAONI YANGU HAYA NI MAONI TU.

    TUSIENDELEE KUFANYA UNAFIKI NA WALIOTUTANGULIA WANAONA NA TENA TUNAVITA KUBWA YA KUPIGANA NA RUSHWA HATA RAIS WETU INAMPA TABU KUONGOZA NCHI ILIYO JAA RUHWA IMEKUWA VIGUMU KUITOA RUHWA NA IKITOKEA RAIS KIKWETE MIAKA KUMI YAKE IKAISHA BILA RUSHWA KUISHA SIDHANI KAMA KUNA RAISI ATAKUJA KUITOA RUSHWA TANZANIA

    ReplyDelete
  5. alikuwa mzuri wa sura,tabia,roho,na mchapakazi we real miss you

    ReplyDelete
  6. siamini kama hatunaye mtu mzuri vile jamani ama kweli wema hauna maisha

    ReplyDelete
  7. Mungu ampe raha ya milele mpiganaji huyu shupavu bila mfano hapa Tanzania.

    ReplyDelete
  8. Kumi na mbili tarehe, aprili nane nne,
    ilikuwa si sherehe, kufariki sokoine,
    mkemea walanguzi, waangushao uchumi.
    Kiongozi mshiriki, nchi kuitembelea,
    mtatua kila dhiki, nchi ipate pendeza.
    bado tunaomboleza, kifo chake sokoine.

    Wa bara na visiwani, nisikieni jamani,
    kupitia redioni, niliona kama ndoto,
    na katu sikuamini, nikauliza jirani.
    Kiongozi mshiriki, nchi kuitembelea,
    mtatua kila dhiki, nchi ipate pendeza.
    bado tunaomboleza, kifo chake sokoine.

    alitokea dodoma, kwenye bunge kujadili,
    sheria zenye hekima, pia kujibu maswali,
    akija daresalama, akapatwa na ajali.
    Kiongozi mshiriki, nchi kuitembelea,
    mtatua kila dhiki, nchi ipate pendeza.
    bado tunaomboleza, kifo chake sokoine

    ReplyDelete
  9. Yaani nilikua mdogo sana lakini bado nakumbuka nilikua wapi alivyofariki huyu waziri....First time kumwona mama yangu analia....

    ReplyDelete
  10. Nakumbuka nilikuwa na miaka 10 wakati ule ilikuwa nadra kusikia msiba.
    Tulimpoteza kiongozi shupavu na kamwe hatutapata kama yeye. Waliopo ni mafisadi tupu!

    ReplyDelete
  11. Eee Bwana Mungu mpe pumziko la aman MTanzania shupavu mpenda ukweli asiyekuwa na majungu wala tamaa ya madaraka wala pesa..... Moringe, waTanzania tutakukumbuka!!! Pumzika Baba!!

    ReplyDelete
  12. Nyie ni washenzi sanaaaaaaaaaaaaaaa, Nimetuma comments yangu jana hamjaiweka watu wakaisoma wakaona kuwa tunajua waziri ni mafisadi # 1. Basi na nyie mnahusika. Ningekuwa nimeongelea mambo ya ngono hapo mgeiweka sasa kwa vile najua siri za viongozi wenu jinsi wali mafisadi mmezitoa. Lakini tutaandamana hadi Ikulu.

    Viongozi wenyewe wanatuchafulia nchi yetu.

    Tena mkome kabisa.

    Huyu alipigania nchi yetu kwa kila jasho lake uhakikisha kila mtanzania anapata haki yake.

    ReplyDelete
  13. Yaani ungelikuwepo kila mtanzania angelikuwa anatapata haki yake. Tunakulilia sana. GUSA vilio vyetu.

    Malaika wa Bwana akulinde na uendelee kupumzika milele. Amini

    ReplyDelete
  14. Nikitaka kukumbuka Marehemu Sokoine alifariki lini huwa naimba mwanzo wa wimbo huu, maana enzi zile huwa hii ilikuwa inatoka ktk mtihani wa Siasa, nilipoona hii post nikauimba ili nijue kama tushafika au tumeipita siku hii, nimeuimba tu na mara nnaouona wimbo, big up mdau uliyetukumbusha wimbo huu. Nilikuwa la tatu A pale muhimbili primary , dah.
    Yule dereva yupo wapi aliyesababisha ile ajali???

    ReplyDelete
  15. Nilikuwa Masange JKT wakati huo. Nilikuwa najiandaa kwenda kwenye zamu ya ulinzi, halafu tuliitwa mbele ya ofisi kuu. Tukaambiwa hiyo habari ya kusikitisha.

    Na kweli yule dereva Dumisane sijui yuko wapi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...