madaraka selemani 'mzee wa kiminyio'

UONGOZI WA FANJA SPORTS CLUB HAPA OMAN UNAPENDA KUTOA SALAMU ZA DHATI KWA MCHEZAJI WAKE WA ZAMANI MADARAKA.  MADARAKA SELEIMANI ALIKUWA NI MCHEZAJI ALIEPATIA SIFA SANA TIMU YA FANJA YA HAPA OMAN. 

MECHI YAKE YA MWANZO ALIPOICHEZEA FANJA - INAKUMBUKWA NA WATU WENGI - KWANI GOLI ALILOFUNGA ILIKUWA KARIBU UMBALI WA METER 35.  ITAKUMBUKWA MWAKA HUO ALIWEZA FANJA KUCHUKUWA UBINGWA WA OMAN.  YEYE NA MAREHEMU RAMADHAN LENI WALING'ARA SANA KATIKA TIMU HII.  

WENGINE WALIOKUWA PAMOJA NA MADA NI AHMED AMASHA, HILALI HEMEDI, TALIB HILAL, ZAHOR SALIM , ABDUL WAKATI NA BAADAE WACHEZAJI ATHUMANI CHINA, YUSUF TIGANA, SHAABANI RAMADHANI, RAJABU SHAMTE WALIWAKA SANA KATIKA KUIENDELEZA FANJA. 
 
ALIKUWAS MFUNGAJI BORA WA LIGI - NA KWA NIABA YA WAPENZI NA VIONGOZI WA FANJA SPORTS CLUB YA OMAN - TUNATOA SALAMU ZETU ZA DHATI KWA VETERANI HUYO AMBAYE SASA AMESTAAFU SOKA. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Hawa Fanja walikuwa hawanunui wakristo ?

    ReplyDelete
  2. Jamaa kweli alikuwa moto, hata Yanga wanamuota hadi leo alikuwa akichukua mpira anawakusanya anavyotaka. Nadhani hata sasa pamoja na umri mkubwa akipewa wingi ya kulia sioni mtu wa kumzuia pale yebo yebo!!

    ReplyDelete
  3. Mdau wa kwanza usilete udini. inaonekana umetawaliwa na udini, hata hao wachezaji wenyewe watakushangaa. Kila jambo unatanguliza dini mbele wewe si mpenzi wa mpira, labda mlokole. Kwani hao wachezaji walikuwa wabovu?

    ReplyDelete
  4. Walitakiwa wamtumie BARUA ama wampigie simu. Kama haingii katika 'Blogu ya Jamii" atapataje ujumbe. Pia wasimuenzi kwa maneno tu, wanaweza hata kuitisha mechi ya "Veterani" mapato wamkabidhi na wengineo.

    ReplyDelete
  5. kalaghabaho, FANJA hujawahi kumsikia INNOCENT HAULE aliyekuwa akiichezea small simba? acheni udini.

    ReplyDelete
  6. Mzee wa Kiminyio alikuwa noma. Anastahili pongezi zaidi kwa kuweza kucheza soka la kiwango cha juu katika umri mkubwa. Kuna mechi alienda kuichezea Taifa Stars huko Botswana au Swaziland nafikiri, mwandishi wa habari alipomwona akashangaa kwamba bado anachezea timu ya taifa. Aliendelea kushangaa zaidi alipomwona akifanya vitu uwanjani.
    Mastriker wa kibongo, nendeni kwa mzee wa kiminyio mkachote hazina ya maarifa kwake. Huyu alikuwa akiwepo uwanjani mashabiki tunajua kuna bao.

    ReplyDelete
  7. TOENI HELA BASI IL TIMU TUIFUFUE TENA,WACHEZAJI BADO WAPO WA UHAKIKA NA KUWEZA KUIREJESHEA TIMU YENU JINA LAKE LA ZAMANI,KAMA MUKO OK WEKA ADRESS YAKO ILI TUWASILIANE NA WEWE TUKULETEENI VIFAA VYA UHAKIKA ,ILA TU MLIPE KWANI SOKA NI HELA,MUKISHINDA UBINGWA NA KUFIKA MBALI KOMBE LA ASIA,HELA KIBAO MUTAINGIZA,FUFUENI TIMU KWANI HELA MNAYO ILA UBAHIRI TU NDIO UNAKUSUMBUENI,ANYENI SASA HISTORIA HIO HISTORIA INATAKIWA IZIDIWE NA KITU CHA LEO,WACHEZAJI WAPO WENI WAZURI TU,HERA MNAYO KWANINI MUDORORE HADI LEO.

    ReplyDelete
  8. HAPO MBONA UMEMSAHAU GAGA RHINO,NA METHOD MOGELLA,NA WENGINEO

    ReplyDelete
  9. MNAMKUMBUKA JINSI ALIVYOWASAIDIA. JE NYIE MLIMFANYIA NINI CHA MAANA KWASABABU NAMUONA MECHOKA KISHENZI?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...