ALIYEKUWA mkurugenzi wa utumishi na utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatus Liyumba (pichani kulia) pamoja na Meneja miradi wa Benki hiyo Deogratius Kweka (pichani shoto), wanaokabiliwa na tuhuma za kutumia vibaya madaraka waliyonayo, wameachiwa huru na mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya mahakama hiyo kufuta hati ya mashtaka iliyotumika kuwashtaki.

Maofisa hao wa BoT waliokuwa wakishtakiwa kwa tuhuma za kuisababishia serikali hasala ya zaidi ya Sh Bilioni 200 kupitia ujenzi wa majengo pacha ya Benki hiyo, waliahiwa na mahakama hiyo kulingana na na kifungu namba 128 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.

Hata hivyo mahakama hiyo baada ya kuwaachia maofisa hao, walikamatwa tena na jeshi la Polisi kulingana na kifungu hicho cha sheria kuruhusu upande wa mashtaka kuwakata na kuwatengenezea hati mlpya ya mashtaka.

Kutokana na kukamatwa huko upya, washtakiwa hao walipelekwa katika kituo cha Polisi cha kati, mpaka hapo hati ya mashtaka itakapoandaliwa ambayo itatumiaka kuwashtaki washtakiwa hao upya.

Awali upande wa utetezi katika kesi hiyo, uliwasilisha mahakamani hapo maombi ya kutaka washtakiwa hao waachiwe huru kwasababu ya kukosewa kwa hati hiyo.

Ombi hilo lilipingwa na upande wa mashtaka katika kesi hiyo, uliodai kuwa washtakiwa hao wanatakiwa kuachiwa kwa kufuata kifungu namba 128 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, ili hati mpya iweze kuandaliwa.

Kufuatia mabishano hilo, mahakama imelikubali ombi la upande wa mashtaka la kuwaachia huru kwa kufuata kifungu hicho cha sheria, kinachoruhusu washtakiwa hao kukamatwa upya pindi mahakama inapo waachia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 27, 2009

    jamaani hakuna kuleana hapo, na kuendeleza kufuga ujinga huu mpaka lini,hawa watu wachache ndio wanangusha sana mataifa ya africa,na taifa letu kiujumla ndio maana kila siku tunaitwa watu wa ulimwengu wa tatu, kwa sababu ya tabia kama hizo, na hii inakua inaendelea isipolekebishwa

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 27, 2009

    SASA KWELI TANZANIA IMEISHA!!WANAACHIWA HURU KWA VIPI?HELA ZILIENDA WAPI WAKATI WAO NDIO WALIOKUA MADARAKANI!JAMANI KWEL HII NI RUSHWA IMETOLEWA

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 27, 2009

    Jamani inatia uchungu sana kuona kesi yenye hisia za watanzania wote wenye uchungu na nchi yao zinakuwa na danadana sisizo isha.Hivi inakuwaje kesi nyeti kama hii hati ya mashtaka inakosewa? au ndio ufisadi mungine ndani ya vyombo vyetu vya sheria?kesi ya hasara bilioni 200 kwa serikali hati inakosewa!hivi hatuoni kama ni hasara kuendesha kesi za aina hii? tunawalinda hawa, tunawalisha na tunawasafirisha kwa pesa ya walipa kodi.mimi naomba hata uwezo wa hawa waendesha mashitaka uchunguzwe nahisi ni vihiyo wa sheria,na polisi uwezo wa kuandaa mashtaka ni mdogo hivyo kazi hiyo wapewe wataalamu wa mambo ya sheria.mbona kesi ndogo tu rushwa laki saba zinakamilika haraka na hakuna hati inayokosewa.nchi hii watafungwa masikini na mafukara tu.tajiri hafungwi, tutaendelea kuonyeshana kiini macho ili kuwafurahisha wahisani tu.Hizi kesi zote kubwa ni usanii tu unafanyika, ushahidi upo wazi ya nini kuzunguka? wahasibu wakigushi wanafungwa,polisi manesi wakila rushwa wanafungwa, mahakimu wa mwanzo pia mbona inakuwa ngumu kwa MAFISADI?

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 27, 2009

    That is so strange!!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 27, 2009

    Ndivyoo itavyo malizwa

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 27, 2009

    duh bongo ni noma, evresing is possibo...

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 27, 2009

    WIZI MTUPU

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 27, 2009

    whats the point?
    wako wapi kina Mramba, Mgonja na Yona?
    whats is gonna happen to Rostam Aziz?
    PURE 100% Rubbish

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 27, 2009

    Tangu lini fisadi akafungwa?kesi zitakwendaaaaaaa,mwisho wake zitazimika tu. hiyo ndio hali ya Tanzania.

    ReplyDelete
  10. Wengi tulijua hili ni changa la macho.Bado kina nanilii nao waachiwe huru.
    Btw- kiswahili fasaha ni hasara si hasala.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 27, 2009

    broo michuzi habri za leo ?

    hii habari haishangazi sana na wengi wataachiwa huru . haya ndo matokeo ya kuundwa kwa tume zisizo na faida kwani wahusika watume elimu yao ndogo pengine haipo kabisa kwa maneno mengine ni mambo ya kiushkaji ndio haya.

    sasa serikali waandae jinsi ya kukwepa kuwalipa fidia hii serikali ni aibu !

    ReplyDelete
  12. afande midakoMay 27, 2009

    msitake niamini wadau waliokuwa wanatoa maoni jamaa walipokamatwa kwamba ni janja ya jk kuwanyamazisha watu, na wapo walioapa kwamba hamna lolote litalotokea kwa jamaa, nawengine walisema bloguni "hapo utasikia tu ushahidi hakuna".

    wengine uliona wapi kigogo akafungwa jela?

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 27, 2009

    NDIYO BONGO HIYO??

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 27, 2009

    Sasa mashitaka mapya ni yapi? Hivi viswahili vya shera ......zungusha zungusha mara wanahukumiwa tena na vijikesi visivyo na kichwa wala mkono.... mara kesho utasikia ......utasikia mvua moja basi wametoka na wanakeep mahela yote waliyoyaiba....hicho kifungu 128 walichoachiwa kinasemaje? Na sasa hivi wamewekwa kwa mashitaka yapii? Tuelezwe wazi kwa vili wanataka maji yapoe tu halafu kesho wako mitaani na mambo yanaisha

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 28, 2009

    Unajua ndugu zangu mimi nafikiri sasa tusimlaumu JK, nafikiri tuwalaumu office ya mwanasheria wa Serikali kwasababu zifuatazo:-
    a) JK kashawapeleka mbele ya Haki
    b) Wanasheria wanafanya intentionally very unprofessional mistake wajinga wanaachiwa inauma sana
    c) Tatizo ni "Experts kwenye ofisi, wataalaamu watatumaliza kuanzia kusaini miktatba, kuachia wahalifu ..etc
    d) uozo mtupu mungu saidia

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 28, 2009

    Utasikia serikali imeshitakiwa kwa kuwachafulia jina, na wanadai fidia ya sh bilion 200 + gharama za kesi.
    Wajinga ndio waliwao.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 28, 2009

    Sasa mwendesha mashtaka wa serikali ajiuzulu kwa nini alifungua kesi isiyokuwa na miguu wala kichwa na serikali itaishia kuwalipa hawa watu kwa kuchafuliwa majina. Kwa msaada tu kidhibiti cha ufisadi ni hizo bilion zao za dhamana.

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 28, 2009

    Hadi leo sielewi hiyo HASARA inayozungumziwa hapo ni ipi?

    Mbona majengo yamejengwa tena mazuri tu, hata IMF nasikia wamepanga humo humo? Na isitoshe BoT ili-host mkutano wa dunia kwenye ukumbi wao ambao hakuna mfano wake hapa Tanzania.

    Cha mwisho, hii figure ya bilioni 200 wameitoa wapi wakati kazi ya Evaluation (audit) ya Majengo bado haijaisha? Kwa kufungua kesi ya namna hii tayari italeta influence katika ripoti ya wakaguzi.

    Wanaoshitaki wakubali ukweli kwamba WAMEKURUPUKA.

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 28, 2009

    Hapa watanzania tunafundishwa kitu kimoja ukitaka kuwa na maisha mazuri bongo kuwa Fisadi tu ndio system now. Ukipiga pesa pesa kubwa km billion 200 hufungwi. kwanza unakuwa maarufu; pili ukienda mahakamani kesi inaisha pole pole .we unaendelea kupeta. Ila ukiiba kuku au simu utafungwa maisha. Sasa ujinga gani huu mtu anaachiwa huru analeta hasara billion 200 estimation. Na bado mtamuongeza pesa Utajili kwa kumlipa Fidia. Tunakwenda wapi? Nyerere na Sokoine hupo mlipo tuombeni nchi imekwisha ,nyie wawili ndio Viongozi niliowakubali

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 28, 2009

    Kaka,Michu
    Nani mtoto asiyeelewa kama hii ni serikali iliyojaa ushkaji,usanii na ufisadi uliokithiri?
    Kinachofanyika ni kupoteza maboya tu,na kuwadanganya watanzania,lakini hakuna jipya litakalotokea.
    Kifupi,JK na serikali yako tumechoshwa na usanii wenu.

    ReplyDelete
  21. AnonymousMay 29, 2009

    Na mmiss SOKOINE period

    ReplyDelete
  22. AnonymousMay 29, 2009

    BONGO TAMBALALE...
    MAHAKAMANI MAIGIZO...
    DODOMA ZE COMEDY

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...