mdau martin akiwa nou camp nou

Mheshimiwa nanihii pole na majukumu ya kitaifa
Napenda kuungana na watanzania wenzangu duniani kushangilia ubingwa wa Barcelona Fc timu ambayo mimi ni mkereketwa sana.

Hivi majuzi i nilikuwa kwenye vekesheni huko Spain nikaenda Camp Nou( Barcelona Stadium) kucheki game ya Barcelona VS Real Zaragoza. kitu kilichonishangaza baada ya kuingia ndani waspain wengi walikuwa wakiniuliza kama mimi ni tajiri,na walikuwa wakiniomba tupige picha na mimi kwa wingi.

Baada ya wao kuniuliza kama mimi ni tajiri nami nilikuwa nawaliza swali kwa nini wananiuliza kama mimi ni tajiri? Wakawa wanajibu kuwa sehemu niliyokaa(mbele kabisa karibu na ground)kuwa ni gharama sana kununua tiketi. Watanzania wenzangu hapo nyie mnapata picha gani?
ina maana waafrika waliokuwa Spain huwa hawaendagi Camp Nou? au Waspain wanaubaguzi na hawakupenda mimi kuwa pale?
Naomba maoni yenu,na napenda kusikia kwa watu wenye uzoefu na hilo.
Mdau
Martin

mdau akipozi na mashabiki wa barca
kila mtu alitaka kupiga picha na mdau



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 30 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 28, 2009

    tutajuaje kama na wewe ulikuwa uwanjani? hayo mengine ni bla blah blah!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 28, 2009

    Walikuwa wanakuuliza kwa sababu walikuwa na wasiwasi na wewe, wengine walifikiri wewe ni GHOST, au mafia au mwizi. Hapa umekuja kuuza sura wewe huna dili, sema kama unatafuta mke/bwana acha kuzunguka mbuyu

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 28, 2009

    Lengo haswa ni kutaka kutuonyesha kuwa ulikuwa Spain,na kwamba ulikwenda Nou Camp kucheki boli. that's it. nothing else!!! haya tumepata ujumbe mtaalam. hilo swali wala si ajenda yako!!! ingeku ni ajenda ungeweza kuuliza hata bila ya kutuwekea picha!!! halafu pia umetaka kutuonyesha kuwa unazo na unajua kuzitumia!!! shenzi mkubwa we!!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 28, 2009

    Yani NANIHII leo kawa mdogo sana, mbona huandiki chochote kuhusu boli la jana? pole mheshimiwa, ndo mpira huo, wanaume leo wako chaliiiii...tumewawowa!!! tuko hanemuni...

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 28, 2009

    tajiri hawi wa mwisho kutoka uwanjani, we ndio uliwaomba kupiga nao picha, wangekuwa wabaguzi wangepiga picha na wewe?

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 28, 2009

    hivi inakuwaje kuwa mkereketwa wa timu za ulaya? mambo ya waafrika ovyo kweli

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 28, 2009

    naona umepiga picha na wazungu,safi sana ujiko tosha kujipatia totoz huku kwetu,uliwaombaje lkn?au ulipiga mimi want to beat diagram with u?

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 28, 2009

    Jamani wabongo si mumpe sifa zake tuu kila kitu mnaponda khaaa!!
    Mwayego imetulia kaka kumbukumbu ambayo wengi wanaitamani.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 28, 2009

    Kwani ni bei gani vile hadi waulize????????????

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 28, 2009

    Acha upuuzi wako we kijana, hawakuonyesha ubaguzi wowote kutokana na maelezo yako, wamepiga picha na tena inaonekana mmegusana mabega kwamimi sioni kama ni ishu. Wamekuuliza hivyo ni kw sabab ya viingilio vyao jinsi vilivyo. Pia inaonekana wewe ndio umejipendekeza na kutaka kupiga naopicha kama wao ndo walitaka basi picha zingelibakia kwenye kamera zao!!!!!!! usiniambie eti ulitumia sim!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 28, 2009

    Am bit confused!Hoja ilivyowasilishwa ndiyo inanichanganya.Je hiyo picha kama waliomba kupiga nawe walikutumia ka e-mail ama nawe ulikuwa na Camera yako ukapiga ndiyo ukaileta kwa blogu hii.

    Swali lako ni la msingi sana, inawezekan jinsi ulivyoliwasilisha ndiyo mapokeo ya jamii nzima ya blogu hii. Ni kweli mimi niliishi Ujerumani,Bremen muda mrefu, kila mara ukienda uwanjani ilikuwa ni nadra sana kukutana na Waafrika. Na waafrika wengi nchini Ujerumani hutokea magharibi ya afrika, kazi kubwa ni kuuza madawa ya kulevya kwenye vituo vya Treni(Hauptbahnhoff).Hivyo taswira iliyojenga mingoni mwa jamii ya Wajerumani wa miji mingi, waafrika ni wauzaji wa mihadarati. Na wauzaji hao si rahisi kuingia Mpirani.

    Hii inawezekana hata mji uliopo uwanja huo wengi wanabangaiza maisha kama kwinginepo. More confusion is that When I was living in UK pia wazungu wakitaka Bangi mara kwa mara watakuuliza kama unauza marijuana.

    Dr. Confusion

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 28, 2009

    man u hoi huo ndo ujumbe du afasali maana hata maji hatunywi tumelala safi thanks Messi best player of the world Ronaldo hoi.

    Arsenal Supporter.

    UK

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 28, 2009

    familia yako haitafarijika wala kunufaika na hizo kumbukumbu zako. watoto wako hawata kuelewa pindi wanakuomba ada kwa ajili ya shule wewe badala ya kuwapa ada unawaonyesha hizo picha ulizopiga ulipokuwa ulaya... acha ujinga! tungekuona wa maana kama ungetuonyesha mali ulizochuma huko ulaya ili nasi tupate mwamko... sio unauza sura sijui nimepata marafiki wa kizungu, hata email zao ninazo, hawa hapa nimepiganao picha nilipokuwa nou camp wamesema wakija africa watanitafuta... acha ujinga wewe africa ni kubwa!

    Nondo

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 28, 2009

    Picha tunayoipata hapo ni sawa tu na hiyo waliyoipata hao wenyeji wa hapo na wazoefu (wazungu).. kuwa wewe ni Tajiri..
    Unahitaji nini tena ndugu kama wenyeji ndio wameshatoa tathmin na kuona hivyo.. sisi huku tutasema nini?? hakuna ubaguzi hapo.. unajistukia tu.. wasingekubali kupiga picha..

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 28, 2009

    Wabongo acheni ubaguzi, yaani kabla hamjabaguliwa na wabaguzi wa rangi nyie tayari mshajiona si kitu, pumbaffff.

    Na wewe uliyeleta picha zako pole sana maana umeleta kwa furaha lakini umeweka kwenye nyumba ya watanzania wengine wasio wastaarabu

    ReplyDelete
  16. Hivi ukienda kuangalia mechi ya Simba na Yanga uwanja wa taifa familia yako inafaidika vipi na kumbukumbu ya wewe kuwepo pale.Watu wengine huwa mna "donge" la ajabu sana.Kama jamaa ka-afford kwenda spain na kuangalia mechi nyie kinachowauma ni nini.Wengi wenu mliompiga madongo mshikaji hamuwezi hata ku-afford tiketi ya ndege.
    Nirudi katika swali-Ni kweli tiketi ya ulipokaa mshikaji huwa zinauzwa kwa gharama sana.Na wanaozinunua huwa ni watu wenye mshiko.Unajua kuna watu duniani bado wana fikra za miaka 1700s kuwa mtu mweusi hawezi ku-afford hiki au kile.Hasa nchi hizo zenye watu weusi wachache ndo bado zipo nyuma sana.Siishi Spain lakini nasomaga visanga wapatavyo watu weusi wa huko hasa wacheza soka.Inasikitisha kuona na kusikia baadhi ya watu bado wana fikra mbovu juu ya sisi weusi.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 28, 2009

    Mimi wala sijatuma,Eti wabaguzi wamekushtukiwa,mimi nacheka tu, Nilikwambia lakini usitume ukusikia,ayasasa unaona.

    ReplyDelete
  18. Wagoloko utawajua tuu hata wakijificha kaburi utawajua tuuuuuuuuu.

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 28, 2009

    Huyu mdau michosho sana tuu! Utajifanya vipi hujui kama ni ghali kukaa mbele? Halafu unajiita mshabiki wa mpira,wakati huo huo hujui kuna viwangi ndani ya uwanja,na pia inaelekea wewe ni fisadi ama mtoto wa fisadi kwani mzungu ashtushwe na bei ya kiingilio hapo wewe umetoka Afrika wala hujui hadi unauliza,Fisadi wewe!

    ReplyDelete
  20. DAH POLE SANA KAKA,HAO NDIO WABONGO AKA HATERS NDIO MANA NCHI YETU IPO VILE VUMBI KILA SEHEMU,UNGEPELEKA KWENYE BLOG NYINGINE YA NCHI NYINGINE UNGEOSHA JINA KINOMA HAPA WATAKUUMIZA BURE HA HA!BOMBA LAKINI COZ UMETIA TEAM HAPO STADIUM DATS IT,USIJIBU COMMENTS ZAO KAMA JAYDEE ALIVYOFANYA WATAKUNING'INIZA ZAIDI!!

    ReplyDelete
  21. AnonymousMay 28, 2009

    We nawe umechemsha!!! yani demu huyo wa kitasha kifuani saa sita mwanawane ha'fu unang'aa na mabega!!!! dah ama kweli wenye bahati hawabahatiki!!! matiti hayo mtaalam huyaoni hadi umshike mabegani?? si ungeng'aa nayo tu hayo ya kifuani mtaalam!!!
    dah, haya bwana!!

    ReplyDelete
  22. AnonymousMay 29, 2009

    Kama ulisikiliza maoni ya watu waishio London wakati fulani miaka ya nyuma walisema kuwa kwanini nilipe Pound 50 wakati naziitaji kununilia chakula. At least watu wengi wanaokuwa huko ni watafutaji. Waafrica walio huko wenye pesa ni mastar au wale wanafanya kazi kwenye balozi au International organisations. Mtu baki anawaza kujenga nyumbani anasahau kuwa ndugu zake wanamwibia na kumdanganya kila siku. Ukipata nasafi itumie ndugu wa nyumbani hawana lolote ni wezi na hawajui wenzao wanavyo hangaika kupata pesa. Hapa hakuna holidays kama nyumbani lakini wezetu wanatumbua tu.

    Wenzetu wakifanya kazi ni pesa zao na familia ya karibu basi siyo kwa mara baba, mara shangazi, mara mjomba ndo kugawana umaskini na ndo maana ngozi nyeusi kuiona mle shida.

    Achana na hao ambao hawajui lolote. Tembea uone.

    ReplyDelete
  23. AnonymousMay 29, 2009

    Acha ulimbukeni wewe mdau!

    ReplyDelete
  24. AnonymousMay 29, 2009

    HAHAHAAA ULICHOKITAFUTA UMEKIPATA NA WATANZANIA TULIVYOJALIWA MIDOMO UTAKOMAAA NA UTAJUUUUUUUUUUTA KUWEKA PICHA YAKO APA

    ReplyDelete
  25. AnonymousMay 29, 2009

    DAH IKIWA KAMA WE NDIO WAMEKUCHENGUKIA KIHIVYO BASI ETOO HUWA WANA MVULIA NGUO,WE MWEHU KIMTINDO.ILA POWA UMEKUWA STAR KIMTINDO KULIKO HATA NANIHII MWENYE HII BLOG COZ MI NIMESIKIA WATU WANAKUDISCUSS MAENEO YA HUKU KWA OBAMA NDIO NIKAZAMA KWENYE NET KUCHEKI PUMBA ZAKO,POWA MZEYA!

    ReplyDelete
  26. AnonymousMay 30, 2009

    khaaaa

    ivi kuna mijanadume fala ivi??

    sasa ndo nini?toa upupu umu alaaah

    ebu tutolee sura ilo

    mwanaume pekee uko ni ETOO TU BASI

    wengine nye....e tu!!

    ReplyDelete
  27. AnonymousMay 30, 2009

    yan ungekuwa bwana'angu

    ningekuchapa MAKOFI kishenzy

    una bahati sana

    kazi kuuza sura tu

    ReplyDelete
  28. AnonymousMay 30, 2009

    watasha bwana
    ndo mana nawafagilia stms

    yan watamkosha/watamlambaa weee ngozi nyeusi adi ajione mungu

    kumbe wanakutukana kwa tusi lisilo na lugha za kibinadamu

    ona sasa uyu mdau na izo pichazz

    hahahahaaaaa

    ReplyDelete
  29. AnonymousMay 30, 2009

    Huyu mdau si lolote si chochote ni mpenda sifa zisizo na msingi,picha hizo ungemtumia demu wako ama maiwaifu wako na si kwenye globu hii murua ya jamii,umeniudhi yani ungekuwa kariba ningekulamba mbata ya uso,usituletee upuuzi hapa,unaingia uwanjani sehemu ya ghali halafu unajidai kuwa hujui,kama wewe ni tajiri sana na hujui what is expensive then nakubaliana na mdau wa hapo nyuma kuwa wewe ni FISADIII!Utashindwa vipi kujua this is cheap and this is expensive kama wewe si mtoto wa mama uliyepata tu bahatiya kuzitumbua za walalahoi....Usituletee kichefu chefu kwa kutaka misifa isiyo na mpango hapa globuni.

    ReplyDelete
  30. AnonymousMay 30, 2009

    SWALI: Je, walikupiga picha na wakakupatia kopi bila kuwaomba, au hizi ni wewe uliomba upige nao? Why are you so stupid...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...