KUTOKANA NA KWIKWI KATIKA UONGOZI WA JUMUIYA YA WABONGO HUKO WASHINGTON DC , AMBAKO GLOBU YA JAMII IMETHIBITISHA KWAMBA KUNA MAKUNDI MAWILI YANAYOTOFAUTIANA NA KESI IPO UBALOZINI KUPATA UFUMBUZI WA NI UPANDE UPI HASA UNAOSHIKA UONGOZI HALALI WA JUMUIYA, NA KWA MASIKITIKO MAKUBWA NAOMBA MSAADA TUTANI TOKA KWA WAHUSIKA KWA NIA NJEMA TU.
MSAADA NINAOOMBA NI KUKUBALIWA KUSITISHA TANGAZO AINA LOLOTE KUTOKA WASHINGTON DC HADI HAPO UTAPOPATIKANA UTHIBITISHO KUTOKA CHANZO HURU (MFANO UBALOZINI) KWAMBA UPANDE FULANI NDIO ULIO HALALI KUENDESHA SHUGHULI ZA WADAU WANAJUMUIYA YA WABONGO WASHINGTON DC.
GLOBU YA JAMII, AMBAYO NI KWA WADAU WOTE ULIMWENGUNI, ISINGEPENDA KUJIINGIZA KATIKA LIBENEKE LA UPANDE WOWOTE, HIVYO PANDE HUSIKA ZINAOMBWA KUKAA CHINI NA KUFIKIA MUAFAKA AMBAO KWA JINSI NIJUAVYO KILA UPANDE UNA WADAU WENYE BUSARA, SIDHANI KAMA ITASHINDIKANA KWANI WOTE NIA YAO NI MOJA - KUWAUNGANISHA WADAU.
HIVYO SHIME NA TUJITAHIDI TUFIKIE PAZURI LIBENEKE LIENDELEE KAMA KAWA. GLOBU YA JAMII INAZITAKA RADHI PANDE ZOTE MBILI KWA UAMUZI HUU WA KUSITISHA MATANGAZO TOKA WASHINGTON DC AMBAO NIA YAKE NI KUJENGA NA SI VINGINEVYO.
-MICHUZI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Inaelekea kwenye hizo jumuiya kuna maslahi flani hadi kufikia hatua ya kuwa na migogoro ya uongozi kama ya Simba na Yanga.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 04, 2009

    Michango ya mwezi iyo.UFISADI popote mladi wawepo Wataanzania.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 04, 2009

    HAYA NDIO MATATIZO YA KUKOSA LA KUFANYA.NA KUOTA CK MOJA MTAONGOZA NCHI

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 04, 2009

    matawi ya vyama yamegongana nini? tuliwambia matawi hayo yana mambo.

    kwani mnahitaji viongozi wa vikundi vya nini? kuweni huru mtese US, kwani raisi si OBAMA hatoshi?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 04, 2009

    michuzi acha uandishi uchwala hayo makundi yanakuhusu nini?wewe unachotakiwa ni kutoa habari tu hapa hatupigani wala hatusemeani ovyo juzi wote tulikula nyama greencastle hakukuwa za zengwe wala nini huo ubalozi unatuhusu nini?usituletee mifarakano isiyokuwepo wabongo hapa dc tunamepeana tafu kila likitokea noma huo ubalozi hatujauona hata siku moja,jumuiya hii ina katiba yake inayofuatwa siku zote utoe habari za dc utoe usitoe mpango wako sisi jumamosi tupo meadowbrooke tunajinoma,mipigo ya dc huiwezi hii tuachie wenyewe.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 04, 2009

    here we go!! hii ndio kazi ya watanzania kila walipo. kugombana wenyewe kwa wenyewe au kugombani vyeo. Hebu tuambieni ndugu zenu ni nini chanzo cha ugomci wenu? i bet ni sura ya $. Na kwa nini mnahushisha ubalozi? hamjui kama hakuna sheria yeyote ile inayosema kuwa watanzania waishio nje ya nchi wawe na jumuia yao tena iwe moja kwa kila nchi? sasa tatizo ni nini kila kundi na lianzishe jumuia yao who cares kuwa na jumuia kila mtaa.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 04, 2009

    Mpasuko wa kisiasa uko Zenji wala si DC. Watu hawana time na hayo mambo. Jumuiya inayotakiwa ni ya watanzania na sio CCM. Hao watu wa CCM ndio wanaotaka kujifanya ndio jumuiya ya watanzania DC.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 04, 2009

    badala ya kupiga box mnaanzisha migogoro, inaonekana mna damu ya kifisadi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 04, 2009

    Mimi ni Mtanzania naishi Nebraska. Nasikia eti Washington D.C kuna makundi mawili [MOJA NI LA WATU WANAOJIWEZA NA JINGINE LA WASIOJIWEZA.] Sijui ni kweli ama ni maneno. Lakini kama ipo hii ni hatari kwa Watanzania. Msianzishe ukabila kama jirani zetu Wakenya kuweni kitu kimoja katika jamii husika.

    Mdau USA

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 05, 2009

    Hii migongano ni ya kikabila au? kwani nafahamu watanzania tuna UMOJA popote ulimwenguni. Kwani huko Washington, DC kuna tatizo la nini? or just a TITLE?

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 05, 2009

    kama kawaida ya wananchi wa nchi za africa. kugombania madaraka,popote pale wapatapo mwanya.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 05, 2009

    anony wa june 4, 2:38 nakuunga mkono hawa jamaa wanadamu ya kifisadi. Waswahili wanasema jivi linamfanana mnyaji. Pesa za ufisadi ndizo zilizo wafikisha huko kwa hiyo wananaendeleza tu tabia ya wazazi wao ya kung'ng;ania madaraka.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 06, 2009

    Michu,
    Please tunakuomba pia kusitisha matangazo ya CCM-UK.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...