zoezi la kusajili namba za simu za mkononi kwa kila aliyonayo limeanza rasmi julai 1, 2009 na mchakato unaendelea vizuri kwani wenye simu wengi wanajitokeza kufanya hivyo ili kuwahi mstari-mfu wa miezi 6 uliowekwa. pamoja na mambo mengine ikiwa ni pamoja na kuonesha huduma wazitoazo kwenye banda lake katika maonesho ya sabasaba, vodacom imeweka makarani wanaoendesha shughuli hizo kama inavyoonekana pichani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 05, 2009

    Sasa wanasajili ili iwe nini?

    kwani makampuni ya simu yakizitoa hizo number hazina kumbukumbu ya nani kanunua? Wangewaambia hao wanyemakampuni watoe data za wateja wao. Au hata database za wateja hawana ili kukwepa kulipa kodi tu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 05, 2009

    Rise and fall of a kingdom

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 05, 2009

    Kuwaelimisha ndugu wasiojua kwanini kuna umuhimu wa kuandikisha au kusajili simu za watumiaji Tanzania.

    1) Tanzania simu zinauzwa sehemu bila 'line' au sim card. Hivyo, kampuni ya simu ndiyo hutoa 'line' na siyo simu wanazotumia.

    2) Makampuni ya simu huuza 'line' kupitia wauzaji wa rejareja madukani na si rahisi kujua nani kanunua 'lini' ipi.

    3) Hata ikijulikana nani ana 'lini' ipi, mwizi anaweza kutoa 'line' au simcard na kuweka yake.

    Labda simcard na handset (simu yenyewe) viuzwe pamoja au viandikishwe pamoja. Hata hivo line ikipotea ni ngumu kujua wakati imebadilishwa.

    Hapa USA simu huuzwa au hutolewa moja kwa moja na kampuni na saa zingine ni bure, gharama zake huunganishwa na huduma yote na unasaini mkataba.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 05, 2009

    utaratibu huu umewezekana india kuliko na watu bil 1,4. kule wapo makini zaidi, kwani lazima uwasilishe picha tatu, pasport size, barua toka mamlaka unakoshi, na taarifa zako binafsi. wameweza kudhibiti ujinga wa wajinga watumia simu, na matusi, na ujambazi.pia imewasaidia kukusanya kodi ya pidgio la simu.
    tanzania tuige india, hiyo ya aina hiyo sustainability sina uhakika nayo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 06, 2009

    Yote sawa, lakini mbona bei za vocha zimepanda na hatuambiwi sababu gani, vocha imeandikwa shilingi 1000/- mwenye duka anakuambia unatakiwaulipe sh.1100/- kama vocha zimepanda wabadilishe pia kwenyevocha zenyewe.
    Tumewauliza wauza maduka wanasema wao wamepandishiwa huko wanakonunulia kwahiyo inabidi wapandishe ili wapate faida. Jamani kwanini msiweke wazi! Na ushahidi upo madukani, wenye makampuni tembeleeni madukani muone?
    Hatulalamiki kupanda, ila tunalalamika ushahidi wa vocha, ulipe vingine vocha imeandikwa vingine, utabainishaje kwenye ukaguzi wa mahesabu!
    M3

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...