tizi likianza
wadau kibao walijitokeza
darasa la umuhimu wa tizi

Kaka Michuzi,
Jana (Jumapili) vikundi vitatu vya mazoezi ya viungo vya KITAMBINOMA, MAZIZIZINI BEACH EXCERCISE GROUP NA KATA PRESHA vilishirikiana kufanya mazoezi ya pamoja ya viungo katika kijiji cha Kizimkazi ( a.k.a kijiji cha Pomboo, Dolphin), kama kilomita 50 kusini mwa Zbar town.

Lengo kuu ilikuwa ni kuwahamasisha wanachi wa vijijini kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zao. Uhamasishaji kama huo ulifanyika Nungwi (kilomita 55 kaskazini mwa Zbar town) na wananchi wameshaanzisha kikundi chao huko. Mipango pia iko mbioni kwenda Chwaka na Maeneo mengine ya vijijini.

Kuna zaidi ya vikundi 15 vya mazoezi mjini znz hasa katika funkwe za Ngazimia na KizingoPicha hizi zinaonyesha jinsi mazoezi yalivyokuwa jana. Napenda kuwasilisha,

Mdau Zenjibar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Well done Michu, zoezi lilikuwa bomba sana, tulie enjoy mno, na wanachi walijitokeza kwa wingi kutusikiliza

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...