washtakwia wakiingia mahakamani. kulia nyuma ni simon jengo mbele ni thobias Nkungo, ambapo shoto ni bosco kimela
Baadhi ya washitakiwa wa uhujumu uchumi ambao ni wakurugenzi wa BoT, Thobias Nkungo (kulia) na Bosco Kimela wakitoka kwenye chumba cha Mahakama ya Wilaya Ilala, Dar es Salaam jana, baada ya kusomewa mashitaka ya matumizi mabaya kiasi cha sh. bilioni 104.
MSHITAKIWA Bosco Kimela ambaye alikuwa ni ofisa wa Benki Kuu (BoT), anayekabiliwa na kesi ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), amepandishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, akikabiliwa na tuhuma za kuhujumu uchumi.

Kimela alipandishwa kizimbani jana pamoja na waliokuwa maofisa wengine wa BoT, ambao ni Simon Jengo, Kisima Mkango na Ally Bakari, ambapo walisomewa mashitaka matatu ya kuhujumu uchumi.

Aidha katika kesi hii, Kimela na wenzake wanakabiliwa na tuhuma za kughushi na kuhujumu uchumi kulikoisababishia Serikali kupata hasala ya zaidi ya Sh Bilioni 104.1.

Washitakiwa hao, walirudishwa rumande kutokna na kesi hiyo, kutoruhusu wao kupata dhamana kwa mujibu wa sheria.waliondoka mahakamani wakiwa wamesimama katika kalandinga, baada ya kukosa siti katika gari hilo la mahabusu.

Kimela alikuwa ni Kaimu mwanasheria katika BoT, wakati Jengo alikuwa Director of banking, Mkango Deputy director currency of BoT na Bakari alikuwa Director of banking.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. BoT inaandamwa sana. Ina maana hakuna taasisi nyingine huko TZ?

    ReplyDelete
  2. What do you mean "...hakuna taasisi nyingine huko TZ?". BoT (Bank of Tanzania) is the supreme financial sector in the country, whereby all other such sectors have to go thru. it for their financial needs. BoT is the Bankers' Bank, its the Government's Bank and its the Advisor to the Gavernment.

    ReplyDelete
  3. TATIZO NI KWAMBA MASIKINI NCHI YETU INAENDESHWA KWA REMOTE CONTROL NA AUTO PILOT TENA NADHANI YA MWAKA '48. KUNA BODI YA WAKURUGENZI NA IDARA YA UDHIBITI WA NDANI YA BOT MBONA WAO HATUWASIKII WAMESHITAKIWA NA NDIO WALITAKIWA KUJIRIDHISHA NA UFANISI WA SHUGHULI ZOTE ZA BENKI HIYO.

    ReplyDelete
  4. Tatizo haooo wakurugenzi na idara ya udhibitii wa ndani ya BOT ni watu ambaooo waliwekwa kwa migongo ya wakubwa wakiwa na uwezooo mdogooo wa kielimu katika iyoo secta ,Mimi ninaona muheshimu raisii na wizara zake apitiee upya jinsi haooo wafanyakazi wa BOT walivyoajiliwa kutokana na professional zaooo,Kwa kutengeneza internal rectruitment structure mpya ya sehemu nyetii kama hiyoo ya serikali bila hivyoo watanzania na hizoo ahadii za maisha bora tutazisikia masikioni tuumpaka miaka kumi ya utawala inaisha ya JK

    ReplyDelete
  5. Bora Mzee wangu alistaafu, manake angekuwa ndani sasa hivi

    ReplyDelete
  6. Kwa kifupi hakuna ambapo ufisadi haufanyiki katika nchi yetu, hata karani anafanya ufisadi katika meza yake, ni tabia iliyoota mizizi nchini kwetu hivyo kushikwa kwa hawa ni bahati yao mbaya tu, tupo weeeeeeeeeeengi.

    ReplyDelete
  7. HUYO JAMAA ANAESEMA BoT INAANDAMWA AMELOGWA HUYO SIE TUNAMJUA WALIIBA MAPAZIA MSIKITINI WAKASOMEWA KUULWA ULWAUU 3 NA ALABADILBAYANA 1 MWACHENI AROPOKWE TU

    ReplyDelete
  8. NAJUA TRA HUKO MATUMBO MOTO SASA, NEXT JNIA-JULIUS NYERERE INTERNATIONAL AIRPORT, KAMA UNAJIJUA NI KIBAKA ANZA MAPEMA KUACHIA NGAZI.

    ReplyDelete
  9. Da,, na huyo bwana Jengo yumo muhuu.... mwimbaji mzuri wa nyimbo za dini hapo Azania Front, mungu amsaidie kwa hilo

    Mdau,, Malaysia

    ReplyDelete
  10. hii mijitu ya namna hii ndo inasababisha maisha yanakuwa magumu kupita kiasi..watoto wetu wanasoma katika mazingira magumu ya kukaa chini yenyewe yanafanya uzembe wa kuliingizia taifa hasara za kipuuzi...wacha sheria ichukue mkondo wake...lisipokufika leo kesho litakufika madhambi mengine unayoyafanya duniani malipo ni hapa hapa duniani...mtajuuuuuuta kufanya kazi na awmu ya nne.....

    ReplyDelete
  11. VYEO JAMANI DHAMANI. MSITUMIE NAFASI KUIBIA NCHI. KUWENE NA UCHUNGU NA NCHI YENU. UNAIBIA SERIKALI UNAENDE KUJENGE, KUNUNUA MAGARI, KUHONGA WANAWAKE AU WANAUME.

    MWISHO WA SIKU NA UTU UZIMA WOTE HUO AIBU TUPU NA KUANGAIKA.

    TUISHI MAISHA YANAYOENDANA NA KIPITO HALALI WATANZANIA WENZANGU.

    SHERIA NAOMBA ICHUKUWE MKONDO WAKE

    ReplyDelete
  12. JAMANI HUKO BOT WAKIANZA KUFUNUAFUNUA HABAKI MTU MAANA WAFANYAKAZI WAO WALIFANYA KUFURU NA HELA ZA UMMA. WANAMILIKI MAHEKALU, MAKAMPUNI NA MAGARI YA KIFAHARI BALAA, USEMI WA MAISHA BORA KWA KILA MFANYAKAZI WA BOT WALISHAUTIMIZA!!EEH MOLA UWAANGAZE MAFISADI WOTEEEE

    ReplyDelete
  13. Hawa ni vidagaa tu vya ufisadi, msidanganyike na lolote. Mapapa na manyangumi hayaguswi kabisaaaa. After all baada ya kesi kuendeshwa kwa miaka kadhaa watashinda. Hii ndiyo bongo zaidi ya uijuavyo. Watanzania bado tupo ktk enzi ya ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...