JK akiwasili uwanja wa ndege wa kia asubuhi ya leo tayari kufungua mkutano wa 55 wa chama cha mabunge ya jumuiya ya madola CPA) katika ukumbi wa AICC. shoto kwake ni Rais wa CPA na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania Mh. Samwel Sitta, Mkuu wa mkoa wa Arusha mh. Isodore Shirima na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila. Shoto ni Naibu waziri wa mambo ya Nje Balozi Seif

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. wamevaa masuti ya bei mbaya namna hiyo wakati MTOTO WA MKULIMA PINDA WA MIZENGO keshatoa amri Watanzania tuachane na suti?

    ReplyDelete
  2. Mheshimiwa Rais nadhani hapo unapopita panataka kufanyiwa ukarabati kidogo.
    Mdau MH
    Canada

    ReplyDelete
  3. Hivi ni kwanini maraisi wa bongo wanapenda kutembea na wafuasi mia kidogo ndio kuonyesha madaraka au nini, yaani utakuta raisi anatembea na mamia ya watu au msafara wa watu karibu ishiri ya nini yote hayo, mbona maraisi wengine ni nadra sana?

    ReplyDelete
  4. Kikwete harakisha maswala yale ya TRA, ili wala rushwa watolewe mapema na kufukushwa mahakamani, najua swala unalo unalishughulikia pole pole kama EPA, sisi tunataka ajira mpya hapa TRA.

    Mdau Mfurukutwa TRA

    ReplyDelete
  5. JK arusha!!? DICOTA vipi tena? changa la macho au?

    ReplyDelete
  6. Naona mzee wa "viwanja" leo anacheza uwanja wa nyumbani!

    Mh i hope anaona tofauti kati ya hiyo lami ya KIA na zile alizokanyaga viwanja vya wenzake!

    ReplyDelete
  7. Kaka MICHUZI kikwete kesharudi toka UGHAIBUNI dah afadhali maana alizidi sasa yeye kila kukicha UGHAIBUNI tuu mpaka noma.kila la kheri katika huo mkutano wenu.
    MDAU=UKEREWE

    ReplyDelete
  8. Uwanja wetu unahitaji ukarabati usijetoboa magurudumu ya ndege!

    ReplyDelete
  9. LEO ABC NEWS USA WANAONYESHA JINSI MAUAJI YA ALBINO YANAVYOFANYWA HUKO TANZANIA.JE HUYO KIKWETE HAONI AIBU KILA ANAPOKWENDA WENZAKE WANAMWANGALIAJE? KUANZIA 2006 HAYA MAUAJI YANATOKEA HAKUNA HATUA ZOZOTE ZINAZOCHUKULIWA...NADHANI INALETA PICHA MBAYA KWA NCHI YETU.

    ReplyDelete
  10. Mdau wa 07:45:00PM Mheshimiwa Kikwete amerudi Tanzania (Arusha) kufungua Mkutano wa CPA (Bunge la Umoja wa Jumuiya ya Madola).Kule Houston kwenye DICOTA,Mheshimiwa kikwete kawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje,Mh Bennard Membe,Balozi Sefue na watu wa TIC.

    ReplyDelete
  11. Du anacheka huku akikwepa kuangalia anapkanyaga....Janja hiyo tumeishtukia....Ila na huo umati duuuu !!
    Mzawa

    ReplyDelete
  12. Pinda akisema mnamcheka. sasa suti kali na uwanja wenye matobo vinakwendaje. tunapenda sana kuwaiga 'wenzetu' kwa suti zao lakini si kwa akili na mipango yao!!! na kwa vile tumelimbuka, hilo hatuwezi kuliona tunakalia kudhihaki hoja ya Pinda.

    ReplyDelete
  13. Huyo mdau wa 5:11:00pm anasema marais wa bongo wanapenda kutembea na wafuasi mia kidogo,nataka nitofautiane nae hiyo ni kawaida sio kwa marais wa bongo ni marais karibu wote duniani tusipende kuponda tu vitu vingine kwa vile tu imekua bongo,Bush alipokuja Tanzania alikuja na wafuasi zaidi ya mia 300 sasa rais wetu yoko na hao washikaji wachache hata ishirini hawafiki tena Arusha mmeshaanza kusema.

    ReplyDelete
  14. Hivi huo msafara wote umekuja kumpokea yeye, kweli watanzania tuna self low esteem

    ReplyDelete
  15. HIVI HAO WATU WA DICOTAUS KUMBE WALIKUWA WANATUDANGANYA MAKUSUDI HUKU WAKIJUA HAWANA COMMITMENT YA RAISI KWENDA KUFUNGUA MKUTANO WAO?

    I GUESS THEY STARTED THEIR "THING" WITH A WRONG FOOT!

    ReplyDelete
  16. Politicians' carnival/festival

    ReplyDelete
  17. nyie mnamlaumu raisi kikwete bure tuu,mnataka afanye mangapi..mntakiwa muwalaumu hao maraisi waliopita..yeye kaingia madarakani juzi tuu...keshafanya mambo kibaooo...na uwanja atajenga pia anatakiwa apewe muda...hongera raisi wetu kazi zako nyingi sana

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...