Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Mark Mwandosya akizungumza na wanahabari leo katika ukumbi wa Idara ya Habari, kufafanua juu ya uvumi ulioenea kwamba kuna watu wameweka sumu katika mto Ruvu mto ambao ndiyo una chanzo cha maji cha mtambo wa Ruvu Juu kinachotegemewa na asilimia kubwa ya wakazi wa jiji la Dar. Wengine pichani ni Kaimu katibu mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Damas Shirima, akifuatiwa na Mkurugezi wa Idara ya Habari Maelezo Clement Mshana.
Watu wanne wamekamatwa na polisi baada ya kukutwa wakiuza samaki wanaodhaniwa kuwa wamevuliwa kwa njia haramu za uvuvi. Mh. Mwandosya amesema wakazi wa jiji la Dar wasiwe na wasiwasi wowote na waendelee kutumia maji hayo kwani uchunguzi wa kina umefanyika na kugundua kwamba hakuna sumu yoyote ambayo imepatikana katika chanzo cha mtambo wa Ruvu juu ambako ndiyo husukuma maji kuja jijini.
Profesa Mwandosya Amesema eneo ambalo tukio hilo lilitokea ni sehemu iitwayo Kwala katika Wilaya ya Morogoro Kusini, akiongezea kwamba inaaminiwa lilitiwa sumu kwa lengo la kuvua samaki na wavuvi haramu umbali wa kilomita 70 kufikia kwenye chanzo cha mtambo wa Ruvu Juu.
Amesisitiza kwamba hakuna wasiwasi wowote wa kuwepo kwa sumu hiyo na mpaka sasa Sampuli ya maji iko kwa mkemia mkuu ili kubaini kama kuna tatizo lolote pamoja na kwamba uchunguzi wa awali umeonyesha hakuna aina yoyote ya sumu katika maji hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. kama ni kitu A muwe mnasema A sio ohh ta ta ta, muwe wa kweli.

    ReplyDelete
  2. Hivi hiki cheo cha umwagiliaji..kuna mashamba mangapi Tanzania ya Umwagiliaji mpaka Waziri anapewa hiyo title? Mhh duniani kuna mambo...hili nalo ni mojawapo...!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...