Banda la Tanzania kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Utalii Duniani- London, Excel Centre
Waziri wa Utalii Zanzibar,Mh. Samia Suluhu Hassan(kwanza kushoto mwa picha), Waziri wa Mali asili na Utalii Tanzania Mh. Shamsa S. Mwangunga(pili kulia),wakiwa pamoja na baadhi ya wajumbe toka Tanzania katika Banda la Tanzania kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Utalii Duniani- London, Excel Centre
Mh. Shamsa S. Mwangunga(kulia), Mh.Waziri akiwa na mshindi wa Bahati Nasibu, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii, Bwana Peter J. Mwenguo, Mwakilishi wa Kampuni ya Tanzanite, Mkurugenzi wa Kituo cha Tanzania cha Biashara – London na baadhi wa wajumbe wengine wa Tanzania. Bahati Nasibu maalum ilichezeshwa leo na kumpata mshindi, ambaye amejipatia Tanzanianite yenye thamani ya dola za Kimarekani 1500



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Ushauri kwa waandaaji wa Tanzania kushiriki maonesho ughaibuni, 'shughuli ni watu na watu ni shughuli'

    Hivyo itakuwa vyema kama taarifa hizi zinawafikia wana-Diaspora Wa-Tanzania mapema, ili tuwapashe wenyeji wetu habari kuhusu UTALII na wapi waende wakutane uso-kwa-uso na mfano wadau hao waliokuja Uingereza toka Maliasili, Tanzania tourist board n.k

    Maana huwa tunakutana na watu ughaibuni ambao wanahamu ya kwenda Tanzania lakini habari ktk mtandao ni chache, hivyo maonesho kama hayo yangetumika kikamilifu.

    Mdau
    Jijini London.

    ReplyDelete
  2. jamani wadau hivi kwa nini hili neno maonyesho watu wamekuwa ving'ang'anizi na maonesho???? kiswahili fasaha ni MAONYESHO maonesho haina taste! mbona wakati wa kutamka humsikii mtu akisema nimetoka kwenye maonesho bali huwa uatasikia nimetoka kwenye maonesho

    ReplyDelete
  3. habari wadau
    kuna mtu ana contact za Mheshimiwa Shemsa Mwangunga za London please, nimesoma na mwanawe ningependa kumuamkua,email me please
    suleimoney@yahoo.com

    ReplyDelete
  4. kwenda kutangaza utalii waziri ana kwenda kufanya nini. hata hao mabosi wa TTB hawana haja ya kuwepo. watu wanoa faa kuwepo hapa ni wadau wa utalii. mfano tour oerator wa Tanzania, tour guide wa kuongoza watalii, wamasai wakiwa katika mavazi yao ya asili.vikundi vya ngoma na vivutio kama wachonga vinyago. Nilikuwa kwenye Maonyesho ya utalii hapa marekani nchi hasa visiwa vya carribean walileta vikundi vya ngoma. chakula cha kwao,mavazi na mchanga wa pwani huwezi ukaamini. walikuwa na slides za power point zina onyesha pwani zao na maisha ya kwao full culture demonstration na hatukuona hata mtu mmjo amevaa tai au western dress akitangaza utalii wa carribean kama wanavyo fanya maofisa hao wa utalii na waziri wao. Waziri ni mtu mkubwa sana kuwa hapa hii ni marketing haihitaji mtu kama waziri. haya Kibongo bongo tu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...