Mdau George Josephat Mkoma, mfanyakazi wa Shirika la CARE International jijini Dar akijidai na mai waifu wake Violet Shija Watosha ambaye ni mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Dar. Wadau walimeremeta hivi karibuni katika Kanisa la Azania Front Lutheran jijini Dar na kufuatiwa na mnuso wa nguvu ukumbi wa City Garden Restaurant gerezani. Globu ya Jamii inawatakia kila jema katika ndoa yenu na mbarikiwe kuwa na familia yenye furaha iliyojazwa watoto pia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Michuzi lazima niseme ukweli...mimi simjui huyo bibi harusi lakini anaonyesha katulia kweli..yaani..she was really a marriage material..hongera kaka...mtunze huyo mtoto tafadhali..Lol...!!
    Mdau-USA

    ReplyDelete
  2. mmependeza sana, nawatakia kheri na baraka na maisha bora hongera mtoto wa kisukuma

    ReplyDelete
  3. Yaani hongereni sana na mmependezaaaa sanaaa, kweli binti anaonekana ametulia sana, binti endelea kutulia na Mungu akusaidie katika maisha yako ya ndoa.Of course hata bwana harusi uko poa sana uko juu, unaonekana umefika na umetulia.
    Mmependeza sana, sana nawatakia masiha mema ya ndoa

    ReplyDelete
  4. kiporo kinapashwa moto au??! mh

    ReplyDelete
  5. Hongereni maharusi Mungu awape kila la kheri...Halafu hilo li mtu gani sijui anonymous ushuzi Wed Dec 23, 09:42:00 AM linaonekana lilimmendea one of them likakosa ndo linakuja na macomment ya kiwivu wivu haters mna tabu sana.

    ReplyDelete
  6. Mmependeza sana hongereni, ingawaje ulininyima mnuso! washirika wa OLd MOshi wengi wamenilalamikia eti umewatia kapuni! HONGERENI TENA SANA.

    ReplyDelete
  7. hongereni saaana bibi arusi umependeza saana bila ya makorokoro mrembo wa asili hongera zako kwa kupata mume nyie mnaolalamika mmetoswa mngetoa mchango poleni wee mkono mtupu haulambwi hongereni saaaana maaarusi

    ReplyDelete
  8. hongereni sana vijana,mie mwenyewe nimeoa kitabu muda mrefu sana sasa nahitaji mke wa kunipa pumziko la moyo na kushirikiana ktk taabu na raha.
    mungu awabariki,ndoa ni sehemu nyeti sana na takatifu,muitunze kwa uadilifu wote mtapata maisha mema yenye baraka na stable &successiful family yenye furaha kuanzia wazazi hadi watoto. nami nikimaliza ngwe hii ya shule nitarudi nyumbani kuja kutafuta mchumba na kuoa.

    ReplyDelete
  9. mmependeza sana, Mungu akawajalie kupendeza huko kuwe pia kati yenu, kifo ndio kikawatenganishe, Mungu awabariki sana katika maisha mapya mlioyaanza.

    ReplyDelete
  10. Du mmetoka chicha kinomi,yaani mpendeza kweli na sherehe yenu iliukwa very unique niliikubari.
    Mungu asiwapungukie chochote katika maisha yenu ya ndoa na kila mnaloanza anzeni na bwana yesu.
    By E.samoja

    ReplyDelete
  11. mkeo wa kwanza yuko wapi ?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...