KWA MUJIBU WA TAARIFA AMBAZO GLOBU YA JAMII IMEZIPATA NI KWAMBA SIMBA WA VITA HAYATI MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA ATAZIKWA SIKU YA JUMAMOSI HUKO NYUMBANI KWAKE MADALE WILAYA YA KINONDONI KWA HESHIMA ZOTE ZA KITAIFA.

VIONGOZI KADHAA WA NCHI ZA NJE WANATARAJIWA KUHUDHURIA MAZISHI YA SHUJAA HUYU AMBAYE ATAKUMBUKWA KWA UADILIFU WAKE NA KUJITOA MUHANGA KATIKA KUGOMBEA UHURU NA PIA UKOMBOZI WA BARA LA AFRIKA. HABARI ZAIDI ZITAKUJA KADRI ZITAVYOPATIKANA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Si rahisi kudondosha chozi lakini kwa marehemu Rashid Mfaume Kawawa sikuweza kujizuia.

    Hii ndiyo ada ya kila mja.

    Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mpe pumziko jema na apate kikao chema katika matumaini mapya.

    Amin!

    ReplyDelete
  2. mithupu inatia faraja kumuona mama salma kikwete akijichanganya na wafiwa hapo.pamoja na adamu malima na mbunge wa mafia.

    ReplyDelete
  3. Wa- ChirangiDecember 31, 2009

    Tunatoa pole kwa familia yake na Watanzania wote kwa kifo cha huyu mzee wetu shujaa.

    Faraja kuu itokayo kwa Mola wetu iwe juu yetu sote wakati huu wa msiba.

    ReplyDelete
  4. "PUMZIKA MAHALI PEMA MZEE WETU"

    Mkuu wa blogu ya jamii kwa kidirisha cha "YOU TUBE" umetuweka karibu na msafara wa msiba wa baba na babu wa Taifa letu.
    Mwenyenzi Mungu amlaze mahali pema.

    Mickey Jones-Denmark

    ReplyDelete
  5. Inna Lillahi wa Inna Ilaihi Raajiun.

    Poleni sana wana familia,mwenyezi Mungu awajaalie subra.

    Ameen!

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  6. Jamani najua tuna uchungu...lakini mbona hakuna utaratibu hapo? sasa nani anafanya nini?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...