Habari Mkuu wa Naniiiii!!!!!!! Hii ilitokea pale Lugalo jeshini (aada tu ya daraja kabla ya Makongo Sekondari). Huyo mwenye Fuso alikuwa upande wake....Bongo oye!
Nawakilisha Mdau wa Mbezi Beach

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. ankal hii ajali imetoke mita 5 hivi mbele ya gari yangu ni noumer kama siyo airbag huyu jamaa wa corrola asingefaa hata kuangalia but jamaa aliumia kidogo sana mguu na mkono na uzuri wajeshi walikuwa wanapita pembeni wakamsaidia hakuibiwa chochote wasamaria wema walimsaidi kutoka na akachukua simu yake na kuwapigia ndugu zake.RayTZ

    ReplyDelete
  2. sasa wewe mtoa habari na picha una matatizo ya akili au? sasa unashangilia bongo oyeee kwa ajali.si jambo la kufurahisha hata kidogo

    ReplyDelete
  3. duh,hio gari ndogo ilikuwa speed gani?vinginevyo imetengezwa na maboksi!!hio damage inatisha

    ReplyDelete
  4. mimi nilisoma na kuishi hapo makongo kinachoaminika hapo karibu na daraja(super market ya jeshi)huwa kuna mazingara yanayosababisha hizo ajali,,muda haupiti ni lazima damu imwagike. Hii ipo vichwani mwa watu na waliopitia hapo makongo

    sasa sijui kama ni kweli au vipi au labda kuna makosa ya kiuhandisi

    ReplyDelete
  5. TWO WORDS

    "DEFENSIVE DRIVING"

    ReplyDelete
  6. Hebu wacheni hayo ya mazingira. Huyu jamaa alikuwa anaovertake aliona atawahi.

    Huu ni mtindo uliyopo Tanzania kwa wingi sana, dereva anaovertake haoni mbele au kwenye mlima bila ya kuona mbele, anatarajia nini akipigwa mzinga?

    Pole sana lakini tujitahidi kufuata sheria za barabara.

    ReplyDelete
  7. Bongo (au Afrika) hakuna madereva. Tumevamia fani za watu bila kuwa na nidhamu na uelewa wa hivi vyombo!!

    Iweje ajali zinatokea nyingi hapa wakati magari ni machache, kinyume na ajali chache kwa wenzetu wakati magari ni mengi??

    Wewe unayesoma habari hii inawezekana umeshafoji barabarani katika masaa 24 yaliyopita.

    Bongo oyee!!

    ReplyDelete
  8. Ajali kama hii hainishangazi. Asilimia 80 ya watu wanaojifanya madereva Bongo hawastahili kuendesha magari. Watu wanajifunza kuendesha katika barabara kubwa lakini hawataki kuweka alama za 'learner'. Wengine wanakimbia barabarani utadhani ni madereva wazoefu kumbe ni madereva wanafunzi. Hivi unategemea nini?

    ReplyDelete
  9. ah!aaaa!ahhhhaaaaaaa! hii bongo tambarale inasikitisha kwa sakata la hajari za barabarani,any way bongo tambarale ya kamanda wa ffu.

    ReplyDelete
  10. We Mduanzi ni mgeni na bongo nini?Karibu nusu ya madereva wanaoendesha Dar es salaam ni wanafunzi walioanza kuendesha magari katika miaka mitatu hadi sita hivi na ni vijana wadogo wadogo.
    Wengi wanafikiri uendeshaji Dar ni bora kuwahi badala ya kuangalia usalama wa abiria na mali.
    Huyu aliyepata ajali anastahili na amepata haki yake.Sita sangaa kama ni kijana wa chini ya miaka 30.
    Wengi wamezoea kuendesha kwa kukosa ustaarabu, kutanua utafikiri sheria haipo.Heri wapatae ajali ili wapungue barabarani.

    ReplyDelete
  11. bongo tambarale la namna hii litamaliza wengi

    ReplyDelete
  12. follow the rules or die thats it, most of the people they don't care because it has not affect their life yet but once you are in that crash that is the time to go or drive with manner, you, who don't want to follow the driving rules next time don't risk or take someone else life go by your self. msiendekeze kuwa hii ni nomal huko home TZA people they need to have manners on the wheels.

    ReplyDelete
  13. Bongo noma!
    Tanzania nzima hakuna madereva wote wanajifunza kuendesha magari hata madereva wa Rais hawajui kuendesha magari na ndo maana huwa wanasafishiwa njia ili kazi yao iwe ni kunyoosha tu!
    Weweeeeeeeeeeee, bongo oyee!

    ReplyDelete
  14. ....ohh, lakini kabla hatujalaumu, tujiulize, hii toyota ni kati ya magari ambayo kampuni inayarudusha kiwandani??

    Maana nasikia kuna makosa pale kwenye accelelator pedal, inajiongeza speed kwa ghafla. Inawezekana ndiyo yaliyomsibu huyu dreva!!

    I wish amepona mwili na viungo aweze kusimulia!!

    ReplyDelete
  15. overtake this driver ni stupid

    ReplyDelete
  16. KAKA MICHUZI, HII IMENIGUSA. INAWEZEKANA KABISA HUYO JAMAA WA COROLLA ALIOMBA KUINGIA UPANDE WAKE WAKAKATAA KUMPA NAFASI,(WALIMBANIA) WATU WANA TABIA MBAYA MNO!! ROHO MBAYA!! KWANI UKIACHIA GARI MOJA KUINGIA UNAPUNGUKIWA NINI? SASA WAMEPATA FAIDA GANI KWA MWENZAO KUHARIBIKIWA NA GARI. HII TUNAITA ROHO MBAYA.............. HALAFU UTAKUTA MTU ANASALI KUOMBA BARAKA KWA MUNGU!!!!!!!!!. HUJUI HUYO JAMAA KWANINI ALIPITA HUKO. PENGINE ALIKUWA ANAWAHI MGONJWA. TUACHE TABIA HIZO JAMANI, TUSIBANIANE KWENYE FOLENI, ILA KAMA MTU HUNA KITU CHA DHARURA KAA KWENYE FOLENI.

    ReplyDelete
  17. Wote wanaowaona wezao walioko kwenye foleni wajinga na kuanza ku-overtake kwa kupita pembeni kisha kuchomeka hiyo ndiyo dawa yao tu mapaka waache sometime hata magari ya wanasheria/majaji/jeshi/serikali tunawaona wanafanya ujinga huo kama umechelewa si ungewahi jana mapema. safi sana!

    Madau xyz

    ReplyDelete
  18. wewe anon wa saa 09:33:00 mpumbavu wewe una-overtake wenzio kwa kuwaona wajinga kukaa kwenye foleni nani akukupishe kufaa huko huko si umeona wenzio wajinga kukaa kwenye foleni...na hatuwapi nafasi ya kuchomeka mapaka muishe wote kwa ujinga wenu

    Mdau xyz

    ReplyDelete
  19. We anon wa Wed Feb 03, 09:33:00 AM acha kutetea ujinga na kama roho mbaya unayo wewe!!! yaani mijitu inatanua kijinga jinga ili aje kumchomekea mwenzake ivyo waachiwe tu hiyo ndiyo adabu yao kama mtu anaharaka aondoke jana gari za kupishwa ni za wagonjwa tu! afu inaelekea ndio tabia yako sasa subiri lako laja nawewe.

    ReplyDelete
  20. Hii ndio Bongo. Mtu anachukua mkopo wa milioni 10 benki au saccos na kununua gari, lakini baada ya siku mbili tu linapata ajali na kuwa nyang'anyang'a kwa uzembe wake mwenyewe. Mbali ya kuugulia maumivu ya ajali, anabaki kuugulia maumivu ya makato ya mkopo aliyochukua kununulia gari ambalo ametembelea siku mbili tu. It can only happen in our beloved Bongo.

    ReplyDelete
  21. Dereva wa Lori ana Roho Mbaya na ni mshenzi ameshindwa nini kusimama mpaka amvae mwenzie. Ni yeye aliyemvaa jamaaa, ingawa jamaa alifanya kosa kubwa ku-overtake. Lakini lazima tuwe na utu, alitakiwa angalau asimame siyo anagionga tu kwa kuwa makosa ataandikiwa mwenzie. Madereva wa Malori wanazo sana hizo

    ReplyDelete
  22. KWA NIABA YA FAMILIA YETU NATOA ASANTE KWA ASKARI WA JWTZ LUGALO,DEREVA WA FUSO,MADAKTARI NA WAUGUZI WA HOSPITALI YA IMTU NA RAIA WOTE NA WALIOSHIRIKI KATIKA KUMSADIA NDUGU YETU ALIYEJIKUTA GHAFLA KATIKA MKASA WA BARABARANI.HILI TUKIO LINALOWEZA KUMFIKA YEYOTE BILA MATARAJIO NA HAKUNA SABABU YA WADAU KUWA MAONI HASI KUHUSIANA NA TUKIO HILI.ACHA UPENDO NA KUSAMEHEANA KUTAWALE MIOYONI MWETU LEO NA KWA UMILELE WOTE.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...