Ankal hebu check hii ni Addis Ababa je sisi tutawafikia lini?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 51 mpaka sasa

  1. Hamuawafikii, kwani ndio kwanza munakunywa chai na mafisadi.

    Hivyo tushukuru mungu tuu, tumezaliwa mafukara na wajanja wanachota mabilioni tuu kila leo...Sasa ufike wapi?

    ReplyDelete
  2. wakiacha ufisadi tuta fika tu

    ReplyDelete
  3. Good photoshopping. Adids haiko hivo.

    ReplyDelete
  4. Hiyo ni wanataka kufanya ila mpaka ikubali sizani sababu kwanza njaa tupu huko wa Afrika sie bwana mnataka makubwa madogo yanawashinda. Ethiopia wasahau hiyo kutokea. Mwinyi.

    ReplyDelete
  5. Zenu si mnapeleka kwenye banks za Uswiss? Mtafika siku mkienda kuzichukua..!!

    ReplyDelete
  6. Nani Kasema hiyo ni Addis Ababa? Subuthu! Nimefika Addis, 7 Yrs ago, there was nothing like that

    ReplyDelete
  7. uongo mtupu.

    ReplyDelete
  8. Flyover ya Addis Ababa toka mjini kati hadi Bole eapoti Addis Ababa ilikuwa kitimutimu kuimaliza,ujenzi wa hiyo flyover moja hapo Addis miaka kibao ikasababisha foleni mpaka unapata ukichaa.

    Sasa tukirudi DSM ni bora kujenga vitongoji vinavyojitegemea kwa kila kitu(satelite cities) kuanzia hospitali kubwa, huduma za mabenki, shopping malls au masoko makubwa mengi ya machinga n.k hivyo mtu ukikaa mfano Mbagala au Wazo Hill, Kimara Temboni n.k hufikiri kwenda mjini katika kwa shughuli za shopping, benki, hospitali n.k

    Pia huduma za treni za mjini juu ya ardhi, kuunganisha hizo satellite cities(kusini/kaskazini na magharibi/mashariki jijini) muhimu, Kongowe mpaka Buju na Magomeni Mapipa hadi Ruvu darajani.

    ReplyDelete
  9. Hapo kama mtu unaishi kona ya kusini mashariki halafu unahitaji kununua kiberiti kwenye kona ya kaskazini magharibi basi inabidi uingie kwenye gari.
    Kuwafikia sio kuigilizia walichofanya bali ni kufanya kitu kilicho bora zaidi. Pakiwa na maisha bora kwa kila Mtanzania popote pale alipo nakuhakikishia tupo wengi tu tutakaoikimbia Dar es Salaam na kuhamia Mtwara hadi Tanga kwa wale wanaopenda bichi. Unadhani watu wanapenda kuishi kwenye bonde la Jangwani wakihofia mafuriko? Hawapendi ila wanaona kwamba bora maisha hayo kuliko waliyokuwa nayo walikotokea.

    ReplyDelete
  10. Looh. kumbe Addis iko ivi, kweli bongo tunatia aibu, kazi kupepeta midomo kama Chupaki

    ReplyDelete
  11. siamini kama wakwe wamefikia hapo,vipilefti vya mjini vinawashinda ndo ije hayo fly

    ReplyDelete
  12. Addis Ababa haiko hivyo

    ReplyDelete
  13. Hamna kitu hapo............

    ReplyDelete
  14. Kichwa cha mwendawazimu,Hatutafuka leo hapo

    ReplyDelete
  15. MDAU TUE MAR 23,06;55 PM

    Umeongea ukweli kabisa haya mambo ya ndoto za barabara za kupanda na kushuka si ya sasahivi. Jengeni Masoko na vibanda vya wamachinga watu wapate kutokuwa na haja ya kufika mpaka Samora au kariakoo.


    Jengeni ma hospitali makubwa vituo vya treni na ma viwanda mikoani.

    Ethiopia huko msijidanganye na picha za Project kwani tukianza kuweka picha za Project Tanzania ndio hivi kuweka Blog za Nchi za Afrika zengine nao wataamini tu.

    Seif.

    ReplyDelete
  16. http://www.skyscrapercity.com/forumdisplay.php?s=2644e01eb102e51e1f2868372830c52a&f=372


    TIZAMENI HIYO LINK JUU UONE NCHI ZENGINE AFRICA WANAWEKA ZILIVYO NA PROJECT ZAO. BINYA KILA NCHI YA AFRICA UTAONA ZILIVYO. Juma

    ReplyDelete
  17. ASANTE KWA UONGO WAKO ADDIS HAIKO HIVYO HATA CHEMBE.... LABDA UNAPENDA TU JINA LA HIYO NCHI UKAWEKA PICHA ZAKO ZA KUGUSHI

    ReplyDelete
  18. why does it have to be dar ? everything planned for the country, dar pops up!! kuna msitu mkubwa sana kati ya morogoro na dodoma..i wonder the land is sitting just idle! no reason ;plans for turning that land into a strategic investment location are nowhere to be seen!! nchi imekaa tu kuneemesha wachachi kwa jina la mafisadi...

    Haya ndugu zetu kenya idara ya utalii..they are very aggressive ..opening up tourism centres across the world ..selling the country everywhere ...hapo kwetu matumizi ya kijinga tu..ukisikia kodi ya nyumba ya speaker unazirai, ukisikia nyumba ya governor unadondoka chini, ukisikia zimepotea bilioni 300, polisi hawajui, TRA wako usingizini hadi SERIOUS froud walete habari...

    sasa where are we heading??

    ReplyDelete
  19. just computerized image, not actual complete project image, but it show how much Tanzanian they like their country, kwani kuna wadau hapo juu wamakuwa wakalo hao... Amani!

    ReplyDelete
  20. Wandugu acheni kujidanganya Addis Ababa wako juu,nilifika mwaka jana sikuamini macho yangu,zamani tulikuwa tunamwita mtu mwenye shida Ethiopia,ni zana iliyojengeka kwamba Ethiopia wana njaa lakini ukifika utaona Bongo ndiyo njaa

    ReplyDelete
  21. Yap. Hapo ni Addis Ababa. Nilikuwepo January 2010. NI KWELI TUPU. KWANZA AIRPORT YAO WAMEIJENGA TENA. VERY NICE.

    ReplyDelete
  22. Wa bongo kwa kudanganyika.. hi sio Addis, wacheni kudanganya watu bwana..na uhakika na nachokisema..

    ReplyDelete
  23. ...........WIZI MTUPU........ADIS What?!

    ReplyDelete
  24. Emasegenalo Meles Zenawi! Well done! Yes that is Gutara area with those flyovers. Walianza kutengeneza hizo flyovers 2007. At last wamemaliza.
    Sisi tuzikombe tuu!

    ReplyDelete
  25. Wabongo kwa ubishi , unafiki, uvivu wa kufikiri na na kutafiti ndio maana hamendelei. Wengine wanasema photosho wengine mara nimefika hapo miaka 7 iliyopita. NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK! hapo ni Addis Ababa na hiyo project inaitwa Gotera Interchange. http://www.nazret.com/blog/media/blogs/new/Goter_Interchange.jpg. Kama link haitafunguka tumia search engine yoyote kama google au yahoo kwa kutumia neno Gotera interchange uone kabla ya kuja na ubishi usio na tija. Hayo ndio matunda ya pesa ya walipa kodi siyo ya kweni inayojenga majumba ya wenye mamlaka.

    ReplyDelete
  26. UKITAKA UJUE BONGO NZURI AU MBAYA NGOJA MVUA YA DAKIKA KAMA 20 TU INYESHE:
    JAPO SIJAWAHI KUFIKA ADIS LAKINI NAWEZA KIDOGO KUAMINI ;
    WEE FANANISHA TU AIR PORT YAO NA YETU: YETU KAMA IPO IPO TU KAMA HAINA MWENYEWE:

    ReplyDelete
  27. KWANI KUNA NCHI IKAPATA MAENDELEO IKIWA KUNA VIONGOZI MAFISADI? ANGALIA HIZO NCHI ZINA MADEGE YAKE YA UHAKIKA YANAPIGA KAZI SAFARI ZA KILA SEHEMU

    ETHIOPIA WANA MIDEGE KENYA WANA MIDEGE NCHI KIBAO ZA AFRIKA ZINA MIDEGE KIBAO

    SUBIRINI HAO BURUNDI NA RWANDA WALIKUWA KWENYE VITA KWA MUDA MREFU WAPENI MUDA MFUPI TU UTASIKIA MAKALI YAO

    NYIE ENDELEENI KUWA MAFISADI VINGOZI ZIKICHUKULIWA HELA ZAO WALIZOFISADI BONGO HATUKOSI MIDEGE YETU

    MIMI NAJUWA NCHI YETU TUNAHITAJI KUCHINJANA KWANZA ALAFU NDIO HAKI ITATENDEKA

    ReplyDelete
  28. My bad, its true that the project mentioned above was conducted in Ethiopia, and known as "Gotera interchange roads project"

    ReplyDelete
  29. Msema KweliMarch 23, 2010

    wewe mtoa maoni wa 6.35 pm, ni mpumbavu kweli kweli na ni mjinga hasa,angalia hii link halafu utuambie hiyom photoshop aliifanya babayako?k**mbigilisi.
    http://www.ethiotube.net/video/4028/Addis-Ababa-Gotera-Interchange-from-Start-to-Finish

    ReplyDelete
  30. KIJANA USHASEMA NI PROJECT.. UNAJUWA TANZANIA KUNA PROJECT NGAPI ZA PICHA KAMA HIZO? KIBAO TU MUOMBENI MICHUZI AWAWEKEE NA ZA DARAJA KULE KIGAMBONI KURASINI IPO PIA TATIZO YA PROJECT JE ITAKUJA KUJENGWA? INAKUWA USANII TU FUNDS NI NGUMU KUPATA HIYO ETHIOPIA NI PROJECT ILA KUJA KUTENDEKA NI NDOTO. KWAHIYO BADO HAKUNA KITU HICHO ETHIOPIA. WEKENI KITU CHA UWAKIKA SIO PROJECT ZA UZUSHI. MWANAWANE.

    ReplyDelete
  31. JAMANI SAMAHANINI MIE NILIKUWA KATI YA WALIOPINGA ILA CHUNGUZACHUNGUZA NIMEKUTA KWELI IPO HIVYO VIDEO NII HII HAPA. SEIF.


    http://www.ethiotube.net/video/4028/Addis-Ababa-Gotera-Interchange-from-Start-to-Finish

    ReplyDelete
  32. Video yake hiyo http://www.ethiotube.net/video/4028/Addis-Ababa-Gotera-Interchange-from-Start-to-Finish

    ReplyDelete
  33. tanzania wananchi wakipewa vitenge,t shirt,kofia na skafu za ccm basi mbio kwenda kuchagua mafisadi

    ReplyDelete
  34. WABONGO NYIE NI WAJINGA NA MTABAKI KUA WAJINGA HIVYOHIVYO HADI SIKU YESU ATAKAPORUDI..........RIDE OR DIE HIYO NI ADDIS ABABA NIMEPITA HAPO MWAKA JUZI 2008 NA HIZO FLYOVER ZAONEKANA VIZURI SANA UKIWA UNAKARIBIA KULAND NA NDEGE NA HATA UKIWA AIRPORT UNAIONA MOJA IMEKATIZA KARIBU KABISA NA AIRPORT YAO.........NYIE ENDELEENI TU KUPIGA STORI TU NA MAFISADI WENU HADI MTAKAPO GUTUKA WENZENU WANAENDA MWEZINI..........KUFA HAMFI ILA CHA MOTO MTAKIONA..

    ReplyDelete
  35. Tanzania tumelaaniwa. Mi niko radhi kutoa sehemu ya uhuru wangu kidogo.. ili tutawaliwe tena. Cha msingi kwangu ni elimu bora, huduma bora za afya, na usalama wa maisha yangu.
    Kweli.. Tutabakia na jina moja tu..amani amani.. ambayo nadhani hatuna.. au?

    ReplyDelete
  36. ubishi ni ujinga,hio ni adis ipo na si project kwenye mafile tu,labda hao viongozi wa kibongo wakiacha huo ufisadi wao na 4 once ku care wanaweza kufanyakitu kama hicho,im 27yrs old and naamini that wont happen on ma life tim,sie tukae tu na uzoba wetu maandeleo tutaishia kuyaona kwa wenzetu

    ReplyDelete
  37. wivu umewabana sio?? na kile kibarabara kimoja cha ali hassani mwinyi kutwa kina foleni na vibaka wazoefu ovyo sana hilo linchi tubanana hukuhuku na wazungu kwani nani hapendi kuona vitu vizuri hata kama si kwetu?? utawasikia wadau ooh sifieni vya kwenu sasa tusifie nini wakati hakuna?? tusifie mafisadi kwa kuitafuna nchi?? ndo mana wabongo wakiwa nje wanaringa kuliko wakiwa kwao kwa vile ni ukweli mtakatifu huku kwa watu ni kuzuriiiiiiiii na wala hakunaga mgao wa maji wala umeme full miundo mbinu ya ukweli miaka 50 ya uhuru hiyooo inagonga hadi leo maji safi ni hadithi za abunuasi kwani hawa wazubgu mama zao wana miguu mitatu hadi wawe na maendeleo ya namna hii?? wizi tuuuu nchi hiyo imelaaniwa kila idara watu wanakwiba tuu labda waisraeli waje waiongoze hiyo nchi na haturudi hukuhuku na wazungu huko hakieleweki ufisadi uko juu kuliko maendeleo

    ReplyDelete
  38. MKAPA ALISEMA KAMA MAJANI MTAKULA but RADAR ITANUNULIWA,KAMA WANAWEZA KUNUNUA RADAR YA MABILIONI KWA NINI WANASHINDWA KUJENGA VITU KAMA HIVYO?DIRTY DEALS TO STILL OUR MONEY AND THIS WILL GO ON UNTIL JESUS CRIST RETURNS

    ReplyDelete
  39. Hiyo inaitwa interchange. Hiyo mnayoona hapo kwenye picha inaitwa gotera interchange ni kweli iko ethiopia. Wabongo mnataka interchange ya nini? barabara zenyewe za kuweka interchange ziko wapi? hivyo vijia vyenu utaviwekea interchange? Nyie wabongo mnachojua nikujenga nyumba za magavana, na mawaziri na sio kujenga vitu ya maana...nilishangaa kuona nyumba ya govana ime cost kiasi kile cha pesa upuuzi mtupu.

    ReplyDelete
  40. Mikausho MikaliMarch 24, 2010

    sina hakika la hilo la Addis.lakini kwa Afrika si ajabu kwani Accra Ghana kuna flyovers mbili tatu.Kwa kukujuza zaidi katika masterpaln ya dar iliyotengenezwa 1978 kuna flyovers sehem mbalimbali hata huko kunakoitwa mjini.yaani mtalia mkiona jinsi dar ilivyopangwa vizuri kwenye makaratasi wakati implementation so far ni sifuri

    ReplyDelete
  41. wewe acha hizo, hii picha imetengenezwa. kuna sehemu hata aliyeitengeneza ameshindwa kuondoa roof inagusa barabara. Garden hapo katikati ni ya kutengeneza.
    Wakati mwingine uwe makini ili tuweze kuamini picha zako.

    ReplyDelete
  42. Ni kweli Addis inajengwa sana sasa. Kama ulienda 7 years ago hio ni zamani sana. Wenzetu Africa hii wanapiga hatua sisi miaka mitano ya awamu ya nne nini kimebadilika? Tumwombe Mungu azifungue roho za UBINAFSI; kupenda kila kitu kiwe chako bila kuangalia maendeleo ya nchi na watu wote la sivyo tutapitwa na kila nchi pamoja na raslimali kama madini n.k tulivyo navyo hapa nchini. Katika hali ya kawaida inashindwa kueleweka kabisa kituo kinaangukiwa na mti miaka mi tatu iliyopita hadi sasa kiko vile vile bila kuguswa na mtu yoyote. Mambo mengi tu yanashangaza sana hapa TZ.

    ReplyDelete
  43. Je wana ndege ngapi??? na sisi tunazo ngapi maana tulianza sawa ethiopian airlies na air tanzania

    ReplyDelete
  44. ACHENI UONGO WATU WAZIMA NYIE MIMI NAISHI HAPA ADDIS ABABA NA HAKUNA TASWIRA HIYO. HIZO NI HABARI KTK PICHA TU YAANI PLAN LAKIN BADO HAIJAWA IMPLEMENTED LAKIN PIA TUKIACHA UFISADI TUTAZIDI HAPO TENA KWA MUDA MFUPI SANA

    ReplyDelete
  45. WADAU NI VIZURI TUKAWA WAKWELI. WENGI WANAONGELEA UFISADI, LAKINI UFISADI NA MATOKEO TU YA TATIZO.

    TATIZO LETU KUBWA NI KWAMBA SERA ZETU ZA KULETA MAENDELEO TANGIA UHURU HADI HIVI SASA ZIMESHINDWA.

    HII NCHI INGEKUWA KAMA VILE GARI, NINGESEMA INAHITAJI KUFANYIWA "OVERHAUL SERVICE". WE SERIOUSLY NEED COMPLETE CHANGES.

    MY BIGGEST PROBLEM ALWAYS IS, HOW DO WE START??

    ReplyDelete
  46. how do we start?
    by doing actions and spot blah blah za kisiasa na kuiba pesa kuweka private accounts

    shenzy taip

    ReplyDelete
  47. This is an artistic impression of what is called Gottera Junction in Ethiopia to be constructed by a Chinese (Shanghai)company (Google: Ethiopia infrastructure). I am not sure if the project has already started.

    Mdau.

    ReplyDelete
  48. This is Possible,but Tanzania woga unakuja kwamba wakifanya mambo makubwa misaada itakuwa hakuna Jambo lakipumbavu kabisa.Ujenzi muhimu huishia njiani na barbara za maana huwa za molam wewe unafikiri tutafika??

    ReplyDelete
  49. Mimi niliiweka hiyo taswira hapo ili Watanzani tujifunze kutoka kwa wezetu angalau tulio level moja, kwani Addis ya 2000 si ya sasa imebadilika kutokana na mipango yao mizuri, na resources zao ni chache hawatufikii sisi, lakini wengi wameelewa na inaonyesha wamefika Addis wanaelewa wanachokisema ila kuna ambao hajawaikufika bali wanabisha bila kujua wanacho kisema, hivyo hata nchi kuwa na watu kama hao ni kikwazo cha maendeleo, labda muulizeni Michuzi maana yeye kafika Addis na siyo kubisha kitu usicho kijua, sikujua kama mjadala utakua mrefu hivi, nawashukuru wote hasa walio kuwa positive kwa mjadala.Mungu ibariki Afrika Mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  50. mdau nipo canada never bongo sirudi tena!

    ReplyDelete
  51. TUENDELEE KUIPIGIA KURA CCM TATIZO WATU WANAOPIGIA KURA CCM ASILIMIA 80 HAWAJASOMA NI WALE WALIKUWA WAKIDANGANYWA NA NYERERE SASA MPAKA LEO BADO WANA IMANI ZILE ZILE ZA MCHONGA

    BONGO MPAKA VIZAZI VIPYA VIJE NA VIPATE ELIMU YA KUTOSHA NA VILE VIZAZI VYA ZAMANI VYOTE VIANGAMIE NDIO VIZAZI VIPYA VITAKUJA NA AKILI MPYA NA KUTAKA MABADILIKO

    LAKINI TUKISEMA SASAHIVI TUNATAKA MADADILIKO HALI YA KUWA KINA KINGUNGE MPAKA LEO WAPO KWENYE SERIKALI HICHO KITU MSAHAU

    ccm oyeeeeeeeeeeeeeeeeee
    wasiokuwa na elimu oyeeeeeeee

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...