Ankal pole na miangaiko nakushukuru sana kwa kutuweka wazi kila sehemu,ila mi kwa mtazamo wangu naona mambo ya birthday za watu iwe personal issue kwa sababu watu wote tukiamua kuweka siku za kuzaliwa kwenye blog tutakuwa atuelimishi jamii. nafasi kubwa itachukuliwa na hayo matangazo mwenye siku ya kuzaliwa ya mwanae au yeye au mjomba wake weka kwenye magazeti ya ijumaa na uwazi sani na yale yote ya udaku watakuona wenye interest na birthday,uku watuachie wapenda kuelimika ankal.

nakutakia kazi njema.
mdau
NB. naomba usinitoe jina langu kwani
wapenda birthday party watanimaliza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. You are taking it too far man.
    Hii ni social network hivyo kila kitu ok.
    Hii sio institution ya ma-intellectuals kama unavyodhani.

    Ni ya kila mtu na almost kila kitu

    You might need kwenda jamii forum may be nk.

    Huku ni kwa Jerry Springer mwana sio kwa Oprah

    ReplyDelete
  2. Jina lako litoke lisitoke, we utakuwa mshamba tu. Kwani ulichoandika wewe ndo cha maana kusoma?

    ReplyDelete
  3. Hii Ni Globu Ya Jamii, Mambo Yote Ruksa, kuanza kuwekeana mipaka itauwa dhana ya Globu hii.

    Ila Lugha ya matusi ndio isiyofaa kutundikwa ktk Globu Ya Jamii.

    Mdau
    Mkongwe

    ReplyDelete
  4. eti nafasi itajaa...Huyu nae JEMBE!

    ReplyDelete
  5. NAUNGA MKONO HOJA.

    ReplyDelete
  6. HUYU JAMAA KWA MAONI YANGU NAONA YUPO SAHIHI SANA, HIVI UNATULETEA BIRTHDAY YAKO HUMU ILI IWEJE? NA NAJUA WATU WENGI SANA WATAMPONDA MSHIKAJI JAPO YALE NI MAONI YAKE NA YUPO LOJIKO SANA TUU, NASEMA HIVYO KWASABABU MIMI NI MMOJA WA WATU AMBAO HUWA SIYASOMI KABISA MATANGAZO YA HIVYO NA YANAPOKUWA MENGI NAHISI KAMA YANANIPOTEZEA MDA WA KUSKROO CHINI.

    Ebanaee mtoa maoni naomba uchukue e-mail yangu hii fredsimon65@yahoo.com, ili tuwasiliane. Onyo naomba asiyehusika asichati namimi nina kitabia cha hovyo sana.

    ReplyDelete
  7. Pole ndugu. Kwanza hulipii chochote wewe hapo, pili hujui kuwa wanaotoa matangazo labda wanampa chochote kaka Michuzi halafu haiusu sababu sisi sote tungekuwa na uwezo wa kufanya hivyo tungependa. Hii ni blog ya jamii si ya kitaaluma. Kama ulivyoambiwa hapo juu nenda forum, hapa ni big brother blog hivyo yeye mwenye blog ana haki ya kuchagua anachopenda kuweka kwenye blog yake. Nakushauri utengeneze ya kwako uweke yako na ualike hao unaodhani wana interest ya kuona na kusoma hayo ya kwako.KAKA MICHUZI, UBARIKIWE SISI TULIOUGHAIBUNI TUNAPATA UHONDO KILA DAKIKA. Mi huwa sina hata haja ya kutafuta breaking news kokote ni hapa tu!! Mdau NY.

    ReplyDelete
  8. Ni kweli hii ni social network na ni haki ya kila anayependa kutangaza birthday yake kuitangaza - anapata kile kitu kinaitwa self-satisfaction ya aina fulani. Tatizo ni pale Ankal atakapopokea BDs mia au mia mbili kwa wakati mmoja na akaishindwa aanza na ya nani na kuacha ya nani (sijui nguvukazi aliyonayo kushughulikia mzigo kama huo) - mwishowe atapata lawama kuwa anabagua. Tuendelee kuomba kuwa wakereketwa na wafurukutwa wa ku-post BDs zao wasizidi sana kupita kiwango cha sasa!!!!!!

    ReplyDelete
  9. Candid ScopeMarch 12, 2010

    KAMA ULISHAWAHI FANYA UHARIRI AU USANIFISHAJI WA KURASA ZA MAGAZETI UTAJUA KWAMBA KILA LINALOWEZEKANA KUJAZA KURASA LITAWEKWA VINGINEVYO HATUSAMBAZI GAZETI AMBALO HALIJAA KURASA ZAKE HATA SIKU MOJA. UKIPATA GAZETI KAMA HILO NIONYESHE NITAKUPA ZAWADI YA $$$$ KUWA MSHINDI. SASA BIRTHDAY INA UMUHIMU WAKE KWENYE SOCIAL LIFE MAN!

    ReplyDelete
  10. haya mambo mi nishatoa maoni lakini kwa bahati mbaya watu wanapinga kwa dhana ya neno "jamii".hili neno isije ikafikia mahali mkatuletea picha chafu espec. mkisema eti "jamii". wabongo bana hatutaki kushughulisha vichwa,muda wote birthday tuuuuuuuu!!

    ReplyDelete
  11. Wewe fred na mtoa maoni sio kila kitu kinachowekwa humu mkipende.Kama hamjui siku zenu za kuzaliwa sio kosa la Michuzi waacheni wanaoshukuru siku zao za kuzaliwa wajitanue humu. Mmeshapeana email endelezeni katabia kako ka hovyo huko kwenye email. Tuachieni michuzi wetu.

    ReplyDelete
  12. Fred Simon acha kutisha watu!!Hii blog ya jamii bwana tunasoma kwa furaha.

    ReplyDelete
  13. Globu ya jamii imeonyesha uwezo wa kunyumbulika kutokana na hali. Kuna wakati wanaotafuta wenza walikuwa wanatoa picha zao hapa ikaonekana kwamba wachafuzi wa hali ya hewa wamezidi globu ikaacha kutoa huduma hiyo. Yaelekea mpaka sasa wenye besidei wanaotaka kutoka kwenye globu bado hawajawa utitiri. Wakiwa utitiri globu inaweza kubadili sera bila shida. Let's cross the bridge when we get to it.

    ReplyDelete
  14. kwani uliambiwa kuna habari imekosa nafasi sababu ya picha za birthday?
    huyu atakuwa kazaliwa 29th February.

    ReplyDelete
  15. Namuunga mkono jamaa. Birthdays zinawahusu ndugu na jamaa siyo jamii. Mimi birthdays za mtu nisiyemjua zinanisaidiaje? Afadhali hata kwa wakina mama wawekewe harusi; waone wenzao walivyojipamba.

    ReplyDelete
  16. I second hoja ya huyu mtu. Ni kweli kabisa kama akiweka Michuzi mwenyewe Bday yake huku nitaangalia kwa vile ni blog yake. Lakini wengine wote hasa watu wazima wanaoleta picha za bday yao humu nawaona kama wako desparate sana. kama kwenye FB huna friends wakutosha kuwaonyesha humo picha zako basi engeza muda wakutafuta rafiki. Na kama ni kutangazia umma kuhusu bday yako basi lipia kwenye gazeti huko.

    Mimi birthday za watoto i don't mind that much lakini mimama na mibaba mizima inaleta bday zao huku ili tuone iwe nini?

    Ndio hii ni blog ya jamii lakini kila kitu kinahitaji mipaka.

    ReplyDelete
  17. Labda wabongo mlioko home huko mnaenjoy kuona hizi birthday zikitangazwa. Najua mtanisema na mnamkandia huyo aliyesema hii point lakini the truth must be told. Ni kweli zinaendeza kuwa matangazo yasiyo na umuhimu kwa watu tunaoweka japo dakika 15 kwa siku kuona mambo ya muhimu humu.

    Hii blog inasaida sana kwa habari za haraka kutoka home kwa watu tulio nje ya nchi lakini kwa kiasi fulani watu wa huku ninaowajua wameshaacha kuingia humu na kwenye maparty yetu tena siku hizi husikii jina la michuzi likitanjwa kama zamani au usikie mtu anayekwambia "umeona habari fulani kwa blog ya michuzi" kama hapo nyuma. Watu wanasema siku hizi ni picha za harusi na birthday tu humo.

    Na pia mambo kama hayo ndio yanaongeza speed ya blog hii. Usipoingia siku moja basi lazima uende kwenye kumbukumbu kwa vile ni mavitu kibao yameshapostiwa within a week na kumaliza nafasi. na kama zamani nilikua na feed mwishowe nikaona too much feeds from here zinafanya habari za blog zingine zipotelee.

    Huku siku hizi wanafundisha watu jinsi ya kublog na kutweet ili upate watu wengi...Usipost vitu vingi sana kwa siku au week na usiache kupost kwa muda mrefu sana na kama ni kutweet usitweet mavitu mengi sana kwa siku pia na usipotee bila tweet moja kwa siku. Kumbuka kuna blog nyingi zenye habari tofauti na watu wanaweka muda fulani kusoma kwako na kwa wengine sasa wakiona unazidisha habari kama hizo basi watakusahau.

    Nakusaidia ankal kuongeza quality ya blog yako kwavile mimi ni loyal reader wako wa siku nyingi. Usijeanza kupoteza readers humu

    ReplyDelete
  18. Kwa upande mmoja ni kweli inaboa mambo ya birthday.Lakini najiuliza je na harusi je?
    Naandika comment hii huku nikihofia mashambulizi kutoka kwa mzee wa Pajazzzzzzzzzzzz na Titizzzzzzz, kama akisikia na harusi nazo zinapigwa mizengwe kama birthday anaweza akaandamana hata wale ambao huwa wanatafuta wachumba kupitia picha za harusi zinazowekwa kwny blog nao pia wanaweza kuandamana, ingawaje hawaelewi siku ya harusi kila mtu huwa anaoga na kuonekana bombaaa.

    Mdau wa Kutifuatifua!

    ReplyDelete
  19. kweli bwana michuzi hio mibasidei mingi mno mpaka inachosha kuscrol maana unakua na kamuda kadogo ka kuangalia news unalikuta limama zima na mitoto mikubwa limeweka besidei kama lingine niliona last month, sasa unajiuliza linafikria nini na mchupa wa pombe, sio siri inauzi sana hii web ina wadau karibu milion nane 8 na unajua kabisa bwana michuzi kila mtu kazaliwa hapo hamna alie tagwa so tukisema wote tulete hio mipicha ya besidei sasa hizo zitakua vurugu,kama unaweza stopisha hio itakua bomba sana bora hata uweke picha za sehem yeyote za hio nchi yetu watu tujikumbushe than mipicha ya watu kama wanataka besidei zao beta wajiunge na fesibuku cos hio ndio imemaanaisha kuoneshana sura
    thanx

    ReplyDelete
  20. Huyu alietoa hoja na hawa wanaomsapoti wote wapumbavu, washambu fulani. Mnamuwekea sheria michuzi kwenye globu yake, si mufungue zenu muziwekee sheria. Mijitu mingine mishamba sana!.

    ReplyDelete
  21. NAUNGA MKONO HOJA,HALAFU MTU ANATOA HILO TANGAZO LAKE NA UMRI HAUTAJI,MQAANA YAKE NINI?

    ReplyDelete
  22. Unatuwekea picha zako eti birthday huha albam?.
    Michuzi sikulaumu ila na wewe unaonekana ni mmoja wa wapenda birthday. Tunakuletea michapo yetu ya maana kwa jamii unaibania, mara tunaona kurasa zimejaa picha za birthday, okay anyway.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...