Meneja Masoko wa Kiwanda cha Bonite Bottlers Bw. Girbert Uiso akitoa maelezo jinsi washindi watavyopatikana katika promosheni hiyo iliyozinduliwa kiwandani Bonite mjini Moshi leo.
Mkuu wa wilaya ya Moshi Mh. Musa Samizi akisoma hotuba ya uzinduzi wa promosheni ya Kwea Pipa ya Bonite Bottlers
Mkuu wa wilaya ya Moshi Mh. Musa Samzi akijiandaa kupiga mpira kuashiria uzinduzi wa promosheni ya kwea pipa
Mkuu wa wilaya Musa Samizi akishangiliwa baada ya kufunga bao kuzindua promosheni ya kwea pipa.
Viongozi waandamizi wa kiwanda cha vinywaji baridi cha Bonite cha mjini Moshi katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Moshi Musa Samzi mwenye suti nyeusi aliyekuwa mgeni rasmi.kutoka shoto ni Meneja uajili, Dominic Urasa,Meneja masoko Girbert Uiso,Meneja Fedha Ernest Kaaya ,Mkurugenzi wa kiwanda cha Bonite Zoeb Hasuji na Meneja mkuu mauzo Cristopher Loiruki
Viongozi wa Bonite toka shoto Zoeb Hasuji, Dominic Urasa na Christopher Loiruki wakifuatlia uzinduzi
wadau wa michezo walioudhuria hafla hiyo ya uzinduzi iliyofanyika kiwandani hapo
Picha na Habari
na Dixon Busagaga
wa Globu ya Jamii, Moshi.

KAMPUNI ya Bonite ya mjini Moshi inayojishughulisha na utengenezaji wa vinywaji baridi jamii ya Coca Cola leo imezindua promosheni maalum itakayojulikana kama ''Kwea Pipa na Ushinde''

Promosheni hiyo itawezesha watanzania 200 kushuhudia fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Afrika Kusini hapo mwezi juni mwaka huu .

Washindi watakaopatikana kutokana na bahati nasibu hiyo, watashuhudia mechi ya Brazil na Ureno mchezo utakaochezwa Juni 26 katika mji wa Durban , Afrika Kusini.

Akizindua promosheni hiyo, kwa kufunga penalti katika hafla fupi iliyofanyika kwenye kiwanda hicho mjini Moshi mkuu wa wilaya ya Moshi Musa Samizi alisema hatua hiyo itasaidia kuendeleza soka Tanzania .

Alisema kuanzishwa kwa promosheni hiyo kutaisaidia nchi kw akuwa watakaoenda kwenye fainali hizo watasaidia kupeperusha bendera ya Tanzania hasa katika sekta ya Utalii ambapo itaiweka nchi katika ramani nzuri ya dunia.

Washindi hao watakaokwenda Afrika Kusini, watagharamiwa kila kitu tiketi ya kwenda na kurudi, chakula, malazi pamoja na usafiri wa ndani










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...