JK akiwa katika picha ya pamoja na wanamichezo kutoka Ikulu ya Zanzibar pamoja na viongozi wao wakati walipomtembelea Ikulu ya Dar leo. Kikosi hiki kipo jijini kwa mwaliko wa Ikulu ya Dar katika zoezi la kila mwaka la kutembeleana kimichezo wakati wa Pasaka. Ikulu hizo zitapambana kesho katika viwanja vya chuo kikuu kishiriki cha elimu (DUSE) kilicho karibu na neshno kwa michezo kadhaa ikiwemo mpira wa miguu, netball, kuvuta kamba na mbio za magunia.

Wanamichezo 40 kutoka Ikulu ya Zanzibar, leo, Ijumaa, Aprili 2, 2010, wametembelea Ikulu ya Dar es Salaam ambako wamekutana na kupiga picha ya pamoja na Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wanamichezo hao wako Dar es Salaam kushiriki katika michezo ya Pasaka kati yao ya wanamichezo wa Ikulu ya Dar es Salaam, iliyopangwa kufanyika kesho, Jumamosi, Aprili 3, 2010, kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu Kishiriki cha DUCE, Chang’ombe.

Timu za Ikulu hizo mbili zitachuana katika michezo ya soka, netiboli, kuvuta kamba, na kukimbia ndani ya magunia.

Akiwakaribisha Ikulu ya Dar Es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma za Ikulu, Bwana Frank Mganga ameielezea ziara ya wanamichezo hao kama ziara ya kihistoria.


“Haijahi kutokea tokea tangu mwaka 1964 wakati Tanganyika na Zanzibar zilipoungana ikaandaliwa ziara kama hii,” Bwana Mganga amewaambia wanamichezo hao ambao wamelikwa Dar Es Salaam na wenzao wa Ikulu ya Dar es Salaam.

Amesema kuwa ziara hiyo imelenga kukuza na kuimarisha uhusiano kati ya Ikulu hizo mbili na pia kuimarisha Muungano wa Tanzania.

“Ni kwa kutambua umuhimu wa ziara hiyo, ndiyo maana Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Amani Abeid Karume, ametoa ndege kuweza kuwaleteeni nyinyi hapa Dar es Salaam,” amesema Mganga.

Wanamichezo hao wamewasili Dar Es Salaam katika makundi mawili. Kundi la kwanza lililetwa jana kwa ndege maalum iliyokodishwa na Rais Karume, na kundi la pili limewasili leo asubuhi kwa meli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mmm Mbona hizo sura karibu zote ni ngeni machoni mwetu ?

    Miraji Taufiki

    ReplyDelete
  2. ....michu namimi nataka nikutane na JK afu usinibanie foto yangu kwenye blogu ya jamii... si unajua na mimi nataka kugombania jimbo la naniihiii....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...