Iko Sinza Mori barabarani kabisa karibu na sheli ya GBP Kijiweni
Size ni Sqm 25.
Bei poa, mapatano yapo...
Madalali NO!
Kwa mawasiliano piga namba
0715 120 392
uliza Mac Temba
Kwa nje
Kwa ndani



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Kinapangishwa ni fremu ya duka ama duka lenyewe?

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  2. haina hata dirisha, halafu iwe duka..."Public health" zero

    ReplyDelete
  3. lol no dirisha na hilo joto la dar ndo mteja umeenda kufanya shopping wakati wa kujaribisha nguo unasweatiiiiiiiiii hadi unahisi mapigo ya mtima yanasimama all in all dirisha muhimu

    ReplyDelete
  4. Halafu ni kadogo.Huo ulikuwa uchochoro,mtu akaamua kuuziba kwa kujenga hako kabanda ambako hakina hata dirisha.Yaani ukiweka meza tu inaenea hata nafasi ya kupita kuzifuata hizo fremu inakosekana.Mh! Keroooo.

    ReplyDelete
  5. WADAU HIVI MNATEMBEAGA SHOPS ZA KKOO KWELI???MI NADHANI IT DESIGNED HIVYO COZ LAZIMA IWEKWE AC,NA KWA UKUBWA NI KAMA SHOP NYINGI ZA NGUO HUWA HAZIWI KUBWA KIHIVYO...ACHENI ZENGWE BONGO TAMBARARE...

    ReplyDelete
  6. Alitangaza kodi 400,000/- kwa mwezi! Ina maana lazima uingize sio chini ya alfu 35 - 40,000/- kila siku! Sasa sijui kwa biashara gani?

    Na laki nne kisa eti Sinza! Watu wengine wanajiwekea kodi tu bila kujali usalama wa io frame, choo, ventilation na ukubwa, ndo maana akili ni mali!

    ReplyDelete
  7. Wadau tuache tabia ya kuwa too much pessimistic. Kwani maduka mangapi Kariakoo yana madirisha? watu tumeanzaga na kauchochoro ka hako, leo hii ni nyumba ya pili tunamalizia tokana na kipato ka haka haka kauchochoro.

    ReplyDelete
  8. alikuwa aseme anakodisha kontena la kudumu.

    ReplyDelete
  9. Sio zengwe, na kama umejenga nyumba ya 2 kwa ajili ya haka kauchochoro basi una bahati, na wajingwa ndo waliwao.

    Kwa bei ya laki 400,000/- huo ni ujanja wa mchana, na watanzania lazima wajue, sie watanzania ndo zetu, kila kitu tunachofanya kiholela utasikia tukisema, tumezoea kufanya ivyo.

    Ndo maana ajali haziishi, rushwa imezidi, barabara mbovu, maji hamna, umeme hamna, huduma za afya mbovu. Na sisi tutakalia, jamani ilo zengwe, mbona siku zote hatuna ivi vitu?!

    Yaani wabongo ndo maana hata Uganda inatuacha kwenye mataa, bila kusahau Rwanda, maana uswaili na kufanya kila kitu kiholela tu!

    Sasa wewe hapo huna madirisha, mlango mmoja, choo hujasema kiko wapi, labda kwenda kugonga nyumba ya jirani, kakibanda au ka frame kadogo mno, bado unataka sie tusikosoe, unataka tukae kimya, ukitokea moto au shoti humo itakuaje?

    BURE KABISA!

    ReplyDelete
  10. Viongozi wa miji wako wapi kama wanaachia haya. Hata kama mnasema mlianzia huko that is wrong. Hapo kwanza moto ukiwaka hamna pengine pa kukimbilia. Safety first...mwee huku ukianzisha biashara from scratch utakoma kw vile kuna inspection za kila idara na hao watu wakija wala hawacheki cheki kukupasisha bila sababu...Wanafuata guideline na kama hujapata leseni hupati...

    Ndio maana vitu vinampangilio na mwelekeo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...