(By US Blogger)
Katika pitapita zangu katika maofisi mbalimbali ya Serikali na ofisi binafsi nimeona picha za Baba wa Taifa na Mh. JK zikibandikwa kutani.

Nilipata majibu yasiyolingana kutoka kwa wahusika kama hiyo ni sheria ama mapenzi binafsi kwa wahusika ama uzalendo.

Labda wadau wa libeneke munisaidie.

By US Blogger

USblogger11@gmail.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Nafikiri ni ufisadi. Ile picha inauzwa ghali kweli na ni lazima uwe nayo kwenye duka zamani sijui siku hizi

    ReplyDelete
  2. US Blogger wacha uzushi..hahaha

    ReplyDelete
  3. Mashaka, nitakuandikia na kukufafanulia sheria, kanunu na taratibu zinazoongoza katika matumizi ta picha RASMI ya rais katika ofisi za umma.

    ReplyDelete
  4. NInavyojua hapa kwetu Tanzania katika ofisi za Umma ni Sheria kubandika picha ya rais na ya baba wa taifa, utaratibu huo umeainishwa kwa waraka wa serikali ambao siukumbuki, picha ya rais inatakiwa kuwekwa nyuma ya ukuta ambao amekaa kiongozi katika ofisi hiyo na picha ya baba wa taifa inatakiwa kutazamana na picha ya rais, kwa maana nyingine iwekwe opposite na picha ya rais

    ReplyDelete
  5. si hatuna na pesa za kununua izo picha hatuna...

    kazi kweli izi pesa za mtanzania,yani kodi tunalimwa ya kufa mtu,basi na mengine lazima pia tuyanunue.tule polisi???

    khaaaa

    ReplyDelete
  6. Tuwapende viongozi wetu sio kuwasahau picha napenda kuziona ktk office na zipewe heshma inapendeza. tusipo zipenda nani atazipenda mimi na nyie tukizipenda wote watazipenda.

    ReplyDelete
  7. Mambo ya picha za viongozi ukutani ni kutokana na historia ya mfumo wa zamani wa chama kushika hatamu, lakini siku hizi tungepigia kura hilo halina uzito wo wote.
    Wenzetu walioendelea sijaona picha za marais ukutani hata ofisi za serikali hakuna picha za marais

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...