mpangaji anayehama nyumba huko magomeni jijini dar akihudumia waalikwa kwenye mnuso alioandaa rasmi kwa shughuli hiyo ya kuhama baada ya kunyanyaswa na mama mwenye nyumba wake. habari kamili mtembelee Dina Marios wa Clouds FM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Hapa Ankal labda ungefafanua kidogo, anahama kwenda kwenye nyumba yake au kwenda kupanga tena..??!!. Kama anahama kwenda kupanga, kwani hafanye sherehe..?? Kwanini hasitumie hii nguvu kazi kujenga hata banda lake la chumba kimoja..??.Kuna logic gani kufanyia sherehe kwa mwenzio aliyekwisha tayari kuona mbele..??.
    Anyway, its ok but not right to me,na sijaona kanga nzuri kama vile, "Mtaa wa pili mtanikoma", "Mme chukueni ila mali zangu niachieni" n.k.

    ReplyDelete
  2. Kama haya ndio tunayofikiria katika maisha yetu ya kitanzania tuna safari ndefu ya kufikia maendeleo. Hiyo hela iliyopotea katika hiyo shughuli ingeweza kusaidia maendeleo zaidi katika hiyo familia, kama vile kuchangia maendeleo ya watoto shuleni n.k. Sijui kama wanaweza kupima wamepata faida gani katika hilo na hiyo inatoa fundisho gani kwa watoto walio shuhudia hilo tukio?manake mawazo ya watoto hujengeka kutokana na experience wanayo ipata katika maisha ya kila siku. TUBADILIKE JAMANI, serikali itumie muda kuelimisha wananchi wake. Huo muda uliotumika katika hiyo shughuli ungetumika katika shughuli za kiuchumi ungesaidia kuinua uchumi wetu. Tusitafute mchawi kwa nini hatuendelei, mchawi ni sisi wenyewe.

    ReplyDelete
  3. Kwa style hii, Safari bado ni ndefu sana.
    Ipo haja ya kuibadilisha SERA ya nchi kutoka KILIMO KWANZA na itiliwe mkazo zaidi kwenye ELIMU KWANZA.

    ReplyDelete
  4. Kaka Michuzi katika comenti zote nlishowahi on kwa hii Glob hii imetulia. wapangangaji wa Dar ni noma wananyanyasa muno. Mimi nakubaliana naye huyu mama kwa kufanya huu mnuso. awe anahamia kwa "Polis Post" yake au kwa "mpanganjai mwenye akili tofauti" yote sawa tuuu. Ila nampa Big Up kwa huu mnuso...anaonekana ametulia na ana akili,
    Mwananchi..wa Ughaibuni

    ReplyDelete
  5. kweli uswahilini kuna vituko , Duhhhh !!! hii kali ya mwaka .... si mchezo , yaani nimecheka hadi kicheko kimeisha , duhhh , hana akili huyu dada , au akili zake hazina akili . mdau BAGAMOYO

    ReplyDelete
  6. Duh.. Katika jamii hutawakosa wa aina hii. Kwa manufaa ya baadae kwa hawahawa elimu ya uraia na stadi za maisha ndiyo ukombozi wa wengi. Naomba mdau mmoja aney mjua hyu km Madam Marios - print haya maoni umpe asome na kuhamia nayo huko aendako.

    ReplyDelete
  7. Michuzi kwanza, angekua anatoa comment zote

    ReplyDelete
  8. ni sawa tu kufukuzwa.sasa nenda kajenge yako.TEAM LANDLOAD

    ReplyDelete
  9. Mbona hamsemi maparty ya bethidei ni upuuzi mtupu? Tena unakuta mtu anatumia milioni au zaidi kufanya bethidei kila mwaka hata polisi post hana. Na wengine mwajirusha kila wiki viwanja mnatumia pesa ngapi kwa mwezi? Huyo bidada hapo sherehe yake wala haifikii gharama za mabethidei yenu na maparty yaso kichwa wala miguu. lakini nafsi yake imeburudika, labda aliweka nadhiri akihama hapo atafanya sherehe.

    Sherehe yake haina tofauti na zenu mnazofanya, ingawa ya kwake kapika mchele kilo 20, nyama kilo 10 na matarumbeta mnaipigia kelele ujinga mtupu, je zenu zenye mapombe ya mamilioni na mavyakula ya mamilioni hamuoni kuwa na huo nao ni ujinga?

    Au ndio yale yale kunya anye kuku akinya bata kaharisha? Wacheni kumuona mwenzenu hana akili WaTZ wote mnapenda sherehe na starehe kama nini, utakuta sherehe ya harusi tu yagharimu mpaka milioni 20, wakati maharusi wanaenda kuishi kwenye nyumba ya kupanga, lakini wala huwa hamkomenti kuwa huko ni kukosa akili zaidi ya kusifia kuwa sherehe ilikuwa nzuri, hiyo ya huyo bi mkubwa ya laki 2 ndiyo mnamwambia akajenge? Zinawatosha kweli?

    Michuzi hata ukiibania hii lakini msg sent.

    ReplyDelete
  10. mie naona ni ujinga mtuupuu huu!!!!!nampa big-up mwenye nyumba alomnyanyasa maana ameepuka mengi. alitakiwa ahame aende kwake kwa hasira na sio kujaza watu na kuwapa mpunga... KATOE SADAKA KANISANI/MSIKITINI kwa dhambi hii kubwa ulofanya utakufa masikiini we dada kwa style hii

    ReplyDelete
  11. Mdau wa 12:49 PM,Wape wape vidonge vyao,maana waosha vinywa wamezidi.Kwanza naona afanye sherehe asifanye haiwahusu..........

    ReplyDelete
  12. KWELI SHULE NI MWISHO WAMATATIZO...UKIWA UNA AKILI TIMAMU SIDHANI KAMA UTAWEZA KUFIKIA HAPA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...