Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala ( watatu kulia) Mh. George Lubeleje , akisisitiza jambo kwa watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wakiwemo na Madiwani , ( hawapo pichani) Wilayani humo. Kulia) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Sarah Linuma ( pili kulia) ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Mh. Fatma Mwassa.
Baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba , Sheria na Utawala wakiwa na Mwenyekiti wake George Lubeleje, ( watatu kutoka kulia ) wakisikiliza matatizo ya Mahabusu ( hawapo pichani ) wakati wakipotembelea Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawishi wa Wilaya ya Morogoro. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mh. Said Mwambungu. MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, George Lubeleje, ( watatu kutoka kulia ) akifafanua jambo nje ya jengo la Mahakama ya Mkoa ( wa pili kulia )ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Projestus Kahyoza na wa kwanza kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mh. Said Mwambungu.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala ( wa pili toka kulia) George Lubeleje , akipata ufafanuzi toka kwa Mhandisi wa Ujenzi wa Nyumba za Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Hery Hatibu ( watatu kulia) na kwanza ( kulia) ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Fatma Mwassa.
MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, George Lubeleje, ( wapili kutoka kulia ) na baadhi ya wabunge na watendaji akitoka kwenye jengo la Mahakama ya Hakumu Mkazi Mkoa ( wa kwanza kulia )ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Projestus Kahyoza. P:icha zote na John Nditi wa Globu ya Jamii Morogoro.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. my dad mwenye shati la mauwa,thank u michuzi,sijamuona since 2006

    ReplyDelete
  2. Sijui kama nitakuwa nakosea ila ni vizuri mazuri yasemwe, napenda utendaji kazi wa huyo mheshimiwa Incharge wa mahakama ya mkoa wa morogoro, anajali sana na kutatua matatizo ya watu. Nakumbuka pia miaka ya 2007 kulikuwa na hakimu pale monduli kwenye mahakama ya wilaya ila sijui kwa sasa yuko wapi, nafikiri kuna haja ya kujali mchango wa Mahakimu wanaofanya vizuri.

    ReplyDelete
  3. KAMA ILO JENGO NDIYO MAHAKAMA YA MKOA WA MOROGORO BASI LINATIA SANA AIBU. MIAKA KARIBU HAMISINI YA UHURU BADO MAHAKAMA YA MKOA INAKAA KWENYE JENGO LA HALI YA CHINI KAMA HIYO.

    MUNGU IBARIKI TANZANIA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...