Club maarufu na yakimataifa hapa nchini,Club Bilicanas imenusurika kuungua moto usiku huu mara baada ya moja ya TV zilizowekwa ndani ya clab hiyo kuleta shoti na mpaka kulipuka kabisa,kitu ambacho kilimpelekea kila mmoja aliekuwepo ndani humo kudhania ni bomu na kuanza kukimbia kutoka nje na kwa kuulinda uhai wake.lakini kwa bahati nziri wafanyakazi wa jengo hilo walifanikiwa kuwahi kuudhibiti moto huo.Bendi ya Twanga Pepeta ndio iliyokuwa ikitumuiza hapa siku ya leo katika ambapo kila siku za jumatano bendi hiyo hupiga katika kiota hicho.wapenzi wa bendi ya Twanga Pepeta wakiwa nje ya club kusikilizia kinachoendelea
Askari polisi walikuwepo kuhakikisha usalama unapatikana wa kutosha kwa kila aliekuwepo katika eneo hilo.
gari la faya likiwa limesimama nje ya jengo la club bilicanas usiku huu kuangalia kama kuna lolote ili kazi yake ianze mara moja.lakini kwa bahati nzuri moto huo uliweza kudhibitiwa na wafanyakazi wa club hiyo.
kila mtu alikuwa akihuzunika.
watu kibao walikuwepo nje ya club bilicanas kusikilizia kama mambo yatakuwa poa ili warudi tena ndani kuendelea kuburudika na wana wa kutwanga na kupepeta usiku huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. Duh!! Halafu kesho kazini?
    Nakumbuka kulikuwa na ule msemo kuwa Jumatatu na Jumanne sehemu za kazi ni kuzungumzia wikiendi iliyopita, JUMATANO ndio kazi, Alhamis na Ijumaa ni kujiandaa na wikiendi. Sasa kama na Jumatano (ambayo ndio siku pekee ambayo yasemekana tulikuwa ukifanya kazi imechukuliwa na Bills) sijui tunaelekea wapi.

    ReplyDelete
  2. Kwanza pole kwa wale walopata mshituko kutokana na tukio hili na tunamshukuru Mungu kuwanusuru ndugu zetu na pengine janga ambalo tungekuwa tunazungumza vingine kwa sasa.
    Nashawishika kuuliza Je hapa Nyumbani TZ kuna utaratibu wa kukagua vifaa vinavyotumia umeme baada ya muda gani ili kuonyesha vinatakiwa kufanyiwa ukarabati(service) ndani/baada ya muda gani? au tunatumia tu vyombo hivi mpk vikilipuka kama hivi ndo tunajua vimezeeka?Hii ikiwa kwenye majumba yetu na majumba ya starehe, Je kuna mamlaka yeyote inayohusika na jambo hili?
    Na Je kuna busara gani katika swala la askari Polisi kuwa na nguo za kiraia huku wakiwa na silaha zinazo onekana kama ninavyo ona hapo pichani? je hii haituweki katika hatari yeyote ya kiusalama?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 13, 2010

    Askari polisi kutovaa uniform na kukamata SMG haipendezi hata kidogo.

    Kwa nini wasivae uniform iwe kama wamejitambulisha?Likishika jambazi hapo na silaha za moto tutajuaje nani jambazi na nani askari?

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 13, 2010

    Watu kumbe mnaogopa kufa, lakin hamugopi kumkera mungu, Huo ulikuwa ukumbusho kwenu msijisahau kila siku Club.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 13, 2010

    Wachina watatumaliza nchi zima wapate pa kuhamia!Wanetu maziwa yenye kimikali, sie wenyewe TV zenye kulipuka na vingine hatujui wanatuwekea kwenye nini!
    Sijui hata tujipatie ushauri gani? Used electronics yale yale, kuacha kuangalia Luninga hatuwezi!

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 13, 2010

    yaani wabongo kaazi kweli kweli , yaani bado wanataka kurudi ndani na kuendelea ? yaani siamini, wanajali sana sterehe kuliko maisha yao , wewe ushaona kuna moto umefanikiwa kuzimwa kwanini usiende kulala kwako ? bado unataka kurudi , je lingekuwa bomu dogo limelipuka sasa bomu kubwa linafatia ? hehehehe mungu atawasidia na akili zenu..

    mdau
    USA

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 13, 2010

    sasa hao askari na vipensi jamani tutawatofautisha vipi na majambazi? kweli ukisimamishwa na hao si utakimbia tu wakupige wasingizie wewe ni jambazi ulikuwa unawakimbia!!!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 13, 2010

    polisi hawataki kuchafua uniform zao, tabu kuzifua, yaani kaazi kweli kweli.. mimi nitafurahi na polisi IKIBINAFSISHWA....

    BONGO TAMBARALE....

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 13, 2010

    Naifu hapo juu umenichekesha kweli , eti kama kuna utaratibu bongo wa kuangalia vifaa vya umeme muda hadi muda ,, hehehehe AFYA ZAO HAWAANGALII MUDA KWA MUDA WATAANGALIA VITU VYA UMEME..!!!

    kaazi kweli kweli...

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 13, 2010

    kila mtu alikuwa akihuDHunika, tanzania darasa bovu kiswahili tunafeli hata kiingilishi pia!

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 13, 2010

    Wadau wote mnaolishikia bango suala la Uniform kwa polisi mpo sahihi 100%. Hapo kuna hatari kuu mbili, moja kwa raia na ingine kwa polisi wenyewe.

    1. Tukianzia kwa wananchi wenyewe ni kweli kabisa inakuwa vigumu kutambua kuwa anayekusimamisha ni polisi halali au jambazi anataka kukupora na hivyo kukuweka katika mtihani mgumu sana, mfani ni yule Tax driver aliyeuwawa kule kimara suka baada ya kusimamishwa na polisi wasiokuwa na uniform akadhani ni majambazi na hivyo kukanyaga mafuta huku polisi nao wakidhani jambazi na kummiminia risasi na kumuua. Kitambulisho pekee cha polisi kwa raia ni uniform zao, na si vinginevyo

    2. upande wa polisi wao pia wanakuwa katika risk kubwa hasa pale inapotokea kuwa wanapambana na majambazi na kuomba msaada either wa helicopter au polisi wengine ambao hawafahamiani nao na hivyo kufanya tukio kuwa gumu kwa wasaidizi kwani hawajui jambazi na polisi ni yupi. Pia hapo wanaonekana hawana hata bullet proof kitu ambacho kinaweka maisha yao katika risk kubwa sana


    Sikatai askari kanzu ni muhimu hasa pale wanapofuatilia jambo na wao wasigundulike na mfuatiliwa lakini hawa wawe na silaha zilizofichwa kama bastola na wakati huo huo kikosi cha polisi wenye uniform na silaha kinakuwa alerted pindi vurugu ikianza.

    Style hii ya kutokuwa na uniform inawafanya hawa polisi wakati mwingine kufanya ujambazi wao wenyewe kwa kuwa hakuna atakayejua kuwa ujamabazi umefanywa na polisi pia namba zao ambazo huvaliwa kwenye uniform zinakuwa haizjulikani.

    Mimi ningekuwa waziri wa polisi au mkuu wa polisi basi taratibu kuu ingekuwa bila uniform haupo kazini, uniform ni lazima, mbona askari jeshi wanapigana vita huku wamevaa uniform?

    ReplyDelete
  12. MshirikinaMay 13, 2010

    Jamani Jamani!

    Hii mioto kwenye maukumbi ya Disko vipi jamani? MAISHA club nayo si iliungua siku za hivi karibuni tu?

    Sio bure. Kuna mikono ya watu hapo.
    Nawashauri waende NGENDE wakaangalie hilo

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 13, 2010

    nauliza tu jee kisheria mbali na body gurds askari polisi au jeshi anaruhusiwa kuwa na smg au bastola uraiani akiwa hana magwanda yake?

    Je utamtambuaje kama huyo ni askari/jeshi? si hapa tunawapa idea majambazi?

    ReplyDelete
  14. WABONGO BWANA....SASA WEWE UNAWEZA KUMILIKI CLUB BILICANAS HALAFU TENA UNANUNUA TV ZA CHINA....SASA CLUB INGEUNGUA UNGEPATA FAIDA GANI...SHULE MUHIMU SANA JAMANI....BONGO ZERO

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 13, 2010

    wewe mtoa maoni KILO hapo juu , akili zako ziko KILO moja nini ? una hakika gani kwamba tv zao zilikuwa feki ? uliwanunulia ? kwani tv original ndo hailipuki ?
    huna cha kuongea nyamaza
    nimekusamehe nilivyoona jina lako..

    mdau
    kariakoo

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 14, 2010

    Najiulzia hivi hizo emergency exits zinakau openi au ndio yale yae zina fungwa na siku ya tukio watu wankua trapped?

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 14, 2010

    Hivi nyinyi mnaojidai kukandia kwanini hamuulizi kabla zaii ya kushambulia na kukandia?Eti polisi na nguo za kiraia.Hao kazi ya ni kuzunguka huku na huko kuangalia ulinzi wa raia,wanakuwa na Land rover 110,huwa hawavai uniforms,wao wanavaa kiraia.Sasa cha ajabu ni nini km walikuwa kwenye patrol na wakakuta tukio hapo?mbona wakienda kwenye maeneo mengine kwenye vurugu,au wanapoenda kupambana na uhalifu hamuulizi uniform?au kwakuwa ni Bills?au ndo hizo picha za mitaa mingine hamzipati.Acheni kujidai nyinyi..

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 14, 2010

    poleni jamani ; ila sipati picha hilo sokombinde lake uwiiiiiiiiiii

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 14, 2010

    Wadau hao ni Askari wa Upelelezi na wako zamu! kwa kawaida wanaitwa PATROL! wakati wote wako na silaha, hawahitaji kurudi kituoni kuchukua silaha. Wepesi kureact kwenye tukio! Kwa taarifa tu, msipende kila kitu kucomment negatively!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...