Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua harambee ya kuchangia fedha uchaguzi mkuu CCM mkoa wa Kilimanjaro iliyofanyika katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam jana jioni.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi sanamu ya Twiga Waziri Kiongozi wa Serkali ya Mapinduzi ya Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha wakati wa hafla ya uchangiaji fedha kwaajili ya Uchaguzi Mkuu CCM mkoa wa Kilimanjaro iliyofanyika jana jioni katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.Sanamu hiyo iliyonunuliwa katika mnada huo na wafanyabishara vijana katika soko la Kariakoo iliuzwa kwa shilingi laki saba na vijana hao kuamua kumpatia zawadi Waziri kiongozi.Katika Harambee hiyo jumla ya shilingi Milioni mia mbili( 200m/-) zilipatikana ikiwa ni fesha taslimu na ahadi.Waziri Kiongozi Shamsi Vuai nahodha alichangia fedha taslimu shilingi milioni moja.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku cheti maalumu Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo kwa kutambua mchango wake katika kufanikisha kwa ufanisi mkubwa kufanyika kwa mkutano wa World Economic Forum uliofanyika jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.Katika hafla hiyo wadau wengine wakiwamo mashirika mbalimbali,kampuni na watu binafsi nao walitunukiwa vyeti kwa kufanikisha mkutano huo wa kimataifa.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Mama Vicky Nsilo Swai akimzawadia Rais Kikwete Ramani ya Afrika yenye kuwaonyesha wanyama watano wakubwa(the big five) Simba,Tembo,Faru, Nyati na Chui muda mfupi baada ya kumalizika hafla ya kuchangia fedha kwaajili ya Uchaguzi Mkuu CCM mkoa wa Kilimanjaro jana jioni katika hoteli ya Golden Tulip jijii Dar es salaam.Katika hafla hiyo Zaidi ya shilingi milioni mia mbili zilipatikana ikiwemi ahadi na fedha taslimu

(picha na Freddy Maro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2010

    Hili neno Harambee lilikuwa halitumiki wakati wa mwalimu sasa cha ajabu tunawaiga wakenya kwani wao tokea wakati wa Jomo Kenyatta walikuwa wanalitumia( HARAMBEE-FUATA NYAYO) kwa hiyo sisi pia tunafuata nyayo za wakenya au tusemeje kwa hilo?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2010

    neno Harambee asili yake si Kenya bali India japokuwa waliamua kuliweka kwenye national emblem yao! jaribu kufanya uchunguzi na uache kukurupuka asili ya neno hilo inatokea India na wakina Gandhi so kama wao wameiga kwanini na wengine wasiige ikiwa ni neno lililoingizwa katika Kiswahili

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2010

    Milioni 200 kwa watu kama hao nadhani ni kidogo sana. Ilitakiwa ipatikane walao kijisenti.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 15, 2010

    Yaani mheshimiwa mwenyekiti wa chama changu cha ccm kwa hili umechemka. Katika nyakati zote utakazo kuwa madarakani pindi mungu akikujaalia utajutia uwepo wako katika tukio hili. Pamoja na nia yako njema ya kukichangia chama bado unashindwa kubaini kwamba IBILISI WA MTU NI MTU. Fanya ufanya cho na uende uendako tatizo la kilimanjaro kichama ni MWENYEKITI wa mkoa na wala sii majungu. Cloud huwa wanasema FIKIRIA MJOMBA UTABHAINI!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 16, 2010

    du naungana na mdau hapo juu kwel milioni 200 ni kidogo sana kwa rais kuongoza harambee,milioni miambili kwa mbunge ndio sawasawa.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 16, 2010

    wangemwalika Hasheem Thabeet angeweza kubust kidogo

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 16, 2010

    Hongera sana kwa kiasi kilichopatikana si haba. Maana tunaambiwa tushukuru kwa kidogo. Pia wadau mtambue pia hiyo ni harambee ya mkoa mzima. wabunge wa majimbo tofauti watachangiwa binafsi na washabiki wao hivyo watu wamebana kidogo ili kila mmoja ajue nani anasimama kwenye jimbo lake.

    Ni kweli huyo MWENYEKITI WA MKOA NDIO MCHAWI WA JIMBO LA MOSHI MJINI HALMASHAURI TAZAMENI

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 16, 2010

    Rais wangu Kikwete,

    hiyo pesa ni ndogo sana kumng'oa Ndesamburo. Piga debe zaidi iongezwe. Lakini hii harambaee ilifanywa kichoyo, kwani watu wengi sana walipenda kuchangia na hawakualikwa. Halafu shughuli njema kama hii sio vyema kuipeleka Golden Tulip. Ukumbi wa kawaida kabisa ambao haukuhitaji kiingilio kiikubwa cha 50,000/- ulitosha. Walio na pesa siku hizi ni vijama wadogo na sio mabishoo wa mahoteli makubwa. This blander should not be repeated again.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 17, 2010

    YULE PROFESA ALIFUKUZWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KWA KUJIHUSISHA NA SIASA MBONA HUYU KATIBU MKUU YUPO KUICHANGIA CCM HIYO SIYO SIASA?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...