Mshindi wa miss kanda ya kaskazini Gloria mwanga kutoka mkoani Arusha wa pili ni mshindi wa pili wa shindano la miss kanda ya kaskazini Prisca mkonyi kutoka mkoa wa Kilimanjaro huku mshindi wa tatu ni mshiriki kutoka mkoani Tanga Zulekha Mrisho .Washiriki waliobahatika kuingia tano bora wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutajwa wakwanza ni Zulekha mrisho wa pili ni Prisca Mkonyi wa tatu Gloria Mwanga wanne Anna kimambo na watano Zahar Suleman.Picha zote na woinde shizza

Na Woinde Shizza,Arusha

Hatimaye Shindano la kumsaka Miss Tanzania kanda ya kaskazinilimemalizika na mkoa wa Arusha bado umenagangania taji la mrembo huyo baada ya mrembo Gloria Mwanga kutoka mkoani hapa kutwaa taji hilo.

Shindano hilo ambalo liliwakutanisha washiriki takribani 12 kutoka katika mikoa minne iliyoko katika kanda ya kaskazini ambayo ni Arusha ,Manyara ,Kilimanjaro na Tanga lilifana pale ambapo wasanii msanii ambaye alibahatika kunyakua ushindi wa BSS wa mwaka jana Peter msechu aliweza kuwafurahisha watu na kibao chake cha Hasira za nini na kufanya usiku huo kun’gara.

Katika shindano hilo ambalo lilikuwa na upinzani mkubwa wa kila mrembo kuwa na sifa ya kuwa miss na kila mshiriki kuw ana mori wakutetea mkoa wake na kutwaa taji ambalo lilikuwa likishikiliwa na mrembo ambaye aliwakilishamkoa wa Arusha Susan Emmanuel ambaye amekaa nalo taji hilo kwa takribani mwaka mmoja sasa.

Mshiriki kutoka katika mkoa wa Arusha Gloria Mwanga alibahatika kutwa taji hilo na kuondoka na kitita cha shilingi milioni moja na huku akiwa amebahatikakusoma kozi ya utalii ya miaka miwili ambayo inagarimu kiasi cha shilingi milioni mbili pamoja nakuzawadiwa vocha kwa ajili ya kufanya shoping inayogarimu kiasi cha shilingi laki moja huku akipatiwa kozi ya kifaransa itakayo garimu semista mbili .

Kwa upande wa mshindi namba mbili ambayea ametokea mkoa wa Kilimanjaro Prisca mkoanyi yeye amebahatika kuondoka na fedha taslimu shilingi laki sita huku akibahatika kusoma kozi ya kifaransa ya mwaka mmoja na kupewa vocha ya kufanya shooping na mshindi wa tatu ambaye ni Zulekha Mrisho yeye amebahatika kusoma kozi ya kifaransa kwasemist ambili pamoja na kuondoka na kitita cha shilingi laki nne .

Gazeti hili lilizungumza na Hashimu lundenga naye alisema kuwa anawapongeza waandaaji wa shindano hilo kwa kutoa kipaumbele kuwa pa elimu washiriki ambao wameshiriki shindano hilo na pia sio waho tu bali amewapongeza hata wale ambao waliandaa mashindano ya ngazi ya mikoa.

Naye mratibu wa shindano hili ambaye ni Mkurugenzi wa Miss Northern Zone Erasto Jones toka kampuni ya Crown International Entertainment alisema kuwa wamemaa kuwapa warembo hawa zawadi za elimu kwani wandio nyia ya pekee ya kuwakomboa kimaisha na hawataisahau kabisa.

“unajua tumeona tuwape elimu kwani mfano ukampa gari atatumia litaisha na matokeo yake anaeza ata akapata magonjwa kupitia gari hilo hivyo naona tuwape elimu mana ndio njia pekee ya kuwakombo kimaisha”alisema Jones.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 19, 2010

    LAKINI HAYO MANYWERE!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 19, 2010

    Yote tisa huyo mwenye sketi ya rangi ya chungwa lilioiva ni nani vile?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 20, 2010

    mimi nazani uku kwenye u miss wangekuwa wanawafundisha jinsi ya kuwa mwanamke bora na jinsi ya kumburudisha mumeo!!kwani naona kama kungekuwa na university hiyonayotoa kozi ya umiss nazani 99.9% ya wanawange wa kitanzania wangekuwa graduates !! kwanzi yote kumi kila siku nasikia miss miss utazani kwenye jukwa la kimataifa tuna perform vyema !! kila kukicha miss temeke mara miss kimara mara miss kinondoni AU hii ni biashara ya mtu ??

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 20, 2010

    ulikuwa hujui kuwa ni biznesi!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 20, 2010

    Bongo ikishagundulika biashara fulani kila mtaa wa miji yote utaikuta, kwani ubunifu wa biashara tofauti ni haba. Hii biashara ya ulimbwende kila kukicha haiishi? na kila siku mara miss ilala, mara miss magogoni, mara miss tanangozi, lakini je hawa tunaowapeleka Umiss wananufaikaje na biashara hiyo kiuchumi, kimwenendo na future yao?
    Biashara hii jamii ina mtazamo gani? Je ni kwa kiasi gani iendelezwe au maana utitiri huu wa umiss sijajua ni kupata ubora kweli au mradi tu ubunifu wa biashara. Wanaotumiwa (wasichana) wananufaikaje kimaisha, kiuchumi na kimwenendo?
    Alamsiki wanablog

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...