Mwanamuziki nyota wa Jamaica Sean Paul akitummbuiza katika uzinduzi wa Big Brother Africa All Stars usiku huu hapa Johannesburg

washiriki wa Big Brother All Stars wakiingizwa mjengoni kuanza safari yao ya kusaka dola 200,000 atazopewa mshindi baada ya kukaa humo kwa muda wa siku 91. hii ilikuwa usihu huu hapa Sandton, Johannesburg, Afrika ya Kusini ambako Globu ya Jamii ilikuwepo kushuhudia na kuripoti laivu kuzinduliwa kwa shindano hilo linalorushwa masaa 24 na DSTV
Baada ya kuingia mjengoni ambapo haruhusiwi mtu mwingine kuingia, waliohudhuria uzinduzi walioneshwa kinachojiri kupitia bonge la luninga. hapo anaonekana Mwisho Mwampamba akiingia wa kwanza mjengoni. Pia alikuwa wa kwanza kutambulishwa baada ya waandaaji M-Net na DSTV kuficha majina ya washiriki hadi dakika ya mwisho. Mara tu baada ya kuingia mjengoni Mwisho
alionekana akiongea na Tatiana wa Angola kwa muda kiasi... Kisha wakakumbatiana kwa furaha... Limo iliyokuwa ikiwaleta washiriki mmoja baada ya mwingine.


Listi kamili ya washiriki 14 toka nchi 14 walioingia mjengoni usiku huu ni: Mwisho (Tanzania), Jen (Msumbiji) Code (Malawi), Hannington (Uganda), Kaone (Botswana), Lerato (South Africa), Meryl (Namibia), Munya (Zimbabwe), Sami (Ghana), Sheila (Kenya), Uti (Nigeria) na Yacob (Ethiopia), Paloma (Zambia) na Tatiana (Angola)
mwisho akiwa na jen wa Msumbiji na Paloma wa Zambia










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 26 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 19, 2010

    Michu nilikuwa naomba urekebishe ulivyoandika kuwa mshindi wa Big brother atapata dollar millioni 200,000. Michu hizo dollar ni za kiZimbabwe ?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 19, 2010

    dolar milioni 200,000?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 19, 2010

    Mwisho aache u-chapombe wake bali aendelee kuwa Diplomatic and considerate atashinda tu mzee. Kumbe kuna kurudia!

    Observer

    ReplyDelete
  4. kaka misoup angalia hizo shavu za kufa mtu mama naniii yuko wapi jamani kila cku alone nomaaaaaaa sana naona ulienjoy kwa sana kaka all the best broo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 19, 2010

    Tunakutakia kila la kheri mwisho. tafadhali punguza pombe.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 19, 2010

    UNARUHUSIWA KUSHIRIKI MARA MBILI?

    ReplyDelete
  7. Michuzi hicho kikofia kama ndumilakuwili jamani!!!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 19, 2010

    That's very cool. Love u 4 posting dat clip. U make us feel so close 2 home. U just don't know how u're blog do "us" excerpt 4 Chichiem news. Other than that u're cool. I bet ur kids' friends say ur the coolest dad in town

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 19, 2010

    Kuhusu kurudia, ni kwamba hii season BBA5 ALL stars ni special kwa washiriki wote walioshawahi kushiriki lakn hawakubahatika kushinda...BBA wameamua kuwapa nafasi nyingine, hawa ni wale walioonekana walikuwa na burudani wakati ule mwanzo.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 19, 2010

    mi naamini mwisho kashajifunza hata kama atakunywa hizo pombe hatozidisha jamani mana june july kaiona atii, hiyo ni kama golden chance akicheza tena basi yeye hapa dunianai hatofanikiwa tena.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 19, 2010

    Mwisho, Chukua hizo dola laki mbili uje ununue shamba huku Mbeya kwa sababu wapambe wa mas-star huko Dar watakumaliza na Morogoro ni karibu mno na Dar. J. Kyoma.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 19, 2010

    Ankal! naona unazua nyago,safishaaaa nyota

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 19, 2010

    Mzeiya wa libeneke, sina uhakika kama unaimanya vema iyo mistari,.coz nakuona live unavyomung'unya maneno...kudadek, safi lkn unajua kujimegea...jipanguseeeee

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 19, 2010

    mbona richi hayupo?

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 19, 2010

    Kweli kila mtu na bahati yake, hii sasa ni chance ya Mwisho kutoka kimaisha.Asipokuwa serious this time ndo atakuwa kapotea kikweli sasa.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 19, 2010

    mwisho hiyo second chance itmie vizuri ukirudi uraiani,nadhani umejifunza sana tu

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 19, 2010

    Picha ya Chini,mzee wa Pajas uko wapi?Hujaona?

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 19, 2010

    mweeee tena?kumbe wanarudia
    ila hizi pesa tusizozionea matokeo yake kwa hawa washiriki?hadi huruma

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 19, 2010

    siyo SANDTON hapo ni BALFOUR PARK kuna umbali mkubwa kutoka hapo hadi SANDTON

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 19, 2010

    WANASHIRIKI MARA YA PILI KWA SABABU WAMEITWA WASHIRIKI WA ZAMANIN JAMANI. NDIO MAANA INATWA BIG BROTHER ALL STARS MAANAKE WALE WALIOSHIRIKI ZAMANI! WATANZANIA WAGUMU KUELEWESHA DUUU.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 19, 2010

    Hivi TZ siku zote inawakilishwa na mashombeshombe (chotara) tu. Si maanishi ubaguzi ila inawezekana watu weusi tii kuna kitu wanamiss.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 20, 2010

    Any wa Mon Jul 19, 07:12:00 PM ni kuwa tatizo letu tunakomalia kimatumbi sana hivyo kujikuta tunamungunya kiinglish. May be watu wa diaspora wakiacha boksi wakaanza kurudi basi tutapata mshiriki mwenye rangi ya kimatumbi.







    Joke!!




    Nkyabo - Bongo

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 20, 2010

    Wapi Gaitano wa Uganda kama ni all stars?

    ReplyDelete
  24. AnonymousJuly 20, 2010

    Hey Mwisho.....KULA MTUNGI MWANA YAAANI SANA TENA KAMA VIPI ANZA STYLE YA KUZIMA KABISA AU C O? BIG UP !!!

    BY LAGER FAMILY

    ReplyDelete
  25. AnonymousJuly 20, 2010

    Mwisho ndani ya BBA tena hahahahaaaa, who lets the .....out? who?who?who?who????

    ReplyDelete
  26. AnonymousJuly 20, 2010

    Ankal nakuona unavyomumunya maneno hapo, ila big up mshkji, kuhudhuria hapo ni bonge la shavu.
    Mwisho I wish you all da best BUT tuwakilishe wa tz kwa maadili yetu manake naona kuingia na kuingia tu ushabambwa half naked, duuh!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...