Msanii Dokii akiwatumbuiza wajumbe wa MkutanoMkuu wa CCM katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma usiku wa kuamkia leo Mwenyekiti wa CCM akihutubia mkutano mkuu wa chama hicho Kizota, Dodoma Mwenyekiti CUF Profesa Ibrahim Lipumba akimpongeza Mwenyekiti wa CCM taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa CCM uliofanyika katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma jana. Katibu Mkuu wa CCm Yusuf Makamba aakimkabidhi Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete kadi maalumu ya viongozi waliwahi kushika nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho.makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa ufunguzi wa mkutano Mkuu wa CCm huko Kizota mjini Dodoma leo asubuhi
Mwenyekiti wa CCM Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mama Salma Kikwete wakiongea na Katibu Mkuu wa CCM Mh. Yusufu Makamba. Picha zote na mdau Freddy Maro wa Ikulu





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 11, 2010

    mbona chadema wamealikwa hawajaja,ndo maana nasema chama cha kweli cha upinzani bongo ni cuf,chadema siasa za chuki,wao wanadhani upinzani ni kuchukiana tu,nakumbuka kwenye mkutano wa cuf hawajaenda na walialikwa,wakati mkutano wao lipumba aliibuka kule,ndo maana watu wenye bif kama mr 2 wanakimbilia huko,michuzi ngoja uniudhi,nakuwa chadema alafu nafungua blog

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 11, 2010

    Wardrobe advisor wa Mama Kikwete kweli anafanya kazi yake ipasavyo. Panapostahili sifa inabidi zitolewe / zipewe (sifa).

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 11, 2010

    Mheshimiwa Rais Kikwete tuna imani kubwa sana na wewe. Ila chonde chonde baba uweke mawaziri watakaosidia wananchi, sio uangalie urafiki. hatukatai kujali marafiki lkn marafiki sio mafisadi.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 11, 2010

    kama kuna mke wa rais Tanzania anaejua kuvaa basi na watu wakamkubali lazima atakuwa SALMA.
    big up sn mama

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 11, 2010

    sio advisor tu,mama mwenyewe pia ni wakisasa (mjanja)

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 11, 2010

    Du kweli dua retu limepokelewa na mwenyezi mungu. mrema sasa ajuwi muelekeo wake alitufanyia kitu kibaya sana sisi watu kariakoo enzi ya utawala wake

    ReplyDelete
  7. Acheni ushabiki wa kijinga. CHADEMA kama chama huru na makini cha upinzani hakin ahaja ya kujipendekeza kwa CCM kama ilivyo kwa TLP au CUF. Kwani nani asiyejua kwamba CUF sasa ni mamluki wa CCM? TLP ndio kabisa imewekwa mfukoni mwa CCM na Mrema ndiye mamluki nambari wani. CHADEMA chama kubwa, CHADEMA chama mbadala!!!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 11, 2010

    Hakuna chama kiboko wala mbadala, Chadema mmejawa Chuki na wengi wenu ni wale2 tunawajua mnajiona nyie njii hii yenu peke yenu, waapi mmeshaula wa chuya andikeni maumivu mwaka huu na magwanda yenu ya MGAMBO! Pesa kibao mnapata kutoka kwa maswahiba wenu wa CONSERVATIVE/TORY, lakini hamjachimba hata kisima cha maji japo ya chumvi watu wakatumia! huo mbadala wetu tutaounaje? Au mnataka kuja kuliza watu kama Tory? Mmebanwa mbavu hata wizi hamuwezi tena mnabaki kulalama!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 11, 2010

    kwani chadema ni chama cha siasa,si ngos ile jamani.ndo maana zito na marehemu chacha walivyojaribu kumgusa share holder wa chama ikawa balaa.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 11, 2010

    we mjinga achana na CUF kabisa,nabi amekwambia wanajipendekeza kwa ccm,cuf wanajua siasa ndo maana unaona wameweza kuilazimisha serikali serikali ya mseto zanzibar.na kama hujui historia ya cuf nyamaza,maana hata hiyo sera ya ufisadi ni cuf ndo waloianzia kwenye ndege ya rais na ubalozi wa italy,ambao saa hivi bob makani mwenyekiti mstaafu wa chadema ndo anamtetea yule fisadi mahakamani.cuf kila siku sera mpya sio nyie ufisadi tu ndo point yenu,wananchi wanataka kujua paln za chama.kama chama kweli si mngepitisha mgombea urais,mnasubiri mpaka wafuzwe ccm ndo mchague.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 12, 2010

    Jamani amkeni, mbona tunababaishwa na mavazi ya kijani, shoo nyingi kwa viongozi lakini hamna matendo. CCM wakati umepita au kiongozi mwingine atokee, maana Kikwete hana viongozi.Marafiki wa kumlinda, na ufisadi kwa nguvu.

    ReplyDelete
  12. When two opposition parties agrees to each other and pat themselves on the back, who is srewed?
    US, the citizens!

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 12, 2010

    CHADEMA walikuwepo, alikuwepo makamu mwemyekiti

    ReplyDelete
  14. bwana michuzi, asante kwa kazi yako nzuri na kubwa katika fani hii ya habari, tunakilasababu ya kukupongeza kwani wengi wetu tumekua fans wako katka kuhakikisha tunapata habari za nyumbani,mbali na kwamba wakati mwingine inakuwa ngumu sana kwako kuleta kila habari ya muhimu lkn tunatambua wajibu na nafasi yako katika taifa kendeleza na kukuza nyanja hii ya habari.ninaombi moja kubwa ktk hbari kama hii ikiwa unaweza kutupostia video ya hawa waheshimiwa na sisi tukawasikia kwa masikio yetu na na kujua ni barabara lipi wanalokusudia kutupitisha utakuwa umetusaidia sana mizani zetu katika kupima tanzania yetu ya leo na kesho itatupa mwelekeo kujua hatua inayofuata. ASANTE, MUNGU ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 12, 2010

    Za leo wadau, kwa sisi tunaotegemea TBC kuangalia Kombe la Dunia, jana ilikuwa shubili, kama mkutano wa Chama ungeendelea ingekula kwetu.
    Maoni yangu, mashindano makubwa kama haya yawe yanaonyeshwa kupitia TV mbalimbali, Tv nyingine za bongo mnafanya nini? Nendeni na wakati kama hamuwezi fungeni vituo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...