Ofisi ya Makamu wa Rais imegawa kompyuta sita zitakazotumika katika upashanaji wa taarifa za masuala ya matumizi salama ya baiteknolojia ya kisasa kwa njia ya mtandao, kwa wizara na taasisi za serikali leo jijini Dar es Salaam.
Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk Julius Ningu ambapo alisema kuwa, Tanzania ikiwa mojawapo ya nchi iliyoridhia itifaki ya Cartagena inayohusu Mazingira salama dhidi ya athari za Baiteknolija ya kisasa, ambayo inalenga zaidi kusimamia matumizi salama ya baiteknolojia ya kisasa, na vile vile ni njia muhimu ya kuboresha maisha ya binadamu hususan kwa kusimamia uzalishaji salama viwandani, chakula, kilimo na kuboresha afya ya binadam kwa ujumla.
Dk. Ningu ameeleza kuwa kompyuta hizo sita zimekabidhiwa kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,Taasisi ya utafiti wa Kilimo ikocheni,Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha kilimo cha Sokoine (SUA).
Ameongeza kuwa Kompyuta hizo zimegharimu kiasi cha shilingi milioni kumi na mbili za Tanzania na mradi huo umetekelezwa chini ya ufadhili wa mfuko wa Mazingira wa Dunia kupitia Shirika la umoja wa mataifa linaloshugulikia mazingira (UNEP/GEF)
Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk Julius Ningu ambapo alisema kuwa, Tanzania ikiwa mojawapo ya nchi iliyoridhia itifaki ya Cartagena inayohusu Mazingira salama dhidi ya athari za Baiteknolija ya kisasa, ambayo inalenga zaidi kusimamia matumizi salama ya baiteknolojia ya kisasa, na vile vile ni njia muhimu ya kuboresha maisha ya binadamu hususan kwa kusimamia uzalishaji salama viwandani, chakula, kilimo na kuboresha afya ya binadam kwa ujumla.
Dk. Ningu ameeleza kuwa kompyuta hizo sita zimekabidhiwa kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,Taasisi ya utafiti wa Kilimo ikocheni,Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha kilimo cha Sokoine (SUA).
Ameongeza kuwa Kompyuta hizo zimegharimu kiasi cha shilingi milioni kumi na mbili za Tanzania na mradi huo umetekelezwa chini ya ufadhili wa mfuko wa Mazingira wa Dunia kupitia Shirika la umoja wa mataifa linaloshugulikia mazingira (UNEP/GEF)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...