Brand Image Limited pamoja na wadhamini wake, wametangaza leo kuwepo kwa Corporate Golf Day, inayotegemewa kufanyika tarehe 24th September 2010,katika viwanja vya golf vya Gymkhana.

Ikiwa kama kampuni inayojihusisha na masuala ya kukuza Mahusiano ya makampuni mbalimbali kwa kupitia michezona shughuli nyingine mbalimbali, Brand Image inayapatia makampuni binafsi nafasi ya kujenga mahusiano mazuri baina yao, kukuza brand zao pamoja na kupimana nguvu katika mchezo wa golf.

Wazungumzaji katika habari maelezo iliyofanyika jumatano tarehe 15, walikuwa wawakilishi kutoka Pepsi, Ecobank, Harbour View, MGen Insurance, Brand Image, na Gymkhana golf club. Hata hivyo, shughuli hii imeandaliwa na Brand Image na kudhaminiwa na DT Dobie, Stanbic Bank, TBL, PEPSI SBC, Harbour View, MGen Insurance, Zantel, Aggrey & Clifford, CHOICE FM, Vodacom, The Citizen, Standard Chartered Plc, Precision Air, Tanzania Distillers Limited, Ecobank na Clouds FM;

Wawakilishi kutoka Gymkhana Golf Club waliwashukuru sana Brand Image Ltd kwa kuwaunga mkono katika kazi zao, na wakatoa changamoto kwa makampuni mengine kuungana na kampuni hii ya Brand Image katika kukuza na kuendeleza michezo Tanzania.

Mchezo huu wa Corporate Golf utafanyika katika viwanja vya Gymkhana, siku ya Ijumaa tarehe 24th September 2010, kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa nne usiku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. all the best, what a great way to network. Way to go...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...