JK akimnadi mgombea ubunge wa CCM kiti cha Korogwe Vijijini Bw. Stephen Ngonyani maarufu kama Profesa Maji Marefu mchana huu katika kijiji cha Mashewa kilichoko Korogwe vijijini
Bango la Profesa Maji Marefu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. we michu si huyu si ni mganga wa kienyeji au? kikwete kweli ananetwork tanzania hii ingawa mbabaishaji tu

    ReplyDelete
  2. Kazi kwelikweli mpaka wagangawa kienyeji kugombea ubunge hii kali

    ReplyDelete
  3. huyu si mchawi jamani huyu au?waganga wa kienyeji nao wanaingia serikalini,nahisi huko bungeni ni ndumba kwenda mbele...michuzi usiibane hii sijatukana wala sijasema ktu kibaya maana wewe na ccm......utamalizia mwenyewe

    ReplyDelete
  4. Duh...Hadi Profesa Maji Marefu..mwaka huu Bongo si mchezo..Game sasa ni kwenye ulingo wa Siasa na kila Mtanzania anayo haki yakuongoza..uwezo wa kuongoza mbele kwa mbele...

    ReplyDelete
  5. MMMH! BUNGE LA 2011 NAKUENDELEA KIBOKO. ANONY.

    ReplyDelete
  6. Safi sana. Dokta anamuunga mkono Profesa.

    ReplyDelete
  7. Maji Marefu!! huyu ni yule mganga wa dawa za asili au?

    Kama ni yeye basi, bunge la Tanzania litakuwa la aina yake. Kutoka miti shamba mpaka ubunge.

    ReplyDelete
  8. hivi huyu mganga wa jadi aliishia wapi? hadi kwenye siasa lazima kafulia

    ReplyDelete
  9. plofesa Maji Malefu atatusaidia sana kule bungeni mana unajuwa siku izi wapinzani wanawachezeya sana wabunge wetu, na shehe yahaya apewe ubunge wakuteriwa tuwone kama wateenderea na mchezo wao, wabunge wetu awaongei sana bungeni sababu wapinzani wanachezea midomo.
    mbunge wetu akitaka kuhuliza swari anasaau anahongea upuhuzi

    kidumu

    ReplyDelete
  10. Bwana michuzi mimi naona wewe ndiye unayetoa comment , yani wanaotoa comment jamani waweke na contact zao nitafurahi kuwasiliana nao, kama anonymous uliyesema : Safi sana.Dokta anamuunga mkono Profesa.

    ReplyDelete
  11. CCM WAMEZIDI KUWEKA WATU WATATA MNO KWENYE CHAMA. HADI WAGANGA WA KIENYEJI?? NDIO MAANA KIKWETE ANAANGUKAANGUKA SOMETIMES. INAWEZEKANA NI LAANA KUTOKA KWA MUNGU HIZO.

    ReplyDelete
  12. ngonyani na korogwe wapi na wapi jamani mhh kali sasa

    ReplyDelete
  13. JAMANI PROFESA MAJI MAREFU AMEWABWAGA WAKINA DR. EDMUND MDOLWA; LUPATU ETC; NI MOTO WA KUOTEA MBALI.

    ReplyDelete
  14. Wahaya kwa nini h- zinawashinda sana? Yaani huyu anony wa Mon Sept. 13, 06:13:00 PM amehangaika wee mpaka ujumbu haueleweki. Eti:

    "mbunge wetu hakitaka kuhuliza swari anasaau anahongea upuhuzi"

    Mnaniudhi sana

    ReplyDelete
  15. na wewe mbona umeandika ujumbu badala ya ujumbe? na wewe kabila lako......? Turudi kwenye mada kuanzia leo sitaki tena siasa za bongo, kama kila mtu anaweza kuwa mheshimiwa. Hebu nijinyanyulie baksi zangu mie nisijepigwa kipapai bure

    ReplyDelete
  16. Na wewe mbona umeandika baksi badala ya boksi

    ReplyDelete
  17. NAONA WAPIGA BOKSI MNAPAMBANA KWA UFASAHA WA LUGHA.......!!! SAFI SANA!

    ReplyDelete
  18. Maji Marefu ni msanii kaona bungeni kuna deal na wala PCB haifanyi kazi na ana uhakika wa kupata uwaziri, kwanini asijiingize?? Poa tu katiba inasema kila mtanzania mwenye akili timamu anaweza kuwa mbunge mradi awe mkulima ama mfanyakazi.

    Nadhani inabidi tubadilishe katiba tuwaruhusu hata vichaa kugombea labda tutakuwa na bunge lenye nguvu.

    Hongera Maji Marefu Vulata yu nyuma yako soon ataingia Chadema ama TLP kugombea ubunge.

    ReplyDelete
  19. Ha ha ha !!
    Nyie wabeba maboksi acheni hizo!
    Huku bongo ni kipapai kwa kwenda mbele, asiye na kibuyu anabeba kifuu siku hizi.
    Na hebu mcheki mkuu alivyokaa kimachale na huyo Maji Marefu!!
    Haanguki mtu hapa!!

    ReplyDelete
  20. "Ngonyani na Korogwe wapi na wapi" Sijui unamaanisha nini. Lakini kama unamaanisha ninachofikiri naomba nikusihi uachane na mawazo hasi. Tanzania hakuna ukabila. Mtu anaweza kugombea cheo chochote popote aishipo ndani ya Tanzania ili mradi ni raia halali wa Jamhuri ya Muungano.

    ReplyDelete
  21. Kaka Michuzi mbona naona habari za CCM tuu.
    Mimi nipo hapa Texas na huwa napenda hii blog kwani inatupa habari za nyumbani.
    Habari za leo zimekuwa kuhusu chama tawala tuu, naiuliza kumetokea nini.

    ReplyDelete
  22. Kaka imekuwaje mbona leo ni bari za chama tawala tuu. Mimi nipo hapa Texas napiga box na huwa napenda kujua habari za nyumbani bila upendeleo. Pls tunaomba utujulishe kama hii tovuti imekuwa ya CCM.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...