




kwa picha zaidi
BOFYA HAPA
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Maskini dada zangu!! Hivi mtaendelea kutumika kama 'property" hadi lini?? Hayo maumbo na maungo yenu mazuri ni kwa ajili ya kuburudushana vyumbani na sio kuuzia vinywaji au vitu vingine.
ReplyDeleteKama mnataka kuweza kisawasawa kataeni kutumika kama vyombo, huu ni udhalilishaji.
Mmmoja mmoja anayejisikia vizuri kuchojoa mbele ya kadamnasi (kama mwanamziki mmoja huko duniani) ruksa. lakini sio kujianika bila ridhaa yenu.
Na sehemu nyingine za mwili ni vizuri zikabaki kwenye uficho, kuonekana tu kwa mmoja mmoja unayemruhusu kufika hizo sehemu za mwili.
Kumbe dini fulani hazikukosea kuweka sheria kali!!
Couldn't you wait for Ramadhan to end you Kaafirs?
ReplyDelete'Salaa' 'Leyku'
ReplyDeleteduh mamiss wa mwaka huu wana miguuu mapedeje roho zinawatoka na hivi walivovalishwa lingerie? yani ......
ReplyDeleteMiguu jamani! Da! Niko hoi kabisa; yaani kwishne
ReplyDeleteKama wameamua kutumika kama ambavyo baadhi wanasema hapa, ni wao. Kuna tofauti gani kati ya hilo na wanaume wanaotumika kutangaza pombe au sigara? Kama hupendi kinachofanywa hapa kumtafuta Miss Redds, USIANGALIE HIZO PICHA ZAO. Bila shaka sirini umependa hiyo miguu na mapaja, lakini hadharani unajifanya mkali. Typical African. Kujifanya wakali kukemea hili na lile wakati ndio wa kwanza kuwa na nyumba ndogo, na kulala na wanafunzi wa kike. Jiulizeni swali hili? Kwa nini magonjwa ya zinaa ni mengi zaidi Afrika kuliko sehemu nyingine duniani pamoja na ukali wote? Kujidai mna maadili na heshima wakati ni wanafiki na wazinzi wakubwa nyie.
ReplyDeleteUMODO NDO AJIRA PEKEE KWA WALIOSHINDWA SHULE BONGO !! WAKALE WAPI ?
ReplyDeleteNakubaliana na Anon wa Sat Sep 04, 09:46:00 PM. Wengi wanajidai kupinga lakini hawako wazi: wanatamani na wanafanya. Vile vile tuko kwenye utandawazi kazi si ofisini tu. Modelling, fashion na advertising ni KAZI na inakuja juu bongo. Cha maana tu ni kwamba kina dada wanaoingia kwenye fani hiyo WAJIHESHIMU. Kushiriki kwenye shoo si kwamba mtu hana maadili. Kuna watu wako maofisini na kazi zao za maana tu lakini machangu kichizi, kisiri siri. Na ndio mana huko huko kwenye maofisi ya hadhi kila siku WAMAWAKE KWA WAMAUME wanazikwa kwa UKIMWI!! Ulaya na US amapo mambo haya yako wazi rate ya UKIMWI iko chini. Hiki ni kielelezo cha unafiki wetu...
ReplyDeleteHivi karibuni blog hii ilichapisha picha za dada na kaka zetu waliokuwa katika hafla fulani. Kina dada walikuwa wamevaa nguo za heshima kabisa. Cha ajabu comments nyingi ziliwatukana kina dada hao kwa kuvaa mavazi ya heshima. Swali langu ni simple kabisa: mbona hao watukanaji wamenyamaza wakiona wasichana wa kitanzania wakianika mapaja yao hadharani? Au huu ndio "utamaduni" wa Mtanzania? Tuacheni double standards.
ReplyDeletePoleni dada zangu kwa kudhalilishwa. J. Bosco. M. Chang'ombe.
ReplyDeleteDAH WATOTO WAZURI,....MIILI INANYAMA YA WASTANI...I LOVE U BABIES....MNAOJIFANYA MMECHUKIZWA WACHENI UNAFIKI...UREMBO NI FANI NA TUTAJUAJE KAMA NI WAREMBO LAZIMA WATUONYESHE KAZI ALIYOFANYA MUUMBA...C'MON!KAMA KAWAIDA NITAWATEMBELEA ,NA MAMBO YETU YALE...WATAKAOPENDA,NITAWAPA AJIRA KWANGU KAMA KAWAIDA
ReplyDeletechaos
Jamani me mwenzenu humu ndo nitakamokufia humu!
ReplyDeletewe anony wa 6 una ufinyu? hao wanaume wanaotangazaga pombe wanavaaga chupi na kuacha vifua wazi na nanii??acha utumwa wa akili, Mungu alituumba kwa makusudi, kwa kiburi chetu twasahau kuwa anaweza kutuchukua wakati wowote. tutunze thamani ya utu wetu. wasichana hawa wanatia mpaka huruma. hata hawajitambui, kesho tangazo likisema wavue chupi waweke kichwani watafanya hivyo, halafu itakuwa nini?wako kazini??utumwa huu wa mawazo. urembo haupo katika utupu.
ReplyDeleteyalabi toba
ReplyDelete