Mchezaji wa timu ya Yanga, Nurdin Bakari ( kulia) akijaribu kumtoka beki mmoja wa timu ya Maji Maji ya Mjini Songea katika mchezo uliofanyika leo kwenye uwanja wa Jamhuri wa Mjini Morogoro, ambapo Yanga ilishinda bao 1-0.
Mchezaji wa Yanga, Jeryson Tegeta, akiwa amekaa katika mstari wa goli la Maji Maji baada ya kukosa bao la wazi kati ya matatu aliyokosa kipindi cha kwanza , kabla ya kufuga bao pekee dakika ya 67 dhidi ya wana lizombe ya Songea , katika mchezo uliofanyika leo kwenye uwanja wa Jamhuri wa mjini Morogoro.
Waamuzi wa mchezo kati ya Yanga na Maji Maji wakiwa wamejipanga tayari kwa kuanza kazi ya kuchezesha mchezo wa timu hizo, huku vijana wa Maji Maji wakiweka mduara kuomba dua ili washinde mchezo huo , hata hivyo timu hiyo ilifungwa bao 1-0 katika mchezo uliofanyika leo kwenye uwanja wa Jamhuri wa mjini Morogoro.
Kocha Mkuu wa Timu ya Yanga, Msebia, Kostadin Papic ( wa kwanza kulia) akitafakari jinsi ya kuwapatia maelekezo wachezaji wake ili kufanikisha ushindi dhidi ya timu ya Maji Maji ya Songea kabla ya mapunziko, hata hivyo Yanga ilishinda bao 1-0 katika mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri, leo mjini Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. tutaendelea kweli ebu ona bechi la ufundi walipo kalia !! 2010 bado tuna kalia viti vya soda !! ahhahahhahhahaha ahhahhaahhhhhhhhhhhh

    ReplyDelete
  2. Uncle Mithupu nimekustukia ndugu yangu wewe ni Wanajangwani maana kila wiki unatoa habari zao tu utafikiri ndiyo timu pekee Bongo.....

    ReplyDelete
  3. Uwanja unatia aibu kwa kweli.

    ReplyDelete
  4. Kwa kweli uwanja unatia aibu maana una mabonde utadhani uko katika kilimo cha viazi. ila nawapongeza wachezaji na benchi la ufundi kwa ushindi wa mechi ya majimaji. maana imezidi kuleta uhai kwenye timu ya wazalendo. sasa pole zao kwa hao waliochukua kichapo na timu iliyopigwa na Yanga. walicheka sana ilipopatikana droo sasa wao wamekula kichapo saaaaaafi!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...