Habari za kazi wadau,

Natumaini mtakuwa mnawajua vijana wa Mapacha Wa3 ambao ni Khalid Chuma a.k.a Chokoraa, Kalala Hamza a.k.a Kalala Junior wote kutoka bendi ya Twanga Pepeta na mimi mwenyewe Joseph Mponezya a.k.a Jose Mara wa FM Academia Tunatarajia kuzindua album yetu ya kwanza iitwayo "Jasho la Mtu" Album itazinduliwa tarehe 15 Octoba 2010 katika ukumbi wa Travertine - Magomeni kuanzia saa 3 usiku kwa kiingilio cha Tshs. 10,000/- tu.

pia tutasindikizwa na The African Stars (Twanga Pepeta) Full squad na Mfalme wa Taarab nchini Mzee Yusuf.

Naombeni msaada wenu wa kunitangazia kwenye blog zenu.

Shukrani.

Jose Mara

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Jose, big up kijana. Nyie ndiyo wanamuziki wa kweli, tunataka ku-support wanamuziki wa kibongo na si wa kifleva. Nawatakia kila la kheri katika uzinduzi wenu. Big up ile mbaya.

    ReplyDelete
  2. Jose Mara
    Hongereni sana. Kazeni buti tu mtavuna yaliyo mema.


    Rafiki-Abu wa Namanga,
    mdau wa Uholanzi.

    ReplyDelete
  3. YONNA JUNIOROctober 14, 2010

    NYINYI MAPACHA SINA ROHO MBAYA LAKINI MNAPOTEZA MUDA MWINGI MZIKI HAULIPI HIVYO MNAVYO FIKIRI MNAPOTEZA MUDA SANA KUNA VYUO VINGI SANA TANZANIA SASA HIVI JARIBUNI KWENDA KUJIPATIA ELIMU LAKINI BILA HIVYO HAMFIKI MBALI ANGALIA WALIOWATANGULIA KINA REMMY MAKASSY NA WENGINE WENGI HAKUNA WALICHO PATA NI KUPOTEZA MUDA WA BULE NENDENI DARASANI HUU NI USHAURI WA BURE, ACHENI UOGA WA KUSOMA ANGALIENNI WAKE MARAFIKI NDUGU NA JAMAA WALIOSOMA WANAVYO KULA NCHI JIFUNZENI KWA MAKOSA YA WENGINE SHULE INALIPA MAPACHA WATATU

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...